Bado, gharama za harusi jamani, tafadhali

Bado, gharama za harusi jamani, tafadhali

Hizo cost naona kama hazina uhalisia kwa jiji la Dar....mfano ukumbi now days, Gari la maharusi,gharama ya suti, upambaji, gauni la bib harusi, MC

Pia cjana Cake hapo....gharama hizo unatafuta stress my frnd.
Asante, sasa Ukumbi wa nafuu hiyo upo hapa sabasaba ndani maonyesho unaitwa Kobe uwezo wa watu 300, gari la maharusi bado nafuatilia the best way, gharama ya suti ipo hivyo nimehakikisha, upambaji ilikuwa niweke hapo ninafanya baargaining na mama mmoja anasema nikitaka best 350,000 lakini 300000 inawezekana, bibi harusi anasema nisijali gauni anapambana kulipata. Keki natumia advantage ya mke wangu mkubwa (mke wa kaka yangu) anafanya kazi hiyo, I will buy materials, she made for her wedding she is going to do it for me too. No stress ndugu yangu, just fighting, asante sana, nimependa hivyo.....
 
hapo bado garama za kuwarudisha wazaz/ndugu mkoan.
Je gest unakaa siku 1 tu
mara nyingi wanywaji wa bia ni wengi kuliko soda, nilitegemea wa bia wawe 100, wa soda 50.

Nakuelewa vema, halafu ndo Babati huko dah, nitaona uwezo wangu juu ya hilo. Wanywaji bia unaweza ona sio wengi kivile ila huwa wanataka bia nyingi hata hao wachache ndio tatizo- tutafanya kulingana na uwezo, nilifika sherehe moja wakaleta mbilimbili each, ikabidi tuagize nje kwa kujigharamia. Thank you
 
Keki kama sijaiona hapo,halafu kuna haya ya kuzingatia:
Ukishaamua kufanya sherehe tena na Brass Band ipo basi ujue lazima cost itaenda juu.
1.Kama ni mapambo ukumbini wengi wanaanza laki 4
2.Music na MC nayo almost laki 4
3.Vinywaji sherehe nyingi wengi wanakunywa bia hata kama hapendi bia watakunywa Grand malt kitu ambacho inarudi kwenye gharama ya bia.
4.Magari kama hutatafuta ya marafiki zako ukae ukijua hizo bei zitapanda.
5.Still picha na moving pamoja huwa inarange laki 3 mpaka 4 na nusu bila projector.
Hii sherehe ukienda ukumbini lazima gharama ile kwako otherwise punguza watu au kafanyie mazingira ambayo hizo kumbi au bar wateja wamepungua basi anaweza kukupa kwa gharama ndogo.
Halafu hapo ukumbini kama vinywaji bei ni ghali,nunua hapo vichache hasa vile vya kopo vingine kanunue mtaani kwenye bei rahisi.Hapo Bar nunua vichache vya sample tu.
Asante kwa concentration: sasa keki nategemea kumtumia shemeji yangu amesomea kazi hiyo na alitengeneza keki nzuri ya harusi yake, nategemea kununua materials. Mapambo kuna mama mmoja bado tunaongea anasema nikitaka best 350000 ila 300000 inawezekana. Muziki na MC bado naongea nae anasema 350,000 shampeni 3 anatoa yeye. Yes wewe ni mtu wa pili juu ya suala la bia kunijuza, unajua tatizo wanywaji wa bia hata kama ni 30 wanaweza hata kumeza sitasita kila mmoja na huwa hawapendi bia mbili sherehe imekwisha, wangependa waendelee sana, kwa kweli tutalizingatia hili kulingana na uwezo. Homa ni magari, najaribu kutafuta namna ya kuto ya commit siku nzima baadhi ya magali hasa costa, yatumike pale tu yanapohitajika, nafahamu menejiment ni ngumu kidogo lakini cost has to speak. Kwenye picha mzee yes yes, muda si mrefu nimehudhuria send off moja walikuwa na projector, binafsi sikuipenda sana, niliona kama concentration imegawanywa, kwenye projector mara waweke matangazo huku shughuli inaendelea bahati mbaya nilikaa kwenye kiti kinachotazama projector ilinibidi muda mwingine kugeuka nyuma kuona nini kinaendelea so, not impressed with it, i dont even care for that, SASA gharama ni kweli nategemea kufika kiasi ulichotaja. Gharama kula kwangu kweli naliona kwa namna yeyote ile, tatizo mimi mwenyewe nina ndugu wengi kweli kweli, nafikiria hilo. Nashukuru kwa ushauri na observation nzuri.
 
Kuhusu gesti 60000 apo umeniacha kidogo mkuu:what:

Kwa kweli, hili hata lisingeonekana hapo kwa sasa, sio mbaya, alifikiriwa zaidi wazazi wa binti toka babati, nafahamu nk watu wasio kupenda kabisa Dar hivyo kimekadiriwa kiasi kidogo hicho
 
Harusi million 4, kweli we umebana vizuri. Hongera. Me najua hiyo million 4 inalipia mapambo tu tena inaweza isitoshe. Hongera sana.
 
Hizo cost naona kama hazina uhalisia kwa jiji la Dar....mfano ukumbi now days, Gari la maharusi,gharama ya suti, upambaji, gauni la bib harusi, MC

Pia cjana Cake hapo....gharama hizo unatafuta stress my frnd.

Ni kweli kwa Dar hiyo gharama itapanda tu.
 
