Bado, gharama za harusi jamani, tafadhali

Bado, gharama za harusi jamani, tafadhali

Unrealistic unless unaifanyia nje ya mji kabisa

wish you all the best
 
1. Chakula: watu 150 x 7000 (kwa kila sahani) = 1,050,000 .00
2. Vinywaji: Bia At least watu 50 watatumia bia x 3 @ x 2300Tshs = 345,000.00
Soda Watu 100 watakunywa soda x 3@ x 600Tshs = 180,000.00
3. Suti ya bwana harusi 150 000Tshs. x 1 = 150,000.00
4. Gauni la bibi harusi kukodi 150,000 Tshs x 1 = 150,000.00
5.Suti ya best man 150,000 x 1 = 150,000.00
6. Gauni la best woman 100,000 x 1 = 100,000.00
7.Kushona suti za watoto wasimamizi 4 x 25,000 = 50,000.00
8. Usafiri A. Gari ya bibi harusi 1 x 50,000 = 50,000.00
B.Gari ya bwana harusi 1x 50,000 = 50,000.00
C. Gari costa 2 kwa ajili ya ndugu x 60,000 = 120,000.00
9. Gharama ya Ukumbi 1 x 500,000 = 500,000.00
10. Gharama za upambaji 1 x 250,000 = 250,000.00
11. Gharama za kurekodi 1 x 200,000 = 200,000.00
12. Gharama za Shampeni 2 x 200,000 = 400,000.00
13. Gharama za guest 60,000 = 60,000.00
14. Mc na Muziki 200,000 = 200,000.00
15. Vipodozi bibi harusi 150,000 = 150,000.00
16. Blass Band 200,000 = 200,000.00
= 4,355,000.00


NDUGU WASHAURI WANGU, NI MIMI NILIYEOMBA USHAURI JUU YA UWEZEKANO WA KUFANYA HARUSI YA TSHS. 2000,000 HAPA DAR ES SALAAM. MLINIONYESHA KUWA HAKUNA KINACHOSHINDIKANA, ILA NI AINA GANI YA HARUSI NILIHITAJI NI SUALA AMBALO MLINIACHIA.

NIMEENDELEA KUPAMBANA WAKUU, MWANAMKE HATAKI KUNIACHIA, NIMEKUBALI KUPAMBANA.

BADO NARUDI KWENU WAKUU,HEBU KAGUENI VIFAA NILIVYOTAJA HAPO JUU, NINI KIMEPUNGUA, JE HARUSI HAPO NIMEKAMILISHA. NIBORESHE NINI, WAZEE KARIBUNI.
NATANGULIZA SHUKRANI


Pls nitupie namba za mc na huyo wa steel picha na video
 
kaka siku hz sherehe za ndoa hizi mitaji ya watu hasa wanakamati
hapo watajfanya kuchangia ila wanajua zitarudi kwenye maandalizi
take care and all the best
 
Mkuu,utanipa gharama za mwisho kbs utakazotumia,mimi nataka nifanye harusi very simple,ya wageni kama 35 tu...unaweza kualika wengi wachawi nao wakapitia humohumo! Infact,sababu ya msingi ni kwamba nataka kufanya harusi kwa pesa yangu mwenyewe! Sitaki kumchangisha mtu hata senti tano(maisha magumu haya,sitaki kuwabebesha watu majukumu yasiyo na ulazima,ila nikikumbuka nilivyowachangia watu roho inaniuma),ikikost kama 3M naweza kuimudu mwenyewe.
 
Ndio Fanya ivo mkuu... Maisha yanaendelea... Hongera zako lkn kwa kupata jiko bila shaka hujakosea kuchagua na mungu alikusaidia maana ni bora ukosee kujenga nyumba kuliko kukosea kuoa.

