BAKWATA mnayajua mateso ya mwanamke akiolewa katika umri mdogo?

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,194
4,116
Wakati Dunia ikiwa inaendelea kupigana vita ili kumuokoa mtoto wa kike kutoka kwenye kitanzi cha ndoa za utotoni BAKATWA wamemekuja na kauli yao ya kupinga kuondolea kwa sheria ya ndoa inayoruhusu mtoto wa miaka 14 kuolewa kwa ridhaa ya wazazi wake.

Ajabu ni kwamba wao wameongza kuwa mtoto wa kuanzia umri wa miaka 11. 12, 13, 14, anaweza kuolea iwapo mzazi ameridhia na mahakama pia kwa kuangalia mazingira ya mtoto kama hasomi na tayari kavunja ungo.

Kila siku Serikali ya Tanzania na na wadau wa elimu wanapigia kelele watoto wa kike wapate elimu, waweze kuondokana na ujinga ili kujikwamua kimaisha na lakini nyie BAKWATA mnataka akaolewe ili azidi kuwa tegemezi na baadae aonekane mzigo kwenye ndoa asiyeweza kuwa na msaada wowote kwa familia yake kiuchumi wala kwake mwenyewe.

Nawauliza BAKWATA kabla ya kuwaza upande 1 tu kuwa akivunja ungo basi anafaa kuwa mke, hamkuwaza kuwa kuvunja ungo ni hatua za ukuaji anazopitia mwanamke katika kuelekea kukomaa? Hamjui kuwa kabla ya ungo huanza kuota matiti nk? Au hata wao waolewe maana tayari wanaonekana wamekua? Tayari kavunja ungo ndio je, akili yake imekomaa kuweza kutambua kuwa ni mtu mzima mwenye jukumu la kulea mme na familia kwa ujumla, au kuweza kulelewa na mme kama mke au nyie mnajua ndoa ni kuingiliana kimwili tu na kupata mimba basi?

Hivi mnajua changamoto za mimba za utototni wakati wa kujifungua? Au hao wanaume mnaowataka kuoa watoto wadogo mtawazuia kuwapa ujauzito hadi wafikishe mri unashauriwa na wataalamu wa afya wa angalau miaka 20 ndio mtu aweze kubeba ujauzito wa kwanza?

Vipi kuhusu kumpa mtoto majukumu ya kuwa mama wa mtoto hali ya kuwa yeye mwenyewe anatamani kucheza na watoto wenzake? Maswali ni mengi sana natamani kuwauliza na najaribu kufikiria kwa nini mmeweza kuongea swala la aibu na hili tena kwa ujasiri na bila kuona aibu?

Natamani mnioneshe watoto wenu wenye umri wa miaka 11, 12, 13, 14 mliowaozesha kwa wanaume na namna wanavyoweza kumudu ndoa zao au mnapigia kelel jambo ambalo kwenye familia zenu hamuwezi kuruhusu litokee. Naona mnataka kuleta janga kwa Taifa kwa vifo vya watoto kwa kujifungua na kupigwa kwenye ndoa zao kwa kuchanganya utoto na majukumu ya mazito kuliko umri wao wa ndoa.

Hivi BAKWATA mnajua kuwa wazazi wenye tamaa mkiwapa ruhusa hiyo watawashawishi watoto wao waache shule ili wawaoze kwa wanaume wazazi wapate hela? Au watoto kushawishiwa na wanaume waache shule shule ili wawaoe huku wakiwaahidi zawadi kedekede na watoto hao kuamini ili wapate hivyo vitu.

Inanipa mashaka kila nikiwaza wakati mnakuja na tamko lenu, mlikuwa na hali gani ya kushindwa kujua kuwa ndoa si kuzaa tu au ndoa si suluhisho la binti aliyeacha shule au anayesumbua kmalezi.

Nachokiona, Watoto wataolewa watazaa na kuchokwa na waume zao na kuachwa kisha waje uraiani warudi kuwa mzigo kwa familia zao walikotoka na kuzalisha wamama wanaolea watoto peke yao bila baba eti kisa nyie mnaoshindwa kuona hasara ya uwepo wa ndoa za utotoni.

Nimfiche wapi binti yangu dhidi ya nyie wanaume wenye tamaa na watoto wadogo? Oneni aibu futeni kauli. Ndoa za watoto ni hatari kwa mtoto wa kike na jamii kwa ujumla.

Pia soma:
BAKWATA: Wasichana wa umri wa miaka 14 waendelee kuolewa
 
Kila siku Serikali ya Tanzania na na wadau wa elimu wanapigia kelele watoto wa kike wapate elimu, waweze kuondokana na ujinga ili kujikwamua kimaisha na lakini nyie BAKWATA mnataka akaolewe ili azidi kuwa tegemezi na baadae aonekane mzigo kwenye ndoa asiyeweza kuwa na msaada wowote kwa familia yake kiuchumi wala kwake mwenyewe.
Mleta mada mimi hayo mengine sitakujibu watakuja kukujibu wenye dini yao lakini nataka tuelewane humo niliko-bold,"hakuna mke aliyeolewa na akazaa watoto akawalea huku mumewe ameenda kutafuta ridhiki ya familia akaonekana tegemezi au asiyekuwa na msaada"


Hii kauli huwa ni ya hovyo sana,kitendo cha yeye kuingia labour kukuzalia watoto na kila siku unatoka asubuhi unarudi usiku unakuta ni wazima siyo jambo la kubeza wapeni heshima wake zenu na mke toka mwanzo hakuwekwa awe mtafutaji aliwekwa azae awalee watoto kwa maadili yanayopaswa huku wanaume wakiwa source kuu ya matunzo ya familia.
 
Mleta mada mimi hayo mengine sitakujibu watakuja kukujibu wenye dini yao lakini nataka tuelewane humo niliko-bold,"hakuna mke aliyeolewa na akazaa watoto akawalea huku mumewe ameenda kutafuta ridhiki ya familia akaonekana tegemezi au asiyekuwa na msaada"


Hii kauli huwa ni ya hovyo sana,kitendo cha yeye kuingia labour kukuzalia watoto na kila siku unatoka asubuhi unarudi usiku unakuta no wazima siyo jambo la kubeza wapeni heshima wake zenu na mke toka mwanzo hakuwekwa awe mtafutaji aliwekwa azae awalee watoto kwa maadili yanayopaswa huku wanaume wakiwa source kuu ya matunzo ya familia.
Kinadharia iko ivyo ila kiuhalisia haiko ivyo, ni kweli kazi ya kuzaa na kulea ni kubwa sana tena mno, ila jamii haiitambui na haiipi thamani. Mwanamke anayeweza kuwa na kipato chake ana uhuru wa fikra, na ana uhuru wa kubba wa kubeba majukumu ya familia iwapo huyo mme aidha hayatimizi au hayupo kwa wakati huo

Mfano, kifo, kuachana, mme kawa mgonjwa au kakosa kipato. Ukikutana na mwanamke ambaye hana uwezo wa kuingia hata sh, 1000 anaishi kwa wasiwasi na wengi huishia kuwa wanaficha pesa za chakula ili wapate kujikimu mahitaji madogo ambayo wanaona kazi kuomba kila siku.
 
Unataka wawe malaya wa mitaani?

Hv mfano mabint wa kike wasio endelea na masomo unataka mtaani wafanyaje?
Unahisi suluhisho la umalaya ni kuwaozesha mapema? Vipi ndoa zikiwashinda hawatarudi kuwa malaya na mzigo wa watoto tena wasioweza kuwalea maana hawana elimu wala ujuzi wala kipato chochote.

