ATCL kuanza na kosa la kwanza

ATCL kuanza na kosa la kwanza

Mkuu Msambichaka, kwenye digital world, inawezekana kabisa kuuza tiketi online bila kuwatumia mawakala. Mawakala wanaozungumzwa hapa sio mawakala traveling agents, bali mawakala commissioned agents wana operate kama ofisi za
ATCL, badala ya kutumia mawakala, wanauza tickets on line. Fast Jet wana ofisi zao kule tuu mdege yao inakotua, na hawana wakala popote na mauzo yote ni online!, ila kwa mujibu wa sheria ya kimataifa ya shirika la kimataifa la wakala wa usafiri wa Anga, IATA, wakala yoyote aliyesajiliwa IATA kupitia mtandao wa Galileo, anaweza jyfanya booking yoyote ya ndege yoyote, hivyo abiria wa Tanzania yote watapata tiketi za ATCL popote kupitia traveling agents wengine, ila kule ATCL inatua, lazima wawe na agents for clearing.

Pasco

Nafikiri Hapa Pasco umeconclude ubishani mwingine unaondelea ni siasa
 
ATCL ikisimamiwa na serikali ndio haswa itafanya kazi kwa weledi.

Kitu ambacho serikali inatakiwa kufanya ni kwamba wahakikishe HAKUNA ANAEPANDA BURE ndani ya ndege ile! hiki ndio kiliua shirika! kila mmoja anataka kupanda bure watu wakatumia ndege ile kujifaidisha!

Tumeona FAst Jet kwenda bila mzigo wa fare zao na ukiongeza mzigo wana fare zao! kinwaji ndani ya ndege ununue mwenyewe after all hapa na mwanza cha nini kupewa bure!

Nadhani tutaweza kama atatokea Mkurugenzi na Bodi ya wazalendo! kufanya kazi kwa uthubutu na weledi na UADILIFU! tatizo je hawa sio wale ambao wakichaguliwa wanawaza KUPIGA?

kingine ndugu yangu haihitaji kuweka mawakala sasa hivi unalogin kwenye website ya Airline yeyote ile unakata ticket yako kwa kutumia Visa card za CRDB, na mitandao yote ya simu bila wewe kwenda Ofisini! ukimuingiza wakala ndio mwanzo wa kujifilisi!

KUna mtu alitoa wazo hapa kwamba serikali ingeliacha ATCL na kufungua Tanzania Airways, nadhani that was a good move! serikali ingeajiri watu wapya kabisa wenye muonekano mpya! lakini hawa hawa mmmmh nna wasiwasi

Yote kwa yote Hongera sana Serikali Hongera MAgufuli Hongera CCM tuwape muda tuone!
 
Sio kweli...

Siku hizi watu wanakata ticket online...Fastjet watu wanakata ticket online..Precision hivyohivyo...

Mashirika yote ya ndege ya nje KW, Emirates, Qatar, Etihad n.k wanakata ticket online...

Ukienda JNIA..KIA..Songwe na viwanja vingine unakata ticket bila kutumia Wakala.
Stomach gases humnyima mtu wasaa wa kufikiri vyema.
Hebu fungua website ya hilo shirika letu lenye Eicher 2 mpya zinazowapa wazimu wa kujilinganisha na Emirates halafu ndio utajua tunazungumzia ndoto zenu badala ya uhalisia.

Neno ONLINE linawafurahisha sana japo haliendani na mazingira ya shirika na uelewa wa wananchi. Tudege tuwili twa watu 70 kama DCM tayari tunataka kuwa exceptional kisa wazo tukufu. Nje ya ofisi yangu hapa kuna wakala anauza Fast Jet, Precision na Qatar Airways.

