Mr sule
JF-Expert Member
- Oct 14, 2021
- 607
- 1,097
Baada ya kuweka mizizi mizuri ukweni na kuwa na mahusiano mazuri na ukweni kwangu, niliamua nikatoe mahari baada ya miezi kadhaa kutoa posa, mshenga alimuuliza baba mkwe wajipanga vipi siku wakitaka kurudi hatua inayofuata.
Baba mkwe alisema nataka kuona hao wawili wana mahusiano mazuri.
Basi baada ya miezi kadhaa kupita ilibidi nitoe taarifa kwa mshenga kwamba nataka tukatoe mahari.
Taarifa ilimfkia baba mkwe na tulipanga siku ya kutoa mahari.
Ikiwa imesalia wiki moja kufika siku ya tukio, bibie alitangulia kwao ili kupokea wageni wake.
Ajabu baba mkwe aliomba kuongea na mimi, akanimbia anataka mimi niende kwanza kabla ya tukio.
Basi nilipohitikia wito wa baba mkwe, aliniuliza maswala mengi na tuliongea kama masaa 3 hivi na mchanganyiko wa story za huku na kule.
Baada ya maongezi, baba mkwe akasema sioni sababu za wewe kutoa mahari kikubwa ni kuzingatia hayo tuliongea na kumtanguliza Mungu.
Asema baba mkwe, naona kabisa ni jinsi gani mwenzio umemtunza na naona kabisa mabadiliko ya maisha kwa mwanangu, sikuwah kujua kama mwanangu ni mtu mwenye furaha hivi, siku hzi naona kabisa amechangamka tofauti na zamani.
Baada ya kurudi home,simu yangu moja kwa moja kwa mshenga kwamba ukweni hawataki mahari ila tutaenda kufamiana na maongezi zaidi lakini tusipeleke cent yeyote.
Mwenzenu nimeoa ndoa ya kanisani, licha bado tunaishi tofauti. hapa nafatilia maswala ya huakika cheti cha ndoa.
Baba mkwe alisema nataka kuona hao wawili wana mahusiano mazuri.
Basi baada ya miezi kadhaa kupita ilibidi nitoe taarifa kwa mshenga kwamba nataka tukatoe mahari.
Taarifa ilimfkia baba mkwe na tulipanga siku ya kutoa mahari.
Ikiwa imesalia wiki moja kufika siku ya tukio, bibie alitangulia kwao ili kupokea wageni wake.
Ajabu baba mkwe aliomba kuongea na mimi, akanimbia anataka mimi niende kwanza kabla ya tukio.
Basi nilipohitikia wito wa baba mkwe, aliniuliza maswala mengi na tuliongea kama masaa 3 hivi na mchanganyiko wa story za huku na kule.
Baada ya maongezi, baba mkwe akasema sioni sababu za wewe kutoa mahari kikubwa ni kuzingatia hayo tuliongea na kumtanguliza Mungu.
Asema baba mkwe, naona kabisa ni jinsi gani mwenzio umemtunza na naona kabisa mabadiliko ya maisha kwa mwanangu, sikuwah kujua kama mwanangu ni mtu mwenye furaha hivi, siku hzi naona kabisa amechangamka tofauti na zamani.
Baada ya kurudi home,simu yangu moja kwa moja kwa mshenga kwamba ukweni hawataki mahari ila tutaenda kufamiana na maongezi zaidi lakini tusipeleke cent yeyote.
Mwenzenu nimeoa ndoa ya kanisani, licha bado tunaishi tofauti. hapa nafatilia maswala ya huakika cheti cha ndoa.