1. Chakula: watu 150
x 7000 (kwa kila sahani) = 1,050,000 .00
2. Vinywaji: Bia At least watu 50 watatumia bia x 3 @ x 2300Tshs =
345,000.00
Soda Watu 100 watakunywa soda x 3@ x 600Tshs =
180,000.00
3. Suti ya bwana harusi 150 000Tshs. x 1
= 150,000.00
4. Gauni la bibi harusi kukodi 150,000 Tshs x 1
= 150,000.00
5.Suti ya best man 150,000 x 1
= 150,000.00
6. Gauni la best woman 100,000 x 1
= 100,000.00
7.Kushona suti za watoto wasimamizi 4 x 25,000 =
50,000.00
8. Usafiri A. Gari ya bibi harusi 1 x 50,000
= 50,000.00
B.Gari ya bwana harusi 1x 50,000
= 50,000.00
C. Gari costa 2 kwa ajili ya ndugu x 60,000
= 120,000.00
9. Gharama ya Ukumbi 1 x 500,000
= 500,000.00
10. Gharama za upambaji 1 x 250,000
= 250,000.00
11. Gharama za kurekodi 1 x 200,000
= 200,000.00
12. Gharama za Shampeni 2 x 200,000
= 400,000.00
13. Gharama za guest 60,000
= 60,000.00
14. Mc na Muziki 200,000
= 200,000.00
15. Vipodozi bibi harusi 150,000
= 150,000.00
16. Blass Band 200,000
= 200,000.00

= 4,355,000.00


NDUGU WASHAURI WANGU, NI MIMI NILIYEOMBA USHAURI JUU YA UWEZEKANO WA
KUFANYA HARUSI YA TSHS. 2000,000 HAPA DAR ES SALAAM. MLINIONYESHA KUWA
HAKUNA KINACHOSHINDIKANA, ILA NI AINA GANI YA HARUSI NILIHITAJI NI SUALA
AMBALO MLINIACHIA.

NIMEENDELEA KUPAMBANA WAKUU, MWANAMKE HATAKI KUNIACHIA, NIMEKUBALI
KUPAMBANA.

BADO NARUDI KWENU WAKUU,HEBU KAGUENI VIFAA
NILIVYOTAJA HAPO JUU, NINI KIMEPUNGUA, JE HARUSI HAPO NIMEKAMILISHA.
NIBORESHE NINI, WAZEE KARIBUNI.
NATANGULIZA SHUKRANI


mkuu kumbe ndoa bado? kweli maana nimesubiri unijulishe tuvunje kamati baada ya harusi sioni? dah usisahau ehee
 
Harusi million 4, kweli we umebana vizuri. Hongera. Me najua hiyo million 4 inalipia mapambo tu tena inaweza isitoshe. Hongera sana.
Dah, mapambo tu, eeeh, hapo umenipa mtihani. Lakini ndio hivyo, nategemea kuongezeka gharama lakini sina namna nyingine..
 
mbona sioni maji ya kunywa?keki?

Nimetegemea mahitaji ya maji hayatakuwa makubwa ikilinganishwa na soda na bia ingawa yanapaswa kuwepo, kwa suala la keki natarajia kumtumia shemeji yangu anafanya vizuri katika field hiyo na alitengeneza ya harusi yake, nitanunua materials. Asante
 
Wagalatia mna tabu sana, kwetu ni gharama ya pete, uturi, na sinia la pilau mke anaingia ndani...
Mnapenda ufahari mpaka mnakufuru..
Ndiyo maana ndoa zenu hazidumu
 
1. Chakula: watu 150 x 7000 (kwa kila sahani) = 1,050,000 .00
2. Vinywaji: Bia At least watu 50 watatumia bia x 3 @ x 2300Tshs = 345,000.00
Soda Watu 100 watakunywa soda x 3@ x 600Tshs = 180,000.00
3. Suti ya bwana harusi 150 000Tshs. x 1 = 150,000.00
4. Gauni la bibi harusi kukodi 150,000 Tshs x 1 = 150,000.00
5.Suti ya best man 150,000 x 1 = 150,000.00
6. Gauni la best woman 100,000 x 1 = 100,000.00
7.Kushona suti za watoto wasimamizi 4 x 25,000 = 50,000.00
8. Usafiri A. Gari ya bibi harusi 1 x 50,000 = 50,000.00
B.Gari ya bwana harusi 1x 50,000 = 50,000.00
C. Gari costa 2 kwa ajili ya ndugu x 60,000 = 120,000.00
9. Gharama ya Ukumbi 1 x 500,000 = 500,000.00
10. Gharama za upambaji 1 x 250,000 = 250,000.00
11. Gharama za kurekodi 1 x 200,000 = 200,000.00
12. Gharama za Shampeni 2 x 200,000 = 400,000.00
13. Gharama za guest 60,000 = 60,000.00
14. Mc na Muziki 200,000 = 200,000.00
15. Vipodozi bibi harusi 150,000 = 150,000.00
16. Blass Band 200,000 = 200,000.00
= 4,355,000.00


NDUGU WASHAURI WANGU, NI MIMI NILIYEOMBA USHAURI JUU YA UWEZEKANO WA KUFANYA HARUSI YA TSHS. 2000,000 HAPA DAR ES SALAAM. MLINIONYESHA KUWA HAKUNA KINACHOSHINDIKANA, ILA NI AINA GANI YA HARUSI NILIHITAJI NI SUALA AMBALO MLINIACHIA.

NIMEENDELEA KUPAMBANA WAKUU, MWANAMKE HATAKI KUNIACHIA, NIMEKUBALI KUPAMBANA.

BADO NARUDI KWENU WAKUU,HEBU KAGUENI VIFAA NILIVYOTAJA HAPO JUU, NINI KIMEPUNGUA, JE HARUSI HAPO NIMEKAMILISHA. NIBORESHE NINI, WAZEE KARIBUNI.
NATANGULIZA SHUKRANI


kwa hali hii bora ndoa ufumaniwe ndoa ya mkeka
 
Back
Top Bottom