Hizi za kwenu kupunguza gharama wapeni tu Makatibu Kata wa CCM wauze
 
Air Tanzania haiwezi kufanikiwa chini ya akili za awamu ya tano kwa sababu nazo ni akili zilezile za awamu za nyuma zilizoliua shirika, tofauti tu ni kwamba za awamu hii zimejaa kufokafoka zaidi.
Let us excise professionalism! Rais afanye monitoring of what is going on, lakini awaachie wataalamu wafanye kazi with a close eye on what is going on! Awaite wataalamu wa aviation industry, tena mashirika yaliyofanikiwa sana aombe ushauri. This is because he is very much concerned with the health of ATCL!
 
Kaka dunia imebadilika unaweza kata ticket ya ndege popote ulipo bila msaada wa mtu yeyote kilichopo nikuchukua nafasi zetu katika jamii kutoa elimu au kuwasaidia kupata elimu waendane na dunia ya sasa kuleta ukinzani katika kila jambo linalokuwa initiated na serikali haliwezi kukufanya ukawa na busara za kuongoza bali kutatua changamoto zilizoko katika jamii yako ndio ngazi itakayokupandisha daraja na kuwa kiongozi. Je unamkumbuka Marehemu Deo Filikunjombe vaa viatu vyake vikikutosha basi hayo mambo mengine hayatakusumbua. Hongera Magufuli kwa kuonyesha tofauti hata sisi tusio wanachama wa ccm tunaona mwanga kupitia wewe.


Naona uwelewi maana ya wakala hicho unachokiongea hapo tayari ni wakala huyo
 
ATCL ikisimamiwa na serikali ndio haswa itafanya kazi kwa weledi.

Kitu ambacho serikali inatakiwa kufanya ni kwamba wahakikishe HAKUNA ANAEPANDA BURE ndani ya ndege ile! hiki ndio kiliua shirika! kila mmoja anataka kupanda bure watu wakatumia ndege ile kujifaidisha!

Tumeona FAst Jet kwenda bila mzigo wa fare zao na ukiongeza mzigo wana fare zao! kinwaji ndani ya ndege ununue mwenyewe after all hapa na mwanza cha nini kupewa bure!

Nadhani tutaweza kama atatokea Mkurugenzi na Bodi ya wazalendo! kufanya kazi kwa uthubutu na weledi na UADILIFU! tatizo je hawa sio wale ambao wakichaguliwa wanawaza KUPIGA?

kingine ndugu yangu haihitaji kuweka mawakala sasa hivi unalogin kwenye website ya Airline yeyote ile unakata ticket yako kwa kutumia Visa card za CRDB, na mitandao yote ya simu bila wewe kwenda Ofisini! ukimuingiza wakala ndio mwanzo wa kujifilisi!

KUna mtu alitoa wazo hapa kwamba serikali ingeliacha ATCL na kufungua Tanzania Airways, nadhani that was a good move! serikali ingeajiri watu wapya kabisa wenye muonekano mpya! lakini hawa hawa mmmmh nna wasiwasi

Yote kwa yote Hongera sana Serikali Hongera MAgufuli Hongera CCM tuwape muda tuone!
Wewe unaongea kama unatoka Mkuranga! Penye red hao wote ni mawakala ila they operate electronically! Soma humu wameandika sana kuhusu hao agents wa digital world!
 
naona element za "UCHOCHEZI"..mkuu,nakuunga mkono maana umetumia macho kutazama matukio yote,umetumia masikio kusikia matukio yote na sasa unatumia mdomo kutoa ushuhuda wa matukio yote..
mkuu umeeleweka vizuri.
 
Kuwa na elimu nusu ni hatari zaidi kuliko kutokuwa na elimu kabisa. Yaani mtu anasimama kutaka kumpinga tu Magufuli bila kuzingatia mabadiliko ya kiteknolojia hasa ya malipo katika dunia ya leo.

