Azam Media Group

Azam Media Group

Mungu wangu kwangu itakuwa kama kituo cha runinga kwa kuwa na madish mengi nina Zuku,DStv na sasa Azam,jamani kwanini isiwe kama kampuni za simu tuwe tunabadili smart card tu ,hadi mapaa yanaanguka kwa kuzidiwa na madishi na sebuleni hadi meza zinaanguka kwa kubeba ving'amusi.Mapaa ya nyumba yamekuwa kama majumba ya mazungu wa unga kwa kuwa na madish mengi.Naomba Azam asije kutujazia channel za Peace TV na za Yemeni au Mecca

Mkuu mbona umeharisha! Au unataka aweke chanel za yule tapeli tb joshua?
 
mmmhh ngoja tusubiri ila kama nina mashaka na hiyo malipo ya mwezi
 
Nangoja kwa hamu hicho king'amuzi!! Na wakitaka kupiga bao, malipo yawe kadri utumiavyo!!!
 
Azam bhana huwa ananichekesha sana,kaja kuchafua hali ya hewa sasa wazee wanaobebwa na tcra watabebwa na nan???
 
Kwa kweli Azam wanatisha, mimi mwenyewe nakisubiri kwa hamu sana.
 
Azam Media group ni kampuni kubwa na yenye sifs zisizo na shaka, pia inasemekana wataonesha na league one
 
Kisimbus chenyewe ni 48000, ila ukinunua seti nzima pamoja na dishi lake ni 90000, malipo kwa mwezi ni tsh 2000 tuu!!

Tunakisubiri kwa hamu,waanze kuuza mapema, mikoani ianze sambamba na dar.
 
Kisimbus chenyewe ni 48000, ila ukinunua seti nzima pamoja na dishi lake ni 90000, malipo kwa mwezi ni tsh 2000 tuu!!
duh,tz hii hii niijuao?iliyokuwepo gtv?haya,kama kweli jambo la kheri hili
 
Back
Top Bottom