AU's dilemna and the Libyan crisis

Hujui tu maji hutiririka toka kichwani kuja miguuni! Tusubiri sisi huku miguuni matone yatatufikia! Labda tuwe wajanja kuanza kunawa miguu kabla hatujalazimishwa kuoga!
 
Mkuu mbona unakuwa na Myopia kiasi hicho?, Shughuli inafanywa na UN hii na kati ya walipiga kura ya kuidhinisha ni Nigeria, South Africa, Gabon. Hawa wao wanatekeleza kazi waliyotumwa tu.

Unajua ukiangalia sana wanaolaani kichapo hiki ni viongozi wa Afrika waliotaka kuset precedence baada ya Gaddafi kuendelea kutawala kwa kuua raia wasio na hatia na kuitumia wao kama mfano kuwatishia wananchi wa nchi zao ili waendelee kuwatawala kwa nguvu. Kichapo hiki kinatoa somo kwa wenye mawazo kama Gaddafi na Tanzania tukiwemo kuwa dola haiwezi kuwa ndiyo source of power bali ni wananchi kwa ridhaa yao. Pia inaongeza ujasiri kwa wale watakao taka kupinga serikali za kidikteta kuwa theya are not alone, hata kama watauwawa sheria itachukua mkondo wake.

Ule wakati wa kuua wananchi kama ilivyotokea Pemba 2001, Mwembechai 1998 na Arusha 2011 na hakuna accountability yoyote sasa unatakiwa kukoma. Ninaamini kabisa kuwa watawala wa Afrika wanaong'ang'ania madaraka kwa kuchakachua hii attack ya Libya itawatisha sana na kuwatia kiwewe.

Gadafi alikuwa akipambana na waasi, maana hakuna waandamanaji wanaomiliki silaha, vifaru na daraya za kijeshi kisha wanateka miji. ww kwa mawazo yako ukiwa rais wa nchi na waaasi wanafanya kama wanavyofanya libya ungefanya nn?

jengine hao waasi wameambiwa milango iko wazi ya kuzungumza wamekataa na wanasisitiza lazima gaddafi ang'oke, nnaamini hawa jamaa wametumiwa na hao mbwa (marekani na weziwe ) kwa lengo ya kuivamia libya
 
..Ameua vya kutosha kwa kisingizio kuwa wale anaowaua ni waasi...acha kushabikia mauaji..mwache wamwondoe..acheni kuendekeza unafiki Afrika eti 'sovereignity'..kwa mgongo huo Waafrika wenyewe(marais) ndio wamekuwa maharamia mabaradhuli wakubwa ndani ya AFRIKA yao kuliko hata walichofanya wakoloni....bul..sht..!
 
Africa kunatendeka nini?
Leo vikosi vya ushirika vimefanya mashambulizi na kuua raia wengi,uvamizi huu ni katika kile kinachodaiwa kuwalinda raia walibya..
Haiwezekani kuua rai eti ili kuwalinda,ni kweli Ghadafi amekaa madarakani muda mrefu,na ameua rai,lakini sikubaliani na hatua yoyote ya matumizi ya nguvu kumwondoa Madrakani.
Azimio la kuivamia libya ni batili,hakuna nchi yenye kura ya turufu kwa nchi nyingine
natoa wito kwa Africa kuungana na kupinga uvamizi huu wa kijeshi

Ninaunga mkono uvamizi wa coalition forces, kazi nzuri natamani wakimalizana na ghadafi waje kutusaidia na sie
 
Africa kunatendeka nini?
Leo vikosi vya ushirika vimefanya mashambulizi na kuua raia wengi,uvamizi huu ni katika kile kinachodaiwa kuwalinda raia walibya..
Haiwezekani kuua rai eti ili kuwalinda,ni kweli Ghadafi amekaa madarakani muda mrefu,na ameua rai,lakini sikubaliani na hatua yoyote ya matumizi ya nguvu kumwondoa Madrakani.
Azimio la kuivamia libya ni batili,hakuna nchi yenye kura ya turufu kwa nchi nyingine
natoa wito kwa Africa kuungana na kupinga uvamizi huu wa kijeshi

Mkuu nimekugongea thanks,

Kwanini nguvu hiyo hiyo isitumike kumng'oa Gbagbo, kule Ivory Coast? au issue hapa ni mafuta?
 
