Balozi Hassan Simba: Wizara ya Mambo ya Afrika Mashariki ijitegemee ili kukidhi mahitaji ya sasa ya Jumuiya hii

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akipokea ripoti ya Kamati Kutathmini Ufanisi na utendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki leo tarehe 12 Oktoba, 2023 Ikulu jijini Dar es Salaam.


Akisoma mapendekezo ya Kamati ya Kutathmini Ufanisi na utendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mwenyekiti wa kamati hiyo Balozi Hassan Simba Yahya amesema Majukumu ya utangamano wa Afrika Mashariki yahamishwe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, na iundwe wizara kamili itakayoshughulikia masuala ya Afrika Mashariki.

Ushauri huu umetolewa ili kuongeza usimamizi madhubuti wa Maslahi ya Tanzania kwenye Jumuiya hii, Ongezeko la idadi ya wanachama wa jumuia hiyo huku nyingi zikiwa na matarajio makubwa ya mchango wa Tanzania katika mstakabali wa jumuiya hiyo, kukua kwa uchumi wa nchi wanachama pamoja na kuenzi heshima ya Tanzania ya kuwa makao makuu ya umoja huu.

Majukumu mengine ya utangamano yataendelea kusimamiwa na Wizara ya Mambo ya nje.

Aidha, kamati imeshauri kuhamisha kwa muda majukumu ya Wizara ya Mambo ya nje kuwa chini ya ofisi ya Rais kama hatua ya mpito ili ijengwe upya pamoja na kubadili jina la wizara kuwa Wizara ya Ushirikiano wa Kimataifa (Ministry of International Cooperation) ili kuaksi azma ya Serikali ya kutumia diplomasia ya uchumi katika kujenga ushirikiano wa kimataifa. Jina la "Mambo ya nje" haliakisi vizuri majukumu ya wizara.

Pia, Kamati imeshauri kuwa na stability ya viongozi kwenye wizara hii.
 
Kamati ya kutazama upya sera na utendaji wa wizara

Rais Samia Aunda Kamati Ya Kutathmini Utendaji Kazi Wa Wizara Ya Mambo Ya Nje​

MARCH 29, 2023
samia-pc-data.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameunda Kamati kwa ajili ya kutathmini utendaji kazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ili kuiwezesha Wizara hiyo kutekeleza malengo ya Serikali katika kukuza diplomasia ya uchumi na ushirikiano wa kimataifa.

Ili kutekeleza azma hiyo Dkt Samia amemteua Balozi Yahya Simba, aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Zambia kuwa Mwenyekiti wa Kamati.

Aidha, Rais Samia amewateua wafuatao kuwa wajumbe wa Kamati:

1) Balozi Ramadhan Mwombe Mwinyi, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar, Mstaafu;

2) Balozi Dkt. Mwanaidi Sinare Maajar, aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza;

3) Balozi Peter Allan Kallaghe, aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza;

4) Balozi Tovako Nathaniel Manongi, aliyekuwa Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa New York, Marekani.

Kamati hiyo itazinduliwa rasmi tarehe 31 Machi, 2023 Ikulu Dar es Salaam, saa 08:30 mchana.
 
Sio kila MTU ni wa kupewa wizara yoyote ile.
Bado Tena kwenye wizara ya fedha, Rais unda kamati hapo
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akipokea ripoti ya Kamati Kutathmini Ufanisi na utendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki leo tarehe 12 Oktoba, 2023 Ikulu jijini Dar es Salaam.


Pia, Kamati imeshauri kuwa na stability ya viongozi kwenye wizara hii.
Kwenye jina la wizara sawa kabisa na mgawanyo wa wizar. Pia
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akipokea ripoti ya Kamati Kutathmini Ufanisi na utendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki leo tarehe 12 Oktoba, 2023 Ikulu jijini Dar es Salaam.
Naunga mkono hoja
P
 
Siungi mkono badala yake kama Kuna huo uhitaji basi Wizara ya Nje iwe na manaibu Waziri mmja ashughulike na Afrika Mashariki na iwe na vitengi vyake ndani ya Wizara mama.

Ni muhimu sana Kwa sababu Kwa Sasa tunahitaji masoko ya majirani kuanzia Sudan,Ethiopia hadi DRC.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akipokea ripoti ya Kamati Kutathmini Ufanisi na utendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki leo tarehe 12 Oktoba, 2023 Ikulu jijini Dar es Salaam.

na
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom