Waziri Makamba aapa rasmi kuwa Mjumbe wa Bunge la Afrika Mashariki

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,813
11,991
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Yusuph Makamba amekula kiapo cha kuwa mjumbe rasmi wa maamuzi (ex-officio members) wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) katika hafla fupi iliyofanyika kwa njia ya mtandao tarehe 19 Septemba 2023 akiwa katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Kiapo hicho kilichoshuhudiwa na Spika wa Bunge hilo Mhe. Joseph Ntakirutimana kimefanyika kukidhi matakwa ya kanuni namba 5(4) na 9(2) ya kiambatisho cha 10, za uendeshaji wa shughuli za kila siku za EALA. Ambapo, kanuni ya 5 (4) inaeleza kuwa mjumbe rasmi wa maamuzi anaweza tu kuketi katika Bunge hilo baada ya kula kiapo cha Utii kwa Mkataba wa Uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki

EALA inajumuisha wajumbe (Wabunge) tisa (9) wa kuchaguliwa kutoka kila nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Waziri na/au Naibu Waziri mmoja kutoka nchi Wanachama wanaosimamia masuala ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki limeanzishwa kwa mujibu wa Ibara ya 9 ya Mkataba wa Uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ambapo jukumu la msingi la chombo hicho cha uwakilishi ni kutunga sheria za Jumuiya na kusimamia majukumu ya Sekretariati katika kutimiza malengo ya Jumuiya.
 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Yusuph Makamba amekula kiapo cha kuwa mjumbe rasmi wa maamuzi (ex-officio members) wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) katika hafla fupi iliyofanyika kwa njia ya mtandao tarehe 19 Septemba 2023 akiwa katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Kiapo hicho kilichoshuhudiwa na Spika wa Bunge hilo Mhe. Joseph Ntakirutimana kimefanyika kukidhi matakwa ya kanuni namba 5(4) na 9(2) ya kiambatisho cha 10, za uendeshaji wa shughuli za kila siku za EALA. Ambapo, kanuni ya 5 (4) inaeleza kuwa mjumbe rasmi wa maamuzi anaweza tu kuketi katika Bunge hilo baada ya kula kiapo cha Utii kwa Mkataba wa Uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki

EALA inajumuisha wajumbe (Wabunge) tisa (9) wa kuchaguliwa kutoka kila nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Waziri na/au Naibu Waziri mmoja kutoka nchi Wanachama wanaosimamia masuala ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki limeanzishwa kwa mujibu wa Ibara ya 9 ya Mkataba wa Uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ambapo jukumu la msingi la chombo hicho cha uwakilishi ni kutunga sheria za Jumuiya na kusimamia majukumu ya Sekretariati katika kutimiza malengo ya Jumuiya.
Naona akiapa kwa msaafu hapo....baada ya Samia ni zamu ya mkristo
Full stop.
 
Back
Top Bottom