Baba mkwe, mahari hii imenishinda

Baba mkwe, mahari hii imenishinda

Yaan umenikumbusha braza wangu mmoja hiv mtoto wa dingi mkubwa, alienda kupangiwa Mahari wakataka Milioni 3 jamaaa akawa nayo milioni 1. Wakakomaa weee, mshenga kajaribu kuwapangua lkn mashangazi wamekaza hawaelewi kitu. Basi wakamuita bwana harusi mtarajiwa atoe suluhisho kama ataongeza, broo alipoenda akasema kua ana milioni moja tu, hana pesa ya kuongeza hata hivo kajitahidi sana, ila kama hawataki hiyo milioni basi yupo tayari kumuacha binti yao aolewe na mwingine jmaa akaishia hapo. Kumbe binti alikua ndani anasikia akaanza kuangua kilio wakimbembeleza ndo anazidisha sauti. Ilibaki kua aibu tu.
Waliporudi Jamaaa alikaa kimya ikapita miezi 3 hapaeleweki binti anasumbua anataka kuolewa, anashinda kwa broo kila siku ili asije kurafuta mke mwingine wakakubali tu Hiyohiyo milioni moja.
Bro angemtia na mimba kabisa wangempa bure kabisa. Waluguru muda mwingine siwaelew watu wenyewe full utegemezi ila bado masharti kibao
 
Chief huyo dem ulimkuta Bikra?yeye mwenyewe ana utajiri sana ama?hyo 280000 uliyotoa waambie ndio mahali..hawataki waambie wakae na lidemu lao
 
Bado kidogo nikushauri uongee na huyo mama watoto kuhusu hio mil 5 ili awashawishi wazazi wakupunguzie..
ila kila nikiikumbuka laki mbili na themanini ya chakula uliyolipishwa naskia uchungu Chief..

tupa kule hio familia takataka.
King ndio kashasema

na mimi nilitaka kushauri hivyo

ila kulipishwa pesa ya maandalizi ya event yao 280k

Asee ki ufupi hiyo sio familia

Niamini nakwambia hata ukisema ufumbe macho ulipe yote 5M

mbele utakutana na mi cost mengine na watakufanya kama DUKA lao

Funga macho TEMANA nao....

Mtoto akizaliwa mtunze kwa gharama zote Tena in a CLASSIC WAY

ili waone sio kwamba huna hela,ila ni HAUNA hela za kuwapa wajinga wajinga

kwa mambo yakijinga jinga.

Subiri mtoto azaliwe,Hudumia mwanao hadi wahisi n mtoto wa JAY Z
 
Leo week ya pili nimeshindwa kabisa kupokea simu ya Baba mkwe na Mshenga wangu.

Iko hivi katika misoto yangu na kukulu kakala za maisha atimae nikajikuta nimedondokea kwa mtoto wa kichaga Kama ilivyo janga kwa wanaume wengi wa mjini.

Mipango ikapangwa na siku ya kufika ukweni kupeleka posa ikafika. Kidume nikajikoki na Mshenga wangu na wadada 3 wa kukodi tukazuka ukweni.

Mambo yalikua shwari hadi pale mjomba mtu akapewa fursa ya kutupangia package ya mahari ili mpango mzima ukamilike.... list ya makorokoro kibao, Mara mkaja wa mama, Bibi, mablanket ya Mama na mashangazi, mbege mapipa matatu, mbuzi 3 wa maziwa na....mwishoni akataja cash money 3 Mil.


Mimi kipindi anataja yale mazaga hata nilikua sifuatilia ,akili yote ilikua inasubiri point ya msingi Cash money.

Badae ikatolewa option ya ku convert the overall cost ika amount Kama 5 Mil. na ushee!

Jitihada za mshenga kupangua bei hazikuzaa matunda. Mbaya zaidi ile tumemaliza events shangazi anatuzuia hakuna kuondoka mpaka tumelipia gharama za maandalizi walioyotufanyia.

Kwa shingo upande nikausukuma mzigo wa M pesa tsh 280, 000 coz walidai laki 3.


Niliporudi lodge usiku mzima sikulala , series nzima ikawa inaji frash back repetitively.

Nika najiuliza kwani wananiuzia mke kisa ni afisa ustawi wa jamii?

Ana kipi Cha ziada ambacho wake wa ndg zangu wameolewa na jumla ya mahari tulizotoa na makokoro yote hata milioni haikufika?

Kwani ana kismat Cha mafanikio? Mbona tangu tuingie kwenye relationship mambo mengi tunakimbizana kwa had-hoc za kufa mtu?

