ATCL kuanza na kosa la kwanza

ATCL kuanza na kosa la kwanza

Sio lazima. Unaweza kufanya kila kitu online kutumia website ya shirika husika.
 
Hoja hapa ni serikali/wanasiasa kuingilia uendeshaji wa haya makampuni ya umma. Haya maelekezo sio mara zote yanaweza kusaidia kampuni, mengine yana hatari zake. Ni vema bodi na menejimenti zikaachwa huru kwenye uendeshaji. Serikali kama mmiliki iipe bodi ya ATCL, Targets and kuweka KPIs tu ambazo kwazo itakuwa inapima performance ya hiyo bodi/menejimenti.
 
ATCL kama yalivyo mashirika mengine ya umma, kila mara imekuwa ikizaliwa na kufa kutokana na muundo wake usiokuwa wa kibiashara. TANESCO isiyo na mshindani yeyote, TTCL ambayo awali haikuwa na mshindani, na mengine mengi yaliyokwishakufa na yaliyouzwa, mashirika yote hayo yalikufa kwa sababu yalianzishwa, kuendeshwa na kusimamiwa kiserikali/kisiasa.

Serikali haijawahi kuendesha biashara ikafanikiwa. Tatizo linaanzia kwenye muundo wa haya mashirika/makampuni. Wanasiasa/viongozi wa serikali ambao kimsingi si wafanyabiashara ndiyo waliotengeneza muundo wa uendeshaji na ndiyo wenye kauli ya mwisho. Vigezo vya wajumbe wa bodi na watendaji wakuu wanavyo wao. Na siku hizi PhD imekuwa ni kigezo kikubwa sana ingawa kiuhalisia, kwa Dunia nzima, ni nadra sana kuwaona wenye PhD wakiwa wafanyabiashara wazuri na waliofanikiwa.

Juzi wakati Mh. Rais akizindua ujio wa ndege mpya alisema ATCL imezaliwa upya, ina ndege mpya, bodi mpya na uongozi mpya, sikusikia kama ina muundo mpya wa uendeshaji na usimamizi. Bado inaonekana ATCL itandeshwa kwa mkono wa serikali.

RAIS - 'ATCL ISITUMIE MAWAKALA WA KUKATISHA TIKETI'

Hili tayari ni agizo ambalo naamini ni agizo lisilo sahihi. Tayari serikali imeanza toka hatua za mwanzo kuingilia uendeshaji wa ATCL. Rais anapoagiza ATCL isitumie mawakala wa kukatisha tiketi inamaanisha ATCL iwe na wafanyakazi waajiriwa kila mahali nchini. Gharama za maelekezo hayo itakuwa kama ifuatavyo:
  • ATCL italazimika kuwalipa wakatisha tiketi mishahara, matibabu, posho, michango kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii, usafiri, n.k. ATCL italazimika kulipia gharama hizo zote bila ya kujali mkatisha tiketi anakatisha tiketi ngapi au kama amepata wateja au hakupata kabisa
  • ATCL italazimika kulipia ofisi na kuweka miundombinu ya ukatishaji ticket nchi nzima. Ifahamike kuwa ukitaka kuwa na ufanisi unalazimika kuwa na ofisi za ukatishaji tiketi hata mahali ambapo ndege haitui, kwaajili ya kuhudumia abiria wanaotoka maeneo hayo wanaotarajia kutumia usafiri wa ATCL kutokea uwanja ulio karibu
  • ATCL italazimika kuwapa mafunzo wakatisha ticket watakaotapakaa nchi nzima
Wakati ATCL watakapokuwa wanahangaika na kuwa na wakatisha ticket wao na ofisi zao, washindani wao wataendelea kuwa na wafanyakazi wachache, wakiwa na mawakala wengi wanaolipwa kutokana na idadi ya ticket na thamani ya ticket walizokatisha. Hawalipii ofisi, hawalipii matibabu, hawalipii michango ya hifadhi ya jamii, hawalipii likizo ya mfanyakazi. Mawakala wao wanalipwa kutokana na wanachozalisha, wasipozalisha hawalipwi chochote.

ATCL wanaanza na quandary ya kwanza, wafuate maagizo ya mwenye mali au kanuni za biashara? Je, hii ni ya mwanzo na ya mwisho au zitaendelea kuja na nyingine? Kwa kuwa tatizo la msