Bahari ni kiboko ya usafiri wa wachawi

Bahari ni kiboko ya usafiri wa wachawi

Ziko sehemu mbili. Kuna Bermuda triangle, na dragon's triangle. Bermuda triangle iko kati ya kisiwa cha bermuda ,mji wa Miami ,na San Juan Puerto Rico. Dragon's triangle, iko kati ya mji wa Tokyo, pwani ya kisiwa cha Philippines, na kisiwa cha Wake. Triangle hizi ziko katika 30 degree latitude, maana yake ukiwa Bermuda triangle, upande wa pili wake wa pili wa dunia iko dragon's triangle. Kati ya triangle hizi, dragon's triangle ni mbaya zaidi ya bermuda , tena ni pans zaidi ya ile ya Bermuda, na vile vile huwa inapanuka na kupungua. Inapopanuka huelekea mpaka pwani ya China kuelekea Vietnam. Kumbuka ile ndege ya Malaysia Boeing 737 iliyopotea ikielekea China. Hiyo iliingia katika dragon's triangle.
Hili lina tafsiri hiyo kisayansi lakini kiroho ina maana yake pia
 
Vitu anavyokuwa akiviandika huyu jamaa mnaweza sema ni hadithi za kufikirika ila kama umepata kuishi maisha ya namna hiyo hutakuwa na shaka hata kidogo. Wengi wanaokuwa wanakuwa wanakukejeli na kukukebehi ni watoto wa kuitwa kula na kuondoka mezani. Ila kwa watafutaji na wadukuzi wa mambo haya maswala sio mageni hata kidogo. Nyumbani tuliwahi kuwa tunalindwa na MAJINI, hakuna aliekuwa anaweza kuingia nyumbani mwenye nia chafu, waliwahi kupigwa wezi nyumbani pale na mmoja ni kijana wa jirani yetu. Haya malango ya kuzimu yapo mengi tu hapa Tanzania, mfano Kisiju, ziwa Tanganyika, kuna mto Kigoma karibu na upande wa Burundi kwenye mto Malagarasi huwa kuna maji yanapanda mlima, sio kumwagika kutoka juu kwenda chini. Kuna mambo mengi sana ya ajabu ambayo ukiambiwa huwezi kuyakubali.

Meli ya mv Bukoba walioipindua mwaka 1996, huwa inaonekana mara kadhaa kwa wavuvi wanaovua ziwa Victoria na kuna jamaa niliwahi kusikia ushuhuda wake akikiri kuwa ile kazi yeye ndiye aliyewatuma vijana wake wakaifanye kabla hajaokolewa kutoka humo gizani. Ajali ya Treni ya Dodoma alishiriki moja kwa moja yeye. Vitu usivyovijua usibishe, jipe muda wa kufuatilia uufahamu ukweli ingawa sio lazima ukubali.
[emoji120] [emoji120] [emoji120] [emoji120] [emoji120] [emoji120]
 
Nungwi kuna mkondo unaofanana na wa Bermuda hizo ni njia za kuelekea kuzimu kwenye ufalme wa giza
Ok ni bahari zote chini kuna mfalme wa giza au... Kama ndio inamaana kuna dunia mpya na hawezi kuishi pekeake au sio!
-vip kuhusu bara la Antarctica nasikia kule ndo White House yake ilipo kuna ukwel hapo...
 
Ok ni bahari zote chini kuna mfalme wa giza au... Kama ndio inamaana kuna dunia mpya na hawezi kuishi pekeake au sio!
-vip kuhusu bara la Antarctica nasikia kule ndo White House yake ilipo kuna ukwel hapo...
[emoji3] [emoji3] [emoji3]inawezekana kabisa
 
KENZY nilishawahi kulijibu hili siku za nyuma kwenye nyuzi nyingine pengine hukuona
Ni kwamba niliishi kusoma na kupractice mambo ya kiroho kwa miaka isiyopungua 20.
[emoji15] [emoji15] ulipractice ngoja niandae maswal kitabu
 
Nimejifunza, baadhi nimeyaona na mengine nimeshiriki kwa nia ya kufahamu tuu
Kwenye swala la malango nilisoma articles na vitabu tofauti tofauti wanasem vil viumbe vya ajabu kam reptilians na aliens za Aina tofauti nao wanaishi chini ya bahari na ardhi..kwa hao reptilians wanasema walikwepo kabla ya binadamu na ndio kweny bible wanaitwa Evil serpent na wana miili kama mijusi ya kijani pia eneo wanapoishi kuingia ni ishu sasa basi wanaishi vip na mfalme wa Giza au makazi yao tofauti na mfalme Giza? Au wao ndo watumwa wa mfalme wa giza?
 
Kwenye swala la malango nilisoma articles na vitabu tofauti tofauti wanasem vil viumbe vya ajabu kam reptilians na aliens za Aina tofauti nao wanaishi chini ya bahari na ardhi..kwa hao reptilians wanasema walikwepo kabla ya binadamu na ndio kweny bible wanaitwa Evil serpent na wana miili kama mijusi ya kijani pia eneo wanapoishi kuingia ni ishu sasa basi wanaishi vip na mfalme wa Giza au makazi yao tofauti na mfalme Giza? Au wao ndo watumwa wa mfalme wa giza?
Halafu unajua kwenye Biblia takatifu pale Eden anayetajwa ni serpent sio snake?
 
Back
Top Bottom