ATCL kuanza na kosa la kwanza

ATCL kuanza na kosa la kwanza

Mkuu Mkinga naunga mkono hoja.
Ila pia kwa vile ni national flag carrier, it's high time Watanzania tuonyeshe uzalendo kwa shirika letu, tupande ndege zetu kwa faida ya kujenga nchi yetu tuache kuwafaidisha wageni.
Pasco
Mkuu naona ushamba unakuzidi.
Mtu hutumia huduma kwa kuangalia vigezo muhimu kwake.
Huwezi niambia nipande ndege zetu kisa tu ni uzalendo huku huduma zake ni mbovu.

Wewe mwenyewe sijui km unatumia mtandao wa TTCL. Ukitaka kwenda Kigoma au dodoma huwezi panda treni.

Sijui uzalendo unamaanisha nini?
Hao wengine waliokuja kufanya boashara ya ndege kwani wanafanya bure? Hawalipi kodi? Hawatoi ajira?

Usilete suala la biashara na siasa maji taka
 
Ili uweze kukata ticket mahali popote ulipo ni lazima utumie mawakala. Haijalishi unakata ticket kwenye ofisi, simu au kwenye laptop yako, utatumia wakala. Kutaka kila kitu ufanye wewe mwenyewe ndiyo mbinu ya kizamani ya kuendesha biashara.

Hivi unajua hata unapokata ticket yako na kulipia kupitia mitandao kama Airtel, Vodacom na wengineo unatumia wakala? Hii niliyoitoa hapa ni sehemu ya elimu maana usiamini kuwa wanaohitaji elimu ni wale watu wa chini kabisa, kila mtu anahitaji elimu kwenye jambo fulani. Watawala na viongozi wa serikali wanahitaji elimu pia kwenye masuala ya biashara kama ilivyo kwa mfanyabiashara akiingizwa serikalini atahitaji elimu juu ya jinsi serikali inavyofanya kazi. Hakuna anayejua kila kitu, ndiyo maana ukifanya biashara kwa kutaka ufanye kila kitu wewe mwenyewe lazima uangukie pua.

Anayekuonesha mahali penye hitilifu ndiye anayekujenga kuliko anayekushangilia kila mahali. Ndiyo maana hata kwenye management performance assessment wewe uliye boss unatakiwa uwaombe direct reports wako wakueleze your weaknesses na siyo your strengths. Hayo ya Deo RIP ni out of context.
Mungu akubariki sana .
 
ATCL kama yalivyo mashirika mengine ya umma, kila mara imekuwa ikizaliwa na kufa kutokana na muundo wake usiokuwa wa kibiashara. TANESCO isiyo na mshindani yeyote, TTCL ambayo awali haikuwa na mshindani, na mengine mengi yaliyokwishakufa na yaliyouzwa, mashirika yote hayo yalikufa kwa sababu yalianzishwa, kuendeshwa na kusimamiwa kiserikali/kisiasa.

Serikali haijawahi kuendesha biashara ikafanikiwa. Tatizo linaanzia kwenye muundo wa haya mashirika/makampuni. Wanasiasa/viongozi wa serikali ambao kimsingi si wafanyabiashara ndiyo waliotengeneza muundo wa uendeshaji na ndiyo wenye kauli ya mwisho. Vigezo vya wajumbe wa bodi na watendaji wakuu wanavyo wao. Na siku hizi PhD imekuwa ni kigezo kikubwa sana ingawa kiuhalisia, kwa Dunia nzima, ni nadra sana kuwaona wenye PhD wakiwa wafanyabiashara wazuri na waliofanikiwa.

Juzi wakati Mh. Rais akizindua ujio wa ndege mpya alisema ATCL imezaliwa upya, ina ndege mpya, bodi mpya na uongozi mpya, sikusikia kama ina muundo mpya wa uendeshaji na usimamizi. Bado inaonekana ATCL itandeshwa kwa mkono wa serikali.

RAIS - 'ATCL ISITUMIE MAWAKALA WA KUKATISHA TIKETI'

Hili tayari ni agizo ambalo naamini ni agizo lisilo sahihi. Tayari serikali imeanza toka hatua za mwanzo kuingilia uendeshaji wa ATCL. Rais anapoagiza ATCL isitumie mawakala wa kukatisha tiketi inamaanisha ATCL iwe na wafanyakazi waajiriwa kila mahali nchini. Gharama za maelekezo hayo itakuwa kama ifuatavyo:
  • ATCL italazimika kuwalipa wakatisha tiketi mishahara, matibabu, posho, michango kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii, usafiri, n.k. ATCL italazimika kulipia gharama hizo zote bila ya kujali mkatisha tiketi anakatisha tiketi ngapi au kama amepata wateja au hakupata kabisa
  • ATCL italazimika kulipia ofisi na kuweka miundombinu ya ukatishaji ticket nchi nzima. Ifahamike kuwa ukitaka kuwa na ufanisi unalazimika kuwa na ofisi za ukatishaji tiketi hata mahali ambapo ndege haitui, kwaajili ya kuhudumia abiria wanaotoka maeneo hayo wanaotarajia kutumia usafiri wa ATCL kutokea uwanja ulio karibu
  • ATCL italazimika kuwapa mafunzo wakatisha ticket watakaotapakaa nchi nzima
Wakati ATCL watakapokuwa wanahangaika na kuwa na wakatisha ticket wao na ofisi zao, washindani wao wataendelea kuwa na wafanyakazi wachache, wakiwa na mawakala wengi wanaolipwa kutokana na idadi ya ticket na thamani ya ticket walizokatisha. Hawalipii ofisi, hawalipii matibabu, hawalipii michango ya hifadhi ya jamii, hawalipii likizo ya mfanyakazi. Mawakala wao wanalipwa kutokana na wanachozalisha, wasipozalisha hawalipwi chochote.

ATCL wanaanza na quandary ya kwanza, wafuate maagizo ya mwenye mali au kanuni za biashara? Je, hii ni ya mwanzo na ya mwisho au zitaendelea kuja na nyingine? Kwa kuwa tatizo la msingi la uendeshaji biashara zilizo chini ya serikali halijatatuliwa, haitakuwa jambo la ajabu ATCL kufuata projectile ya mashirika/makampuni ya umma.
Hoja ni nzuri na zinazingatia misingi ya kuendesha biashara bila kuingiliwa na mmiliki wa biashara. Lakini kuna kipengele cha tekinolojia ya taarifa na mawasiliano ambayo ina nafasi kubwa ya kutoa huduma za kukata tuketi, kulipa na "check in" kwa mtandao. Kinachotakiwa ni kwa ATCL kuwekeza kwenye tekinolojia ya mawasiliano ya kisasa na itakayokuwa "responsive" kwenye mabadiliko.
 
Kaka dunia imebadilika unaweza kata ticket ya ndege popote ulipo bila msaada wa mtu yeyote kilichopo nikuchukua nafasi zetu katika jamii kutoa elimu au kuwasaidia kupata elimu waendane na dunia ya sasa kuleta ukinzani katika kila jambo linalokuwa initiated na serikali haliwezi kukufanya ukawa na busara za kuongoza bali kutatua changamoto zilizoko katika jamii yako ndio ngazi itakayokupandisha daraja na kuwa kiongozi. Je unamkumbuka Marehemu Deo Filikunjombe vaa viatu vyake vikikutosha basi hayo mambo mengine hayatakusumbua. Hongera Magufuli kwa kuonyesha tofauti hata sisi tusio wanachama wa ccm tunaona mwanga kupitia wewe.
Kama umeshanunua ticket za ndege kutumia wakala compare and contrast. nitoke kijijini niende mjini kufuata ofist za Air Tanzania au ninunue kwa wakala ambaye anapokea Airtelmoney, Tigo, Mpesa? Niende ofisini wakati wenyewe wako busy wanapaka wanja au nitumie wakala anayelipwa kwa ticket atakazouza au kwenye mtandao ambao aliyeniwekea salio kapata mgao? Watu wangapi duniani wanaenda kwehye ofisi za ndege kununua ticket? Wakala wakala wakala, Elimu elimu elimu jamani. Hivi kuna muda wa kukaa dirishani kukatisha ticket siku hizi? Ukiniona Emirate utue nataka kubadilisha tarehe ya kusafiri basi au nabadilisha njia ya kupita siyo niende kununa tick3et.
 
Kaka dunia imebadilika unaweza kata ticket ya ndege popote ulipo bila msaada wa mtu yeyote kilichopo nikuchukua nafasi zetu katika jamii kutoa elimu au kuwasaidia kupata elimu waendane na dunia ya sasa kuleta ukinzani katika kila jambo linalokuwa initiated na serikali haliwezi kukufanya ukawa na busara za kuongoza bali kutatua changamoto zilizoko katika jamii yako ndio ngazi itakayokupandisha daraja na kuwa kiongozi. Je unamkumbuka Marehemu Deo Filikunjombe vaa viatu vyake vikikutosha basi hayo mambo mengine hayatakusumbua. Hongera Magufuli kwa kuonyesha tofauti hata sisi tusio wanachama wa ccm tunaona mwanga kupitia wewe.
Duh!! Sasa mwenzako katoa fact za kibiashara na solution ili shirika lijiendeshe kwa faida na wewe unakuja kutoa hisia na maoni ya kijiwen!!
Ukweli ni Kwamba Mtukufu kachemka, kama anataka shirika lijiendeshe awaachie wataalam wa biashara na uchumi wafanye kazi yao.
 
Air Tanzania haiwezi kufanikiwa chini ya akili za awamu ya tano kwa sababu nazo ni akili zilezile za awamu za nyuma zilizoliua shirika, tofauti tu ni kwamba za awamu hii zimejaa kufokafoka zaidi.
Endelea tu kuombea mabaya,alienunua ndege mbili mpya kwa mpigo,na wewe nani ana akili?
Shirika halijawahi kunua ndege tokea 1978
 
Sasa, kama ndiyo mawakala wenyewe na ATCL ikipata fedha moja kwa moja kutoka kwa mteja kupitia website yao bila hao mawakala, hilo si ni jambo zuri sana?
Unajua matatizo ya website ikizidiwa na visitors?, database inaweza ika ikafail kwa kipindi kifupi ndio maana msaada unahitajika
 
Kaka,
Inasemekana ukitoa ushauri murua ka huu weye ni chocheziii kwa sababu umepinga maagizo au unasababisha watu wapinge maagizo. Lakini, umeeleza kiufasaha japo tofauti ni heading yako ila wenye akili wamesikia ujumbe.
Swali ni Je, kuna CEO atakayethubutu hata kujifanya kasahau maelekezo afuate ushauri wako murua?? Hapo sasa kwa sababu atakuwa ameokoa nyingi tu. Lakini huwezi kujua, pengine kuna mtu wangu au nyumba yangu nataka viufaidi mchezo huu kwa maagizo kufuatwa. Mkija ng'amua nimeshapata angalao nusu.

GO JPM DK GOO

TUSISIKILIZE WANAOTAKA KUKUWEKA KWENYE HISTORIA YA KUUA ATCL
 
Kama umeshanunua ticket za ndege kutumia wakala compare and contrast. nitoke kijijini niende mjini kufuata ofist za Air Tanzania au ninunue kwa wakala ambaye anapokea Airtelmoney, Tigo, Mpesa? Niende ofisini wakati wenyewe wako busy wanapaka wanja au nitumie wakala anayelipwa kwa ticket atakazouza au kwenye mtandao ambao aliyeniwekea salio kapata mgao? Watu wangapi duniani wanaenda kwehye ofisi za ndege kununua ticket? Wakala wakala wakala, Elimu elimu elimu jamani. Hivi kuna muda wa kukaa dirishani kukatisha ticket siku hizi? Ukiniona Emirate utue nataka kubadilisha tarehe ya kusafiri basi au nabadilisha njia ya kupita siyo niende kununa tick3et.

Mkuu, ni wakala yupi unaemtetea, anaechukua kamisheni (tigo Pesa, Airtel Money) au yule wakala wa safari anaetambulika yaani travel agent?

Anaechukua kamisheni (makampuni ya simu) hawahusiki na tiketi kwasababu hawajawa travel agents, wao wanangoja kukata tu kamisheni.
 
Unajua matatizo ya website ikizidiwa na visitors?, database inaweza ika ikafail kwa kipindi kifupi ndio maana msaada unahitajika

Nimeeeleza hapo juu kuhusu hilo la website, ikiwa imara haiwezi kusumbuliwa kiasi hicho yaani abiria 76 wanagombea tiketi za ndege moja tu ya Q400NG?

Ndiyo maana nikasema, wanahitaji kuwekeza kwenye IT.

Yaani kila ikifika usiku saa sita wataalam wanaingia kazini wanafanya updates na mengine.
 
Mkuu naona ushamba unakuzidi.
Mtu hutumia huduma kwa kuangalia vigezo muhimu kwake.
Huwezi niambia nipande ndege zetu kisa tu ni uzalendo huku huduma zake ni mbovu.

Wewe mwenyewe sijui km unatumia mtandao wa TTCL. Ukitaka kwenda Kigoma au dodoma huwezi panda treni.

Sijui uzalendo unamaanisha nini?
Hao wengine waliokuja kufanya boashara ya ndege kwani wanafanya bure? Hawalipi kodi? Hawatoi ajira?

Usilete suala la biashara na siasa maji taka
Kusema ukweli, give a dog a bad name and hang it!, mtu unajiita ibilisi na kweli mawazo yake yanakuwa ya kishetani shetani tuu! .

Uzalendo ni mapenzi ya dhati ya nchi yako na taifa lako. Hao wengine yes wanalipa kodi na ni kweli wanatoa huduma nzuri ila wanatukamua sana na faida wanapeleka kwao.

Ukipanda ATC, unajenga chako, faida yote ni yako na watoto wako na watoto wa watoto wako.
Pasco
 
Nimeeeleza hapo juu kuhusu hilo la website, ikiwa imara haiwezi kusumbuliwa kiasi hicho yaani abiria 76 wanagombea tiketi za ndege moja tu ya Q400NG?

Ndiyo maana nikasema, wanahitaji kuwekeza kwenye IT.

Yaani kila ikifika usiku saa sita wataalam wanaingia kazini wanafanya updates na mengine.
ila kwa sasa wanahitaji usaidizi mpaka hapo watakapo jihimarisha
 
Kaka dunia imebadilika unaweza kata ticket ya ndege popote ulipo bila msaada wa mtu yeyote kilichopo nikuchukua nafasi zetu katika jamii kutoa elimu au kuwasaidia kupata elimu waendane na dunia ya sasa kuleta ukinzani katika kila jambo linalokuwa initiated na serikali haliwezi kukufanya ukawa na busara za kuongoza bali kutatua changamoto zilizoko katika jamii yako ndio ngazi itakayokupandisha daraja na kuwa kiongozi. Je unamkumbuka Marehemu Deo Filikunjombe vaa viatu vyake vikikutosha basi hayo mambo mengine hayatakusumbua. Hongera Magufuli kwa kuonyesha tofauti hata sisi tusio wanachama wa ccm tunaona mwanga kupitia wewe.
mkuu akili yako huilipii bili. Jaribu kutumia hyo rasilimali uliyopewa Bure angalia ukiwa hai
 
Mkuu Msambichaka, kwenye digital world, inawezekana kabisa kuuza tiketi online bila kuwatumia mawakala. Mawakala wanaozungumzwa hapa sio mawakala traveling agents, bali mawakala commissioned agents wana operate kama ofisi za
ATCL, badala ya kutumia mawakala, wanauza tickets on line. Fast Jet wana ofisi zao kule tuu mdege yao inakotua, na hawana wakala popote na mauzo yote ni online!, ila kwa mujibu wa sheria ya kimataifa ya shirika la kimataifa la wakala wa usafiri wa Anga, IATA, wakala yoyote aliyesajiliwa IATA kupitia mtandao wa Galileo, anaweza jyfanya booking yoyote ya ndege yoyote, hivyo abiria wa Tanzania yote watapata tiketi za ATCL popote kupitia traveling agents wengine, ila kule ATCL inatua, lazima wawe na agents for clearing.

Pasco

Sasa hivi inawezekana mtu akalipia tiketi yake hata kwa m-pesa, akapata SMS yenye namba ya ticket na akifika airport atapata ticket halisi na kusafiri. Kwa hiyo wafanyakazi 'redundant' hawana nafasi tena!
 
Daktari wa kupasua goti vs kichwa and vice versa. Unaweza ukawa daktari lakini ukawa na mapungufu tena kama ulisoma hivi vyuo vya "leo", mhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh AU wale wa Urusi enzi hizo waliokuwa hawakubaliki Muhimbili!
Anyway nataka kukupa notion kuwa issue siyo una profession gani, issue je unaimudu? Si umesikia utafiti unasema kuwa around 46% ??? walimu na madaktari hawajui kazi zao!???????
We labda ulitaka niimuduje? Maana mwenzio yule kashiba maharage ya wapi sijui kiasi kavimbiwa na mbaya zaidi yuko katikati ya watu anaogopa kupunguza gesi, matokeo yake anaongea 'pembejeo' na mbolea ya mboji. Kitendo cha kufahamu kuwa ana tatizo 'diagnosis' kinatosha kukuambia wewe kuwa mimi si daktari wa kufunga vituo vya tiba asili, bali ni daktari wa kutibu maradhi.

Namshukuru Mungu sikusoma kabisaaaaaa.
 
Back
Top Bottom