Kuna elimu ya ufundi wapewe, au wakae wajifunze kujitegemea kwa namna yoyote hata biashara wakati wanasubiria kukoaa zaidi kimwili na kiakili ndoa isiwe suluhisho la mtot asiye soma kwa kuwa ndoa si ajira kwa mtoto wa kike wala mradi.

Kwanza wakati huo hana hata maamuzi ya mwanaume wa aina gani anamtaka, mwisho akikua anagundua sio mwanaume nayemtaka anaweza kuanza kutafuta wa aina anayotaka mje kumuita malaya kumbe alifanya maamuzi ambayo si yake wakati wa utoto.
 
Unataka wawe malaya wa mitaani?

Hv mfano mabint wa kike wasio endelea na masomo unataka mtaani wafanyaje?
Of course dunia ya sasa imekuwa chafu sana inaweza kuwa cha kufanya hawana ila tutambue na tukubaliane mtoto wa miaka 15 kurudi nyuma hawezi kuwa salama mbele ya mwanaume ambaye si mzazi wake au kaka yake.

Nilikuwa nawaza labda aliyetoa hilo wazo angekuja na wazo la kushauri kwamba watafutiwe kitu cha kufanya kitakachozidi kuzikomaza akili zao huku umri wao wa kuolewa ukisogea sogea kidogo.

Though siijui imani yenu inasemaje kuhusu hilo la kuolewa wakiwa bado wadogo sana.
 
Ndio maana ushoga unazidi vijana waoane kijana akishavunja ungo sio mtoto, msichana akishavunja ungo sio mtoto.

Kulingana na imani za dini hatuwezi kufuata matakwa ya ulimwengu bali imani zetu haijalishi nani hapendi kwani dini haipo kumfurahisha mtu yeyote yule.

Hata ukristo hauna umri wa kusema eti miaka 16 ni mtoto miaka 14 ni mtoto. Akishavunja ungo ni mtu mzima tayari . Hivyo ana haki ya kujiamulia , muhimu asilazimishwe.
 
Of course dunia ya sasa imekuwa chafu sana inaweza kuwa cha kufanya hawana ila tutambue na tukubaliane mtoto wa miaka 15 kurudi nyuma hawezi kuwa salama mbele ya mwanaume ambaye si mzazi wake au kaka yake.

Nilikuwa nawaza labda aliyetoa hilo wazo angekuja na wazo la kushauri kwamba watafutiwe kitu cha kufanya kitakachozidi kuzikomaza akili zao huku umri wao wa kuolewa ukisogea sogea kidogo.

Though siijui imani yenu inasemaje kuhusu hilo la kuolewa wakiwa bado wadogo sana.
Mama wa yesu kristo alibeba mimba akiwa na miaka 12.

Acheni siasa kweny mambo ya msingi bint akisha balehe kifuatacho ni ndoa tu kama ataridhia yeye mwenywe kuolewa.

Binafsi siwezi kuowa bint wa abave 16 yrs.
 
Ndio maana ushoga unazidi vijana waoane kijana akishavunja ungo sio mtoto , msichana akishavunja ungo sio mtoto.
Kulingana na imani za dini hatuwezi kufuata matakwa ya ulimwengu bali imani zetu haijalishi nani hapendi kwani dini haipo kumfurahisha mtu yeyote yule.
Hata ukristo hauna umri wa kusema eti miaka 16 ni mtoto miaka 14 ni mtoto. Akishavunja ungo ni mtu mzima tayari . Hivyo ana haki ya kujiamulia , muhimu asilazimishwe
Nimekusoma kichwani nikiwaza ndiyo mimi nimekabidhiwa kabinti aged 12 kadogo dogo mahari nimetoa msahafu na wakati huo nina 30+ nimekomaa haswa halafu nikakapige mpini haka kasichana.

Mzee siyo kuuwa huku kuna ndoa kweli hapo?nadhani hii kitu ina-apply sehemu na sehemu siyo mazingira ya kwetu.
 