Asante, ndugu yangu, unashukuru tu kufikia ulipofikia, mengine unaomba Mungu afanye kazi yake. Masuala yanakwenda na kila kitu, unaweza fikiri umepatia mambo yakaja kubadilika baadae, ingawa nafahamu controli ya ndani nayo huchangia mtu kubadilika katika kumbadilisha mwanamke, penye kunihitaji nitajitahidi. Lakini huwa naamini hakuna asilimia mia moja katika hili, ni kuangalia je mtu anaiacha hiyo asilimia mia moja kwa umbali gani, ukimpata wa asilimia 90 pengine una bahati, kuna wa 80, 70, 60 sio mbaya kaa tayari kuziba magepu mengine kwa tofauti inayobaki kufikia mia moja.
Kuna 50, 40, 30,.....Utaangalia uwezo wako. Ingawa sio wote wanaoona ni kazi, wapo wanaoweza hata kwa asilimia 2 kulingana na mtazamo wa mtu.


Nimejaribu kusemea mtazamo wangu kwa asilimia. Nina maana kwamba, ninahitaji mwanamke aliye na sifa zote kama ninavyohitaji (ndiyo asilimia 100) lakini katika hali ya kawaida lazima mtu atapungua kimoja au viwili (ndipo asilimia zinaposhuka) sasa upunguaji ule (ni vitu vingapi vinapungua) ndio unaokupa kusema kapungua mno au kidogo (ndio asilimia 90,80,70,60,50,....) Sasa wewe una kazi ya kuangalia je mapungufu hayo utayabeba? (utaweza kuyachukua? je hizo asilimia 10 zinazopungua utaweza kubeba, je hizo 20,30,40 ....) Ni hivyo ndugu yangu.

------ ingawa sitataja kuingilia kazi ya Mungu, nalenga zaidi yale ambayo sisi wanadamu tunayabeba-----

Hiki si kipimo sahihi ni mtazamo wa kila mmoja wetu, lakini nafahamu wanaume hatutofautiani sana katika hili tofauti itakuja tu kwenye makadirio nitasema 100 mwingine atasema huyu bwana vipi, 50.... siyo hivyo,.... nataka kusema kila mmoja anavyotoa uzito anaouona.

Nimefika mahali baada ya safari ndefu, nimeona asilimia zinazopungua nitabeba, nimeamua kuingia kazini ndugu yangu
 
Mkuu,utanipa gharama za mwisho kbs utakazotumia,mimi nataka nifanye harusi very simple,ya wageni kama 35 tu...unaweza kualika wengi wachawi nao wakapitia humohumo! Infact,sababu ya msingi ni kwamba nataka kufanya harusi kwa pesa yangu mwenyewe! Sitaki kumchangisha mtu hata senti tano(maisha magumu haya,sitaki kuwabebesha watu majukumu yasiyo na ulazima,ila nikikumbuka nilivyowachangia watu roho inaniuma),ikikost kama 3M naweza kuimudu mwenyewe.[/QUOTS


Sawa usijali ndugu yangu. Lakini baadae kidogo nitarudi kwako
 
kaka siku hz sherehe za ndoa hizi mitaji ya watu hasa wanakamati
hapo watajfanya kuchangia ila wanajua zitarudi kwenye maandalizi
take care and all the best

Ndugu yangu umenigusa sana, ni kitu kinasumbua kichwa mpaka sasa kuna kitu najaribu kufanya. Nitawajuza kama nikifanikiwa kupitia hapa JF, yaani nafahamu kuna watu wanangoja hilo sana ili wapate hela.
 
Uislam unakataza hivo vitu Vyote ulivo Orodhesha hakuna karibu katika uislam ndugu yangu
 
Ndoaa ngumu na mke mwema cjapatiwaa na hata nikipatiwa haruc nayo ghali daaaaaaaa!!!!
 
Ndugu yangu umenigusa sana, ni kitu kinasumbua kichwa mpaka sasa kuna kitu najaribu kufanya. Nitawajuza kama nikifanikiwa kupitia hapa JF, yaani nafahamu kuna watu wanangoja hilo sana ili wapate hela.

mi nakwambia wanaweka bajeti kubwaaa
utafkri sherehe inafanyika angani vile
shampeni laki mbili inawasap na instagram na video au inajifungua yenyewe inajimimina yenyewe km ivyo sawa
 
Back
Top Bottom