BAVICHA wana kipindi kigumu sana safari hii kumkosoa Magufuli.
kodi zenyewe zinalipwa kwa kutumia mawakala, tunaomba kabla ya kuchangia soma mada vizuri na uelewe
 
Tatizo wengi wanadhani wakala ni lazima akae ofisini wamwone. Unapokata ticket online ya fastjet au Precision au kampuni nyingine yoyote, pale kuna wakala, na kuna wakati kunakuwa na mawakala wawili. Kwa fastjet kuna mtandao unaokuwezesha ufanye hayo malipo (Mpesa, Airtel Money, MaxMalipo, etc) na pia kuna PayPal ambaye ndiye wakala wa Fastjet.

Kwa hiyo kwa ujumla unazidi kuniunga mkono kuwa ni ngumu sana kwa ulimwengu wa leo kufanya biashara 100% bila ya kutumia wakala.
Mkuu, tatizo watu bado wanafikiri kizamani huku wakitaka kuonyesha kuwa wanakwenda na wakati.
Wakala sio lazima uwe kwenye kibanda chako..!!
Hivi unapofanya booking online, unadhani hiyo transaction / muamala yako/wako unafanyikaje?? Unawatumia akina nani hadi pesa ifike kwa airline?
 
Heshima yako mkuuu...

Nililiona anguko la atcl kabla hata hizo ndege hazijafika.

Tujikumbushe
Tanesco
Ttcl
Shirika la reli
Vimekufaje?? Muuwaji wa mashirika haya ni serikali kuweka siasa kwenye huduma na biashara.
Shirika la ndege siku zote linahitaji watu smart...caring ya private ni tofauti sana na shirika la umma
 
Ticket tunauza kwa M-pesa, airtel money, tigo pesa na booking online ukifika airport unaonyesha ticket kwenye simu yako huhitaji kubeba karatasi wala kukutana na mtu atakayekudanganya kuwa ndege imejaa. Chagua kiti online ofisi za nini acha basi Mkuu
 
Mkuu Msambichaka, kwenye digital world, inawezekana kabisa kuuza tiketi online bila kuwatumia mawakala. Mawakala wanaozungumzwa hapa sio mawakala traveling agents, bali mawakala commissioned agents wana operate kama ofisi za
ATCL, badala ya kutumia mawakala, wanauza tickets on line. Fast Jet wana ofisi zao kule tuu mdege yao inakotua, na hawana wakala popote na mauzo yote ni online!, ila kwa mujibu wa sheria ya kimataifa ya shirika la kimataifa la wakala wa usafiri wa Anga, IATA, wakala yoyote aliyesajiliwa IATA kupitia mtandao wa Galileo, anaweza jyfanya booking yoyote ya ndege yoyote, hivyo abiria wa Tanzania yote watapata tiketi za ATCL popote kupitia traveling agents wengine, ila kule ATCL inatua, lazima wawe na agents for clearing.

Pasco
Unadhani fastjet hawana online booking??? Kwa nini wawe na mawakala???

Watanzania wangapi wanauwezo wa kufanya booking online....??
 
Stomach gases humnyima mtu wasaa wa kufikiri vyema.
Hebu fungua website ya hilo shirika letu lenye Eicher 2 mpya zinazowapa wazimu wa kujilinganisha na Emirates halafu ndio utajua tunazungumzia ndoto zenu badala ya uhalisia.

Neno ONLINE linawafurahisha sana japo haliendani na mazingira ya shirika na uelewa wa wananchi. Tudege tuwili twa watu 70 kama DCM tayari tunataka kuwa exceptional kisa wazo tukufu. Nje ya ofisi yangu hapa kuna wakala anauza Fast Jet, Precision na Qatar Airways.

Hizi za kwenu kupunguza gharama wapeni tu Makatibu Kata wa CCM wauze
Hivi kuna sehemu nimeifananisha ATCL na Emirates?
 
Mkuu aliyeleta hoja amesema vizuri sana. Tujifunze kwa nini TANESCO imeshindwa kufanya biashara kwa faida ndipo tutajua ni kwa changamoto zilizo mbele ya ATCL. Wengine tukisema sana sasa tutaonekana kama tunapingana au kukatisha tamaa juhudi za serikali. Lakini ni heri kusema, kuliko kuwa mjinga. Biashara ya ndege ni ngumu sana. Hata Kenya Airways ambao wamekuwa wakifanya vizuri East Africa kwa miaka mingi, sasa wako hoi. Sina hakika kama watendaji wetu wamebadilika. Tuache muda utoe majibu ya uhakika.
 
