BAKWATA ni Tawi la CCM, iliundwa baada ya kuvunjwa EAST AFRICA MUSLIMS WELFARE SOCIETY ambayo hii ndo ilikua kwa ajili ya waislam wote.
We siku zote hoja yako ni hiyo tena Dhaifu saana.
Society unayoingolea ni kwa Ajili ya East Africa ni sawa na useme CAF na TFF.
Ikifa CAF,TFF itaendelea kuwepo.
Huwezi kusema kwamba TFF isiwepo itegemee CAF,sasa ndani ya nchi chombo gani kitasimamia utendaji.
Hapa kuna watu wanataka tu Kupotosha Watu.
Haiwezekani kuigeuza Tanzania kuwa Dola ya Kiislam hata siku moja,kama baadhi ya Wanaojiita Waislam michepuko.
Uislam ni dini inayojitanua yenyewe bila machafuko wala nini,na ina njia zake za amani.Ila watu wanaona hoja ya kupinga kila kitu kwao ndio njia ya kujitanua.
Leo hii kuna Wajinga wanasema ISI ni sehem ya Wamarekani,we unaona hii Akili ya mtu haswaa?
Yaani Watu wao kwa wao wanapigana halafu mtu anakuambia eti fulani ndio anachonganisha,sasa wewe kama Muislam kweli huna akili?huoni tabu kuuwa Waislam wenzio?huoni Tabu kuuwa watoto wa kiislam?Kisa unasema unaeneza dini.Unanunuliwa kwa hela ili Utoe uhai wako na wenzio?
Hii akili ni ya kipumbavu sana,na mbaya zaidi wapo wanaofadhiliwa kwa kupewa pesa na kuwarubuni waislam michepuko kama hawa.
Wewe Chombo kama BAKWATA,ambacho hadi makao makuu ya Uislam Saudia ndio kinatambulika,na kila nchi inachombo chake cha Kushughulikia Waislam wa nchi husika,hizo Nchi za Africa Mashariki zoote zina vyombo vyao.
na Vyombo hivi ndio pekee vyenye kupata mialiko ya mikutano mikuu ya Kiislam kwenye Mamlaka ya Saudi kama Makao Makuu.
Hao wanaosema BAKWATA ipo ki CCM,ni wale wanaotaka kwamba iwe inasaidia harakati za uhasama.
Na ndio hao wanaosema kwamba BAKWATA in mfumo Kristo,sasa hii akili kweli.
Ila Wasiwape tabu sana,Sie ndani ya Uislam tunawajua hao,ndio wale wanaomwagia Tindikali Maaskofu,wanaochoma makanisa nk.Ikitokea kwao watasema mpaka povu la kule litoke.
Sasa wanataka wapate nafasi ili wahakikishe kwamba Ukristo unaondoka Tanzania kwa njia hii ya vurugu.
Wanajidanganya saana,na wanapotosha sana UISLAM,uislam ni dini ya amani.
We mtu anasema eti Waislam wamenyiwa elim,huu si wendawazim?
Ulikatazwa kwenda shule?na hii mentality imekaa kwa baadhi ya Waislam michepuko mpaka leo na vizazi vyao vikiamini hivyo.
Mbona viongozi wakuu wengi ni Waislam na Wakristo hawa reiz issue ya udini?
Tuache kulalamika.
Wenzetu wakristo wakijenga Kanisa,basi pembeni kuna Shule au Zahati.Sie tukijenga Msikitini pembeni tunaweka Maduka.
We unategemea nini hapo.
Wakristo wakienda Kanisani Jpili,sadaka mtu anatoa kwa moyo mmoja na sala moja ni mamilioni ya pesa
Sie ukienda Kusali Ijumaa msiikiti umejaa,mtu anatoa coins za miambili,na tajiri unamuona anatoa elfu mbili saana katoa elfu tano.
We unategemea mtakuwa sawa?
Sasa mchawi sio Ukristo,wala CCM.Mchawi ni Waislam Michepuko.
Na pia niweke wazi hili,Nchi zoote za Kiislam,Mabaraza yake yote yapi chini ya Serikali.
Kwa sie tuliesoma Uganda ni kwamba kuna Kipindi Museven akitaka kupitisha Sheria kadhaa anaita viongozi wa dini husika hasa kupitia Taasis Kuu ya Waislam nchi mwake pale anapoona kuna muingiliano fulani ili kuweka sawa.
We kuna Taasisi ipi ambayo haina usajili wa Serikali.Hahahah aisee watu akili za ajabu kweli.
Labda niweke wazi hapa.
Wanaoichukia BAKWATA ni maadui wakubwa saana wa Ukristo na Wakristo ila wanapenda kutumia kivuli cha kusema BAKWATA ni sehem ya CCM au tawi la Kanisa.
Watapindua maneno eee lakini dhamira yao ni moja tu
Na ndio maana nawauliza hivi nyie mnachuki na wakrsito,mbona kiongozi wetu Mtume Mohammad(S.A.W) alieneza dini kwa amani na watu hao alikuwa nao karibu sana.Ili ueneze dini ni lazima uwe karibu saana na yule asie dini yako ili iwe rahisi sana kumshawishi abadilishe dini,anaweza kuvutiwa na mwenendo wako kisha akaona Uislam ndio dini ya kufuata.Lakini leo anaona watu mnauwana nyie kwa nyie,Taasisi yenu ya Dini hamuitaki.Chuki dhini ya Ukristo ipo juu.Nani atakubali.
Na wakati huo wapo Viongozi au Maswahaba wa Mtume Mohammad(S.A.W) ambao baba zao walikuwa Wakristo.Ila mbona walikuwa wanaishi nyumba moja,wanakula pamoja.Na wengi wao walibadilisha dini kuwa waislam baada ya kuona mwenendo mzuri wa Uislam na wala hawakutengana eti kisa Dini.
Sasa kama ingekuwa ni uadui huu basi hata wao Vingozi wetu wa enzi hizo za Mitume wangefukuza hadi wazazi wao waliokuwa wakristo.
Vita ilitokea tu pale ambapo mhusika kaja rasmi kwa vita,ila vita ya maneno ilimalizwa kwa maneno ya hekma na kueleweshana.
Msipotoshe watu juu ya chuki zenu kwa Ukristo,fuateni Qur`aan,na sio kufuata mkumbo tu ya chuki za dini.
Kama wewe Muislam na Muumini wa kweli,basi mwenendo wako uwe mwema ili umshawishi Mkristo aingie kwenye Uislam.
Njia hizo zimewashinda kwa kuwa wengi Dini wamevamia kusoma kijuu juu,na pia njaa ndio inawamaliza na kuona kwamba wakiwa na misimamo fulani basi kuna makundi yatawapa misaada.Huu upuuuuzi ,mtupu.Usiuze utu wako kwa Pesa