Ni basi tu nchi haina waandishi wa maana, alitakiwa atoke mwandishi atengeneze documentary kuhusu hao wajumbe wote na watoto wao, uone kama kuna hata mmoja mwanaye kaolewa below 20!
Uongo mtupu dada zangu wote wameolewa wakiwa chini ya miaka 20 nasasa wote wapo kweny ndoa.

Wengine wanazaidi ya miaka 25 kweny ndoa zao

Huu ujinga wa haki za wanawake sijui haki za kichoko unawavuruga vijana mitaani
 
Mama wa yesu kristo alibeba mimba akiwa na miaka 12.

Acheni siasa kweny mambo ya msingi bint akisha balehe kifuatacho ni ndoa tu kama ataridhia yeye mwenywe kuolewa.

Binafsi siwezi kuowa bint wa abave 16 yrs.
Wewe unaye dada yako wazee wako waliruhusu aolewe akiwa under 16?
 
Wakati Dunia ikiwa inaendelea kupigana vita ili kumuokoa mtoto wa kike kutoka kwenye kitanzi cha ndoa za utotoni BAKATWA wamemekuja na kauli yao ya kupinga kuondolea kwa sheria ya ndoa inayoruhusu mtoto wa miaka 14 kuolewa kwa ridhaa ya wazazi wake.

Ajabu ni kwamba wao wameongza kuwa mtoto wa kuanzia umri wa miaka 11. 12, 13, 14, anaweza kuolea iwapo mzazi amaa na watoto wadogo? Oneni aibu futeni kauli. Ndoa za watoto ni hatari kwa mtoto wa kike na jamii kwa ujumla.
Aliyembebesha Maria mamawa Yesu mimba akiwa na miaka kumi na tatu tena bikra unadhani ni kichaa?
Joseph mume wake alikuwa na miaka 84,kuna cha kujifunza hapa?
 
Kuna ostadhi mmoja kaoa Mtoto mdogo kama miaka 14 au 15,baada ya majirani kuwasema sana amehama mtaaa hata sijui kahamia wapi, ila nasikia kahamia Iringa huko. Yaani Binti mdogo hadi aibu
 
Tunaomba kupata ushahidi wa wajumbe wa Bakwata na wote mmaotetea hoja hii humu ndani mtoe picha za watoto wenu walipokuwa wanafunga ndoa kuanzia miaka 11 hadi 15 ili tupate namna nzuri ya kuwajibu na kuwaelimisha wenzetu walio nje ya Jamii Forum.
 
Ni basi tu nchi haina waandishi wa maana, alitakiwa atoke mwandishi atengeneze documentary kuhusu hao wajumbe wote na watoto wao, uone kama kuna hata mmoja mwanaye kaolewa below 20!
Tunaomba kupata ushahidi wa wajumbe wa Bakwata na wote mmaotetea hoja hii humu ndani mtoe picha za watoto wenu walipokuwa wanafunga ndoa kuanzia miaka 11 hadi 15 ili tupate namna nzuri ya kuwajibu na kuwaelimisha wenzetu walio nje ya Jamii Forum.
 
kutoka nje ya mstari ndio kunawafanya hata mletewe hizi sera za LGBTQ sasa.

Huku mitaani vimejazana vibinti vya under 15 mpaka 20yrs vikahaba vilivyokubuhu. Mbona hatuwasaidii sasa hawa mabinti kwakuwapa ajira au mitaji? mabinti yatima wa umri huo wamejazana mitaani mbona hatuwapi mitaji na ajira wala misaada ya kusoma.? ila kuolewa ndio tunaona shida?
 
binti kamaliza la saba, hasomi na hana wakumsomesha, amevunja ungo tayari amebaki anazagaa zagaa....kama jamii tumechukua hatua gani kusaidia hawa mabinti ambao wamejaa huko uswahilini na matokeo wanapigwa mimba na vijana n kuendeleza umasikini.
 
Back
Top Bottom