Naamini upon sahihi kwa asilimia nyingi kama si zote kabisa. ATCL na mashirika mengine ni lazima yajiendeshe kibiashara kama kweli yanahitaji kyendelea. Vinginevyo hadithi utakuwa ni ile ile ya kufanya na kufufuka.
 
Sio kweli...

Siku hizi watu wanakata ticket online...Fastjet watu wanakata ticket online..Precision hivyohivyo...

Mashirika yote ya ndege ya nje KW, Emirates, Qatar, Etihad n.k wanakata ticket online...

Ukienda JNIA..KIA..Songwe na viwanja vingine unakata ticket bila kutumia Wakala.

Yes, lakini bado Fasjet ina agents! Tanzania haijafikia level ya Ulaya mzee. Hata ukiwa na online systems, lazima pia uwe na agents.......
 
wenyewe wenye nini? tuliwaachia ndege kibao tu zote wameua, nazo hizi unataka waziue?
Mkuu mimi nilivyomuelewa KARME alikuwa anamaanisha ATCL watatoa mapendekezo serikalini aina ya ndege wanayotaka kununua kwa mahitaji ya soko lililopo.
 
Pasco, hizi ndege tutazipanda. Nimezitumia mara nyingi, ni nzuri kwa ujumla. Na kwa usafiri wa ndani ni uamuzi mzuri, japo kuna wakati tunazidisha sana katika kusifia. Hakuna mtu anayependa nchi hii tusiwe na cha kujivunia, ingewezekana kila Mtanzania angependa nchi yetu iwe bora kwa kila kitu kushinda nchi yoyote ya Kiafrika. Lakini hayo hayaji yenyewe bila ya jamii yetu kuwa na uwezo wa kutafakari, kujadiliana, kukosoana, kuwajibishana, dhamira ya kweli na mshikamano na umoja kwenye mambo ya msingi. Huwezi kuwa na uwezo zaidi au akili zaidi kwa kuwa kwenye chama fulani au kwa kuwa na cheo fulani. Tukikubali ukweli huo, tutaona faida ya kuwa wengi maana yake una mawazo mengi na una machaguo mengi kutoka kwenye mawazo ya watu wengi.

Tunachoiomba serikali na ATCL wayasikilize maoni ya wadau mbalimbali, hawawezi kuyachukua yote lakini yenye mantiki na uhalisia wayachukue, wayachukue kwa kutegemea uzito wa hoja na wala siyo kwa uzito wa yule aliyeyatoa maana biashara ina miiko yake, na miiko hiyo ni universal haiiangalii wewe unayefanya biashara una mamlaka au huna mamlaka, kama ni serikali au mtu/kampuni binafsi.

ATCL ikitaka kufanikiwa iiangalie biashara yenyewe na kuielewa isiingalie serikali na kuifanya biashara ifuate matakwa ya serikali. Serikali kwa upande wake ianze kuangalia ni namna gani itafanya ili kuhakikisha umiliki wake ndani ya shirika, kwa siku zijazo ushuke mpaka ufikie angalao 40%. Hiyo italisaidia shirika kuendeshwa kibiashara kwa 100%. Umiliki uliobakia wauziwe watanzania wananchi, na makampuni mengine ya ndani yasiyofanya biashara ya usafiri wa anga.

Mkuu Mkinga naunga mkono hoja.
Ila pia kwa vile ni national flag carrier, it's high time Watanzania tuonyeshe uzalendo kwa shirika letu, tupande ndege zetu kwa faida ya kujenga nchi yetu tuache kuwafaidisha wageni.
Pasco
 
Back
Top Bottom