Na mengine mengi ambayo si busara kuyaanika humu.

Alifajiri nikaamua kufanya maamuzi magumu ..."Katu sitorudi tena ukweni." Kwa maana kuwa sitoi tena mahari, mtoto wao nimeshamtia mimba ,wakimtaka waje wamchukue.


Ni hayo tu.....sirudi ukweni tena

Mashemeji zangu wachaga povu ruksa. Ila katu sirudi tena ukweni.
Haki ya nani washamtengenezea usingo mother mtoto wao! Mkuu Ml 5 nenda nayo Kisemvule Obey Village kiwanja tsh 1,400,000/= au 2,000,000/= ....nunua kiwanja... 1000,000/= nunua tofari za vyumba viwili...inayobaki anza ujenzi hata vyumba viwili hamia kama hutaki kukaa huko pangisha..... papuchi ushaila sana na ikitaka itakuja kwako mwenyewe. Nisije ona unanyanyua kwato zako unaenda Moshi tenaaaaa.
 
Mahari ni kikwazo kikubwa sana siku kwa sisi vijana.

Utajiuliza kuwa baada ya mahari hakutakuwa na harusi au maisha ya ndoa?

Je hujaisaidia hiyo familia kumchukua Binti yao na kuishi naye?

Je undugu hatakuwepo kati ya kwao Binti na kwenu katika kusaidiana kimaisha?

Wazazi wanapaswa wajifunze na kujisahihisha la sivyo wataendelea kuongeza idadi za ma-single mothers kila siku.

Mleta mada uko sahihi kabisa 100%.
Kabisa mkuu..... Halafu ukute driving motive yao ni wivu na tamaa ya fedha (nikisema wivu nina maana pana sana)
 
Mahari ni kikwazo kikubwa sana siku kwa sisi vijana.

Utajiuliza kuwa baada ya mahari hakutakuwa na harusi au maisha ya ndoa?

Je hujaisaidia hiyo familia kumchukua Binti yao na kuishi naye?

Je undugu hatakuwepo kati ya kwao Binti na kwenu katika kusaidiana kimaisha?

Wazazi wanapaswa wajifunze na kujisahihisha la sivyo wataendelea kuongeza idadi za ma-single mothers kila siku.

Mleta mada uko sahihi kabisa 100%.
Ukweli sisi vijana tunateseka sana, wazazi nao wametia ngumu sana, hasa haka kamtindo ka kukomoana kuanzia millioni, niliwahi kujaribu nikiwa na kalaki 8 walidai ni pesa ya kununulia kiatu cha sikukuu, aisee niligive up, mpaka sasa siwezi kuwa na mahusiano tena, naona Dunia inaenda kasi sana
 
Mdoa mada na Mimi yalishanikuta kama yako ila Mimi sio kwa mchaga,nilitajiwa kwa USD 3000,sawa na milioni 6 na laki 6,nimewapa tu zawadi ya mjukuu na nikajiongezea mihula miwili ya kwenye kiti cha ubaharia!
Sheria yangu niliyojiwekea mahari hata niambiwe Trilioni moja sitatoa zaidi ya laki 5 na itolewe na VAT kabisa hapo sitaki kukwepa kodi,na risiti nipewe ili ikitokea dharura mahakama wajue pa kuanzia
Mkuu hawa watakua Wahaya tu
 
Waambie utawalipa kidogo kidogo wakikubali ndo mazima iyoo
 
Ukiachana na Mahari kuwa 5M plus haijadiliki

Kitendo cha wewe kulipia Gharama za wao kuandaa sherehe hii mpya...

Sitaki kuwahukumu wachaga wote ila kama ndio utaratibu wenu ndugu zangu thats too much!!

5M hiyo unatoa kwa familia ya Mkeo mtarajiwa kama mahari hizi ni gharama ambazo lazma utazilipa kama Bwana Harusi
--- Gauni la Harusi plus Saloon Nafikri
--- Pete za ndoa
--- Suti ya Bwana Harusi
--- Gharama ya Ukumbi
--- Gharama za Kikao cha kwanza
--- Gharama za Usafiri kwenda kulipa 5M
Plus mambo mengne madogo madogo
Mkuu bora umesepa Kibingwa ila mwambie Afisa Ustawi wa Jamii kwamba gharama zimekua kubwa u cant afford ili ajue ukwel.
Ndoa za kihivyo nitakuwa nazisindikiza kwa macho tu hadi naingia kaburini.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom