FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 100,506
- 123,802
- Thread starter
- #41
Dada Faiza hapana hakuna matumaini hayo.kwa mimi niliepo hapa tangia miaka ya 70 mpaka sioni kama kuna jipya.
Ni kama wamefika kikomo cha kufikiri...
Watu wameengezeka na biashara zimengezeka na kodi pia zimengezeka lakini bara bara zile zile za zamani zinawashinda.
Ulaji ummekua mkubwa.
Nakupa mfano mmoja...ndani ya jiji lote kwa siku ni gari ngapi zinapaki kwenye maegesho ya kulipia ? Kwa uchache ni ni mzunguko wa gari zaidi ya 50000×2000 (average ya kila gari kwani mpaka jioni hakuna parking tupu) =100,000,000 × 20
days tu = 2000,000,000 kwa mwezi.
Sasa uliza jiji linapata ngapi kwa mwezi?
Hapa mbali ya vibali vya magari ya mizigo na mafuta.
Kwa mwezi wanakusanya 0.30% ya turnover ya biashara zote Dar...fikitia mi kiasi gani ?
Jee unaweza kujua kuna mabango kiasi gani katika jiji la Dar? Kila mahali kumejaa mabango haya ulipaji wake si chini ya 100,000 sasa chukulia yapo 50, 000= 5000,000,000
Faiza nchi hii hakuna wazalendo...uzalendo wetu ni katika ngozi tu.
Hili jiji ni la kuwa na mabustani na sehemu maalum za watoto
Ni jiji kama watu wanatuliza akili zao kusinge kuwa na foleni za kijinga au barabara kugeuka mahandaki.
Tusifu pa kusifiwa lakini jiji halina watu wenye vision kabisa
Kwa mapato wanapata mengi sana, lakini kumbuka kuwa hawaruhusiwi kutumia zote hizo, wan portion tu zingine ni lazima ziende hzina kusaidia mambo mengine yanayotakiwa nchi nzima.
Babra mpya mbona zinajengwa sasa hivi, tuna daraja la Kigamboni, tuna BRT, tuna Flyover ya Tazara, tuna ring road inakuja, kuna mengi mazuri tu yanakuja, na sasa tunaweza kukopa kwa wingi kwa kuwa tuna gas ya kutosha kwa hiyo tunakopesheka, wala usiwe na hofu, tutayaona tu mambo yakibadilika.
Tatizo kubwa ni viongozi waliopita, sijui walikuwa wanafanya nini? ndiyo kwanza tunaona Kikwete akijitahid kujenga huku na kule.