Baada ya Mbowe kugeuka na kuwa kama kina Shibuda, John Cheyo na Mrema ni upi mustakbali wa siasa za upinzani Tanzania?

Kwa hali inavyoendelea nchini ni dhahiri hakuna tena upinzani. Bali kuna uungwaji mkono juhudi wa Wapinzani kwa CCM kila mmoja kwa staili yake. ACT Wazalendo wanakula pamoja na CCM kule Zanzibar na CHADEMA nao wanatafuta robo mkate wao huku Tanganyika.

Kabla CHadema hawajaanza kupetiwapetiwa, Kutomaswatomaswa na kulambishwa asali na CCM hii ya leo ya Kinana na Samia, walikuwa wakitokwa povu sana kuhusu ACT Wazalendo kuingia katika serikali ya umoja wa Kitaifa huko Zanzibar. ACT walikuwa wakijitetea kuwa eti ni takwa la kikatiba kuingia humo huku CHADEMA wakiwaita ACT Wasaliti kwa hoja ya kuwa wamewasaliti Wazanzibar kwa kushiriki kula matunda ya uchaguzi haramu.

Leo tunaona CHADEMA nao wamekinga mkono kula ruzuku ambayo hapo mwanzo walisema ni haramu kwa kuwa imetokana na uchaguzi haramu. Kiufupi wamelamba matapishi yao!.

Ukiachilia mbali hilo, CHADEMA walikuwa wakijulikana sana kuwatukana akina hayati Lyatonga Mrema , John Cheyo na Shibuda kuwa eti ni makada wa CCM kutokana na kuwa na siasa za mrengo wa kukubaliana na CCM katika mambo mengi. Leo tunamuona Mwenyekiti Mbowe naye akigeuka kuwa Cheyo na Shibuda aliyechangamka zaidi.

Mbowe leo kaibeba rasmi mikoba ya John Cheyo na ameanza kutumia arguments zilezile za John Cheyo kuwa anataka siasa za "maridhiano", ambazo kimsingi siasa za hivyo ni za kutomasanatomasana, kubembelezanabembelezana ilimradi tu kila mtu aachiwe sphere yake ya influence ili aweze kula kwa urefu wa kamba yake.

Tujiulize, Hizi sifa ambazo Mbowe anazitoa kwa Samia zina tofauti gani kwa mfano na Sifa za Cheyo au Shibuda walizokuwa wakizimwaga kwa Magufuli?

Hii inaonyesha kuwa pengine ukiwa mpinzani na ukaanza kuzeeka, unaanza kuwa na tabia za OLD MAN CCM SYNDROME. Yaani unaanza kuwa na tabia zile za kiCCM CCM. Unaanza kujisogeza kwa CCM, unaanza kuongea kama wanaCCM, na unaanza kubehave kama wanaCCM

Huu ni muda muafaka kwa wanaCHADEMA kumtafakari Mwenyekiti Mbowe kuona kuwa , Je ni kweli siasa hizi za kulala kitanda kimoja na CCM anazoanza kuzifanya zinatokana na utafiti wa kina na upeo wa kisiasa au zinatokana na

1. Mosi, Je ana makubaliano ya siri na CCM ikiwa kama sababu ya kuachiwa kwake Jela na kwa hivyo anafuata script aliyotengenezewa AU

2. Je ana masilahi bianfsi ikiwemo ya kibiashara au kurudishiwa mali zake alizoporwa na serikali ya CCM kipindi cha Mwendazake?

3. Au je ni uzee na uchovu(wa Kisiasa) kwa hiyo ndo ameamua kwenda na falsafa maarufu ya "Kama huwezi kuwashinda, basi ungana nao?".

Katika nchi yoyote ukiona UPINZANI unafanya ROMANCE na Chama Tawala, Jua kuwa hakuna upinzani hapo bali kuna genge la wapiga dili wa kisiasa
Chawa mnamaumivu makali kama vile mmepitshiwa pasi ya umeme. Mnajisikia vibaya pale mama asivyopenda visasi kama mtangulizi siyo !!

Poleni chawa
 
Kuteseka ni sehemu ya struggle. Kama hutaki kuteseka kaa pembeni ili walio tayari hata kufa ili kuleta mabadilikio ya kweli washike usukani. Kuliko kusaliti stuggle na kuanza kujikombakomba kwa CCM bora ukae pembeni ulee wajukuu au ule bata kadri unavyoweza
Wewe umefanya nini kuleta mabadiliko ya kweli ?!. Unadharau juhudi za watu huku unachangia sifuri !!
 
Wakati wanateseka kwa kufilisiwa, na kuwekwa rumande kwa kesi za mchongo, na wengine kuuliwa mlitoa msaada gani kwao

Kwani walipokuwa wanaenda bungeni na mashangingi nani ulimuona akiwaomba hata lift? Acha kuleta mifano isiyo na tija. Ingekuwa watu walienda kushinda nao wakati wanapokea mishahara mikubwa, haya malalamiko yako yangekuwa na maana. Kama umeishiwa na mifano kaa kimya.
 
