BAHIMA Empire na uchaguzi butu 2020

BAHIMA Empire na uchaguzi butu 2020

Nachoweza kusema kwenye uzi huuu,wasiwasi ndio akili.ukaribu wa muhimili uliojichimbia mizizi chini zaidi na kagame ni wa kutiliwa mashaka sanaa.hasa kwa zama hizi za kile kinachitwa vita (hewa )ya kiuchumi.
 
Ni hali ilikuwepo tangu asili, mzungu tusimsingizie sana pamoja na kwamba ana sehemu yake ya lawama... Nijuavyo mini na kwa usahihi kabisa MHUNZI anabaki kuwa MHUNZI kamwe hachangamani na MSUSI... Same applies kwa wakulima na wafugaji! Hizi ni jamii mbili tofauti kabisa.... Sio zile tofauti za kidhana na kimtazamo za CCM na TADEA
[emoji106] [emoji106]
 
Hii kitu siyo conspiracy theories? Ingekuwa hivyo Tanzania ingekuwa kwenye himaya hiyo siku nyingi. Najua ukisema Bahima empire unazungumzia Wahima wa Uganda and their cousins :Watutsi etc. Kuna hofu ipi iliyopo sasa hivi ambayo haikuwahi kiwepo? Vipi watu wenye muingiliano na mwonekano hasa kwa jamii za mpakani hawawezi kutengwa kwa sababu hizi?
Tatizo watu hawasomi history kuelewa migration ya watu na jinsi walivyofikia huko walipo. Watu hawaelewi kuwa wakama au watemi wote wa kanda ya ziwa esp. Kagera, Kigoma, Ukerewe asili yao ni Ankole. Na Ankole yenyewe siyo walikuwa huko kwa karne nyingi bali walikuwa wanamigrate na ng'ombe wao toka East to West. Kuna Nilotes na kuna Ha-mites waliotokea Uhabeshi. Ukiangalia viti vya kifalme wanavyokalia wafalme wa Bukoba vina picha ya Simba ambayo ni emblem ya Simba wa Yuda.
Hawa watu walipohama hawakuhama na lugha zao hivyo kila walipoenda wali assimilate kwenye jamii ila waliwapiga wenyeji na kuwatawala. Ukisikia koo za Wahinda, Wankango, Wami nk. hao ndo watu mnawaongelea. Lakini kuna koo zilizohama nao toka Uganda na wakaweza kutawala kama toka Bunyoro waliweza kutawala Kiziba. Jikumbushe yule aliyekuwa Mkamakazi wa Biharamulo aliyefariki juzi juzi alikuwa ukoo gani? Watu wamekuwa wanahama toka karne ya kumi na tano au kabla na muingiliano ni mkubwa hivyo ukisema oho Kagame oho M7 unajidanganya sababu mtanzania halisi ni yule Mhadzambe, Msandawe wengine sisi wakuja. Wabantu wametokea West Afrika mbona hamlalamiki kuwa nyinyi ni wahamihaji? Wangoni tena hao wamekuja hata baada ya Wahima kutawala lake zone wakati wa vita ya Mfecane mbona hamuwasemi?
 
Ukiangalia sana wachaga wanawaangalia wapare kwa jicho la shaka shaka. Wapare nao walipokuwa kwenye pick wakapeleka umeme mpaka miliman kwao kwa janja janja "enzi za waziri mkuu".

Nao tuwaitaje? Sio wabaguzi na wakabila kama lengo ni kutafuta kabila safi?

Tuache haya mambo ambayo yanaweza kabisa kusambaratisha umoja wetu
 
Ukiangalia sana wachaga wanawaangalia wapare kwa jicho la shaka shaka. Wapare nao walipokuwa kwenye pick wakapeleka umeme mpaka miliman kwao kwa janja janja "enzi za waziri mkuu".

Nao tuwaitaje? Sio wabaguzi na wakabila kama lengo ni kutafuta kabila safi?

Tuache haya mambo ambayo yanaweza kabisa kusambaratisha umoja wetu
Kwanini hii mada imeshindikana kueleweka kabisa? Ishu ya uchaguzi 2020 haijadiliwi tena tumebaki na ukabila
 
Kwanini hii mada imeshindikana kueleweka kabisa? Ishu ya uchaguzi 2020 haijadiliwi tena tumebaki na ukabila
Bahima ni mambo ya kibaguzi. Yana lengo la kumchafua mtu pasipo ushahidi. Hatuna hoja mpaka hizi hoja ambazo ndani zimebeba kabisa sura ya kusambaratishana sababu ya ukanda na ukabila? Kwani wanaotoka kanda ya ziwa ambao wana mahusiano ya kidamu na hao Bahima sio watanzania? Nini kinamfanya mtu awe mtanzania?

Sent from my SM-J700F using JamiiForums mobile app
 
Bahima ni mambo ya kibaguzi. Yana lengo la kumchafua mtu pasipo ushahidi. Hatuna hoja mpaka hizi hoja ambazo ndani zimebeba kabisa sura ya kusambaratishana sababu ya ukanda na ukabila? Kwani wanaotoka kanda ya ziwa ambao wana mahusiano ya kidamu na hao Bahima sio watanzania? Nini kinamfanya mtu awe mtanzania?

Sent from my SM-J700F using JamiiForums mobile app
Mmh umeuelewa kweli muktadha wa mada hii hebu soma tena
 
Back
Top Bottom