Ati wachumi hii imekaaje?

Ati wachumi hii imekaaje?

nzalendo

Platinum Member
Joined
May 26, 2009
Posts
12,898
Reaction score
14,604
Mjukuu wangu ananijuza, babu kuliko kuweka fedha bank na kununua hisa, Kwanini watu wasinunue Dhahabu na ardhi tu?

Nikafikiria nikataka kumjibu nikanyamaza. Kwa hiyo na mimi nawaulizeni ninyi
mananke mie si mtaalamu wa inflation....
 
Mjukuu wangu ananijuza ,,,babuuu kuliko kuweka fedha bank na kununua ma hisa...kwa nini watu wasinunue Dhahabu na ardhi tu?..
Nikafikiria nikataka kumjibu nikanyamaza.....kwa hiyo na mimi namiulizeni ninyi,,,,,
mnanke mie si mtaalamu wa inflation....
Mjukuu wako ana hoja nzuri sana na ya kiakili, kwani dhahabu na ardhi ni rasilimali zinazoonekana kwa macho na ambazo zimekuwa zikitunza thamani yake kwa karne nyingi dhidi ya mfumuko wa bei (inflation).
Hata hivyo, kutoa majibu kwa misingi ya kifedha inahitaji uelewa wa usawa, kwani kila aina ya uwekezaji ina faida na mapungufu yake.
 
Dhahabu ni nzuri ila ardhi ni nzuri zaidi
Liquidity ya dhahabu na ardhi ipoje?
Wakati mwingine inaweza kutokea fursa au shida ya ghafla.
Ukahitaji hiyo rasilimali yako uuze upate pesa, au kunaweza kutokea vita ukaona bora uuze ukaishi nje ya nchi.
Je, ardhi au dhahabu kipi kitauzika haraka kwa thamani ileile au kubwa kuliko kabla ya vita?
 
Mjukuu wangu ananijuza, babuuu kuliko kuweka fedha bank na kununua ma hisa. Kwa nini watu wasinunue Dhahabu na ardhi tu?

Nikafikiria nikataka kumjibu nikanyamaza.....kwa hiyo na mimi namiulizeni ninyi,,,,,
mnanke mie si mtaalamu wa inflation....
Watu wanaofaidika na hisa wakisema wanunue Ardhi pengine Ardhi isiwatoshe, ama Dhahabu isiwatoshe etc wewe mwenzangu na Mimi nunua Ardhi badala ya hisa ila hao matajiri waachie wanunue Hisa.

MTU akiwekeza Bilioni 50 ama 100 kwenye hisa return yake ni kubwa kumwezesha kuishi kifahari, assume hisa ni 10000 na return ni sh 100 kila miezi 3 ina maana kila Bilioni 100 atapata angalau milioni 330 kila mwezi, inatosha kabisa kuishi vizuri Hadi Kufa, na pia mtaji wake kama kawekeza vizuri unakua, unaweza ukawekeza Bilioni 100 baada ya miaka ikawa bilioni 200.

Sasa mwenzangu na Mimi Una milioni 1 badala ya kununua kiwanja unaweka kwenye hisa unapata 10000 kila miezi 3 aka 3300 kwa mwezi, hio si ukila Ugali Tu siku moja imeisha?

Same kwa Dhahabu MTU alienunua Dhahabu 1980 akaiuza 2000 asingepata chochote cha maana Dhahabu imepanda Tu hivi karibuni na itashuka siku si nyingi, hakuna guarantee kwamba inapanda kila mwaka, kama Una Akili za kubeti kawekeza huko.
 
Haziingizi hela daily. Pia dhahabu ndiyo serikali inapata hela za kigeni. Hawapendi kabisa kuona wewe mwenye madafu unanunua na kukaa nayo. Wameweka vikwazo kibao ili mbongo wa kawaida usiweze kuimiliki.
Si kweli, watu wengi Hasa wa pwani huwekeza kwa watoto wao wa kike kuwanunulia Dhahabu, masonara wamejaa kibao Mjini, familia za wahindi, waarabu, hata Makabila ya Pwani Wadigo, wabondei, wapemba etc ni Jambo la kawaida kabisa MTU akiolewa, mtoto wa kike akizaliwa etc kupewa Dhahabu, hio mpaka Kufa kwake inakua ni backup ya Maisha, ngumu kwa mtoto wa kike kuteseka akiwa na Dhahabu zake.
 
Ningeshauri anunue hisa kwa lengo la kulinda thamani ya fedha na sio kupata faida.

Ikitokea amepata ardhi ya bei nafuu achukue coz Kuna muda utafika vizazi vyetu vitateseka sana kwa kukosa umiliki wa ardhi.

Thamani ya fedha inaweza kulindwa kupitia ardhi au hiyo hisa.

Achague Moja.
 
Si kweli, watu wengi Hasa wa pwani huwekeza kwa watoto wao wa kike kuwanunulia Dhahabu, masonara wamejaa kibao Mjini, familia za wahindi, waarabu, hata Makabila ya Pwani Wadigo, wabondei, wapemba etc ni Jambo la kawaida kabisa MTU akiolewa, mtoto wa kike akizaliwa etc kupewa Dhahabu, hio mpaka Kufa kwake inakua ni backup ya Maisha, ngumu kwa mtoto wa kike kuteseka akiwa na Dhahabu zake.
 
Sijajua mantiki ya Uzi wako uliolink na reply yangu, Tanzania utahangaika na vibali pale Tu unaposafirisha Madini "Ghafi" soma vizuri hio keyword Ghafi, Wengine mtaani Dhahabu ya hivyo wanaita Dhahabu chafu.

Ikishapita kwa sonara ukanunua Kihalali ukawa na risiti yako kudhibitisha Kodi umelipa vaa kama mkufu, bangili, Saa etc pita Airport nenda kokote hakuna atakaekusumbua.
 
Sijajua mantiki ya Uzi wako uliolink na reply yangu, Tanzania utahangaika na vibali pale Tu unaposafirisha Madini "Ghafi" soma vizuri hio keyword Ghafi, Wengine mtaani Dhahabu ya hivyo wanaita Dhahabu chafu.

Ikishapita kwa sonara ukanunua Kihalali ukawa na risiti yako kudhibitisha Kodi umelipa vaa kama mkufu, bangili, Saa etc pita Airport nenda kokote hakuna atakaekusumbua.
Achana na mapambo kwa sonara. Kuna duka unaweza kwenda na kununua dhahabu? Kwa wenzetu unaingia sehemu unakuta wanauza dhahabu kama coins au bars. Unanunua kama bidhaa zingine. Unaweza nunua online pia. Bongo serikali ikikukuta na dhahabu haina "vibali" ni kesi ya uhujumu uchumi.
 
Achana na mapambo kwa sonara. Kuna duka unaweza kwenda na kununua dhahabu? Kwa wenzetu unaingia sehemu unakuta wanauza dhahabu kama coins au bars. Unanunua kama bidhaa zingine. Unaweza nunua online pia. Bongo serikali ikikukuta na dhahabu haina "vibali" ni kesi ya uhujumu uchumi.
Hata hapa Tanzania kuna Coins, point ni kwamba isiwe Ghafi, inafanywa hivyo kuzuia utakatishaji Dhahabu watu wasiwe na machimbo feki na Serikali isipate mapato. Sonara wanafuatiliwa na ukinunua kwao ambayo imeshasafishwa unapunguza risk ya kununua Dhahabu haramu.

Na hayo mapambo unayosema yapo makubwa kushinda bars na coins, it's just watu ni artistic.

Na hata hio Dhahabu Ghafi sio kwamba vibali vyake ni complicated kivile kuna minada kibao ya Serikali Nchi nzima.
 
Haziingizi hela daily. Pia dhahabu ndiyo serikali inapata hela za kigeni. Hawapendi kabisa kuona wewe mwenye madafu unanunua na kukaa nayo. Wameweka vikwazo kibao ili mbongo wa kawaida usiweze kuimiliki.
Hivi Bongo huwezi nunua dhahabu ukaifadhi Bank?
 
Back
Top Bottom