Wapinzani sisi hatuelewi huo msimamo wa viongozi wa CDM kwa muongozo wa Mbowe. Wao viongozi waendelee na siasa za kujikomba, lakini sisi hatuna muda huo. Kama Mbowe aliweza kumpokea Lowassa na watu wakamvumilia, basi safari hii atajua hana ushawishi huo aliodhani anao. Ni muda mrefu Mbowe alishaonyesha kupoteza mwelekeo.
Sio rahisi hivyo!!Nyie wafuasi wa MEKO tunajua hiki kinachoendelea kinawauma sana!!mlitaka ziendelee zile siasa za kishenzi tu!!kwani mlikuwa mnafaidika nazo!!wewe una uchungu na CDM kuliko mbowe??
 
"Tumbo niache nim'bakizie Mandawa Uji" Njaa isikie Kwa jirani tu, ni mbaya sanaaaa. Nimemkumbuka zama za Mtikila R.I.P na siasa za Kabachori Hawa wengine ilikuwa ni swala LA muda tu kuunga juhudi.
 
Tuacheni kejeli instead tuwapongeze Samia na Mbowe kwa kuweka masilahi ya nchi yetu mbele kuliko kitu kingine chochote.

Hii nchi angeendelea kuwa hai yule HAYAWANI wa Chato ingekuwa nchi ya hovyo kuliko Yemen na Somalia
Muache aendee kuoza huko aliko
Hii nchi imekuwa ikijisifu kwa amani miaka yote ila sio maendeleo.
 
Sio rahisi hivyo!!Nyie wafuasi wa MEKO tunajua hiki kinachoendelea kinawauma sana!!mlitaka ziendelee zile siasa za kishenzi tu!!kwani mlikuwa mnafaidika nazo!!wewe una uchungu na CDM kuliko mbowe??
Hivi kwanini Chadema walikuwa wanaonekana wapingaji wa kila kitu hadi Kikwete akauliza kuwa kwani mazuri hamuyaoni?
 
Hivi kwanini Chadema walikuwa wanaonekana wapingaji wa kila kitu hadi Kikwete akauliza kuwa kwani mazuri hamuyaoni?
Kwani jukumu kubwa la chama cha upinzani ni kumsifia aliyoko madarakani?!!Na atakusifia vipi wakati hilo ndio jukumu lako kubwa?Hapo ndipo miafrika tunakosea serikali inajenga kisima watu wanaona ni kama hisani na sio haki yao!!!
 
Kamanda kafwata nyao za LipumbaF


Yaan kama sio Chadema anaongea ila uso unaonyesha huyu kashanyoosha ulimi kwa State!
Kwa siasa zile za kishetani za mwendazake,Acha mama atutoe huko na mbowe hata lama atakuwa Mrema sawa tu,cha msingi turudi kwenye siasa zetu za 2015 kurudi nyuma.Najua wafuasi wa JIWE Mnaumia sana kwa hiki mama anachokifanya!!!!Ndio basi tena na kosa hilo la kumpa nchi MPOLI POLI halitajirudia tena!MUNGU FUNDI
 
Mfano south afrika wakati mandela kafungwa watu walikua wanaandamana
Ila Tanzania wakati mbowe na chadema wanashughulikiwa wote tulikua kimya alafu leo hii ndo tunajikuta tunauchungu wa mapambano kwanin ulikuwa huwatetei wakati wanateseka tuacheni unafki

Wewe umekaa nyuma ya keyboard alafu unataka wanaume wakupiganie maisha hayako na wahatarishe maisha yao na familia zao hivyo usipende sana mterereko we ni wa kiume
Ajabu hata hao wanachama wao wa chadema hakuna walichofanya wakati akina Mbowe wanapitia mateso.
 
Kwani jukumu kubwa la chama cha upinzani ni kumsifia aliyoko madarakani?!!Na atakusifia vipi wakati hilo ndio jukumu lako kubwa?Hapo ndipo miafrika tunakosea serikali inajenga kisima watu wanaona ni kama hisani na sio haki yao!!!
Basi sasa chadema sio ya kupinga kila kitu kama ilivyokuwa ikionekana hapo nyuma.
 
Kwa siasa zile za kishetani za mwendazake,Acha mama atutoe huko na mbowe hata lama atakuwa Mrema sawa tu,cha msingi turudi kwenye siasa zetu za 2015 kurudi nyuma.Najua wafuasi wa JIWE Mnaumia sana kwa hiki mama anachokifanya!!!!Ndio basi tena na kosa hilo la kumpa nchi MPOLI POLI halitajirudia tena!MUNGU FUNDI
Unataka kusema chadema huwa hamtofautiani mawazo ndio maana unaona kwa hiki kinachoendelea kwa ccm na chadema ni wafuasi wa jiwe tu ndio wanapinga ila chadema wote wana mawazo aina moja?
 
Basi sasa chadema sio ya kupinga kila kitu kama ilivyokuwa ikionekana hapo nyuma.
Wao lazima waendelee kukosoa tu,wakusifia wapo hao MACHAWA!! Na sasa wabunge watakuwa na wakati mgumu sana kwani toka wamebaki wenyewe bungeni hakuna wanalowasemea wananchi!!wanaowasemea wananchi wapo nje ya bunge!!!
 
Back
Top Bottom