Hivi na utaalamu wao wote kiteknolojia hawawezi kumtungua Gadafi peke yake mara moja, bila kulazimika kuua raia wengine?
 
mkuu nimekugongea thanks,

kwanini nguvu hiyo hiyo isitumike kumng'oa gbagbo, kule ivory coast? Au issue hapa ni mafuta?

Wakimaliza kazi Libya naomba waje kutusaidia na sisi, naomba unigongee thanks plz!
 
Mkuu mbona unakuwa na Myopia kiasi hicho?, Shughuli inafanywa na UN hii na kati ya walipiga kura ya kuidhinisha ni Nigeria, South Africa, Gabon. Hawa wao wanatekeleza kazi waliyotumwa tu.

Unajua ukiangalia sana wanaolaani kichapo hiki ni viongozi wa Afrika waliotaka kuset precedence baada ya Gaddafi kuendelea kutawala kwa kuua raia wasio na hatia na kuitumia wao kama mfano kuwatishia wananchi wa nchi zao ili waendelee kuwatawala kwa nguvu. Kichapo hiki kinatoa somo kwa wenye mawazo kama Gaddafi na Tanzania tukiwemo kuwa dola haiwezi kuwa ndiyo source of power bali ni wananchi kwa ridhaa yao. Pia inaongeza ujasiri kwa wale watakao taka kupinga serikali za kidikteta kuwa theya are not alone, hata kama watauwawa sheria itachukua mkondo wake.

Ule wakati wa kuua wananchi kama ilivyotokea Pemba 2001, Mwembechai 1998 na Arusha 2011 na hakuna accountability yoyote sasa unatakiwa kukoma. Ninaamini kabisa kuwa watawala wa Afrika wanaong'ang'ania madaraka kwa kuchakachua hii attack ya Libya itawatisha sana na kuwatia kiwewe.

Mkuu.
Nani aliandaa hiyo draft ya resolution?
Kama wao wanatekeleza kazi waliyopewa tu!!

Mimi sipingi haki ya walibya kudai mabadiliko. Tumeona yamefanyika Tunisia na Egypt hata pale wafaransa walipotaka rais wa Tunisia aendelee. Tumeona mabadiliko Egypt hata pale US walipotaka Mubarak aongoze reforms.

Kweli yalianza maandamano Libya lakini baada ya siku mbili tatu ,waandamanaji waligeuka waasi na silaha na kuanza vita na serikali. Gaddaffi awafanye nini?
Hata serikali inayoitwa dhaifu kama ipo basi itapambana na waasi. Gaddaffi aliwaoffer negotiations wamekataa.

US walipigana vita vya wenyewe kwa wenyewe kuzuia kumeguka kwa US..raia wengapi waliuawa katika vita ile?

Somalia ni mzozo wa miaka zaidi ya 20 sasa, West na US mbona hawaingilii kati kuzuia mauaji ya raia wasio na hatia wala silaha?

NATO na US wanaua raia wasio na hatia wala silaha huko Iraq na Afghanistan. Sasa niambie mkuu kule wametumwa na nani?

Tena kwa "uhuni" wao wanawaita wahanga hao collateral damage! sio massacre au genocide...wala sio human right violation.

Why Libya?

West overzealous on Libya
West overzealous on Libya - Opinion - Al Jazeera English#

OIL? Human Rights?
http://af.reuters.com/article/investingNews/idAFJOE72I0AD20110319
 
AU watafanya nini wakati budget yao 80% inatoka european union. It's a pity, hata suala la Ivory Coast limekua kama mchezo wa kuigiza.:embarassed2:
 
Hapa naona viongozi wa Africa sasa wameanza kuogopa wakijua kuwa wanaweza ondolewa madarakani pale wanapo kiuka haki za kibinadamu!

Na kwa kuwa wengi ni kama gadafi basi wanaanza "leo" kumtetea gadafi,kama vile alikuwa anaua sisimizi ati
 
Naamini wengi wenu mnafuata upepo baada ya kulishwa propaganda ya magharibi, haiwezekani kuua raia eti kumtoa Ghadafi, halafu nyie mnashabikia bila kujua adui namba moja wa dunia leo ni hizo nchi za magharibi, laiti kama mngekuwa mmefika Libya muelewe ukweli na si kushabikia uvamizi.

Je ni njia ya kijeshi tu ndio sahihi? Naamini wangetumia njia ya kidiplomasia kuliko matumizi ya nguvu kama haya, wanaoumia zaidi ni raia wa Libya na baada ya vita hii wataendelea kuteseka kama ilivyo Iraq, historia itawahukumu wote mnaoshabikia leo...nalaani uvamizi huu...
 
Hakuna haja ya Waafrika kwenda kumsaidia kiongozi dhalimu kama Ghadafi kwa yale yanayompata sasa kwani aliyataka mwenyewe. Kuna haja gani ya kuendelea kuwa na kiongozi huyo huyo kwa zaidi ya miaka 40 hata kama ni mzuri kiasi hicho? Ghadafi ametumia ndege zake za kivita kwenda kuwashambulia wananchi waliomchoka kwa lengo la kuwalazimisha waendelee kumpenda awaongoze, je hili tulihalalishe? Mimi binafsi nilikuwa mfuasi mzuri sana wa Ghadafi lakini kitendo cha kung'ang'ania madarakani maisha yake yote kimenifanya nimfikirie vibaya. Hivi kitendo cha yeye kuruhusu wafuasi wake wafunguliwe maghala ya silaha ili wazitumie kuwaua watu wanaompinga kukaa madarakani kwa zaidi ya umri wangu mimi tukiitaje, ni demokrasia ya kiafrika au uungwana wa kiafrika? Acha ashikishwe adabu nyang'au huyo.
 
Unajua Gadafi keshaua watu wangapi hadi sasa, umeyaona madege yake yanavyoshambulia raia wanaoitwa waasi. Wenye nyumba wameamua kumuondoa mpangaji, wacha wasaidiwe

Hao Rais ambao unaosema wewe sio waasi, walipata wapi silaha?
 
"You're either with us, or against us"

Huo ndio ushenzi unaoendelezwa na Mmarekani na vibaraka zake.
 
Naamini wengi wenu mnafuata upepo baada ya kulishwa propaganda ya magharibi,haiwezekani kuua raia eti kumtoa ghadafi,alafu nyie mnashabikia bila kujua adui namba moja wa dunia leo ni hizo nchi za magharibi,laiti kama mngekuwa mmefika libya muelewe ukweli na si kushabikia uvamizi,je ni njia ya kijeshi tu ndio sahihi?naamini wangetumia njia ya kidplomasia kuliko matumizi ya nguvu kama haya,,wanaoumia zaidi ni raia wa libya,na baada ya vita hii wataendelea kuteseka kama ilivyo iraq,,historia itawahukumu wote mnaoshabikia leo...nalaani uvamizi huu...


Adui wa Africa ni MWAFRIKA! Period!

Mengine ni hizo hizo propaganda unazowatuhumu wenzako! Kutufanya tuamini kwamba ni hujuma za 'imperialists' kutunyima umeme, mgao wa maji, bara bara mbovu, kipindupindu nk! I am always amazed by Africans intellectual laziness and the way we like blaming others for our predicaments! By the way hata Gbabo kasema ni hujuma za magharibi kwa matatizo yanayoendelea nchini mwake...
 
Je kitendo cha mataifa ya magharibi kumvamia kijeshi ni sahihi? Hoja yangu ni kwamba uvamizi huu utaleta maafa zaidi kuliko tija, bado dunia inaweza kutumia njia za amani na kidplomasia kumwondoa Ghadafi... ila hawataki kutumia diplomasia ili waweze kupora mafuta na kuharibu miundombinu ili wachukue hizo kandarasi
 
Je kitendo cha mataifa ya magharibi kumvamia kijeshi ni sahihi?hoja yangu ni kwamba uvamizi huu utaleta maafa zaidi kuliko tija,bado dunia inawez kutumia njia za amani na kidplomasia kumwondoa Ghadafi...ila hawataki kutumia diplomasia ili waweze kupora mafuta na kuharibu miundombinu ili wachukue hizo kandarasi

Mkuu hivi kwanza tupe njia mojawapo ya amani unayoona ingefaa kudeal na issue ya Ghadhafi.
 
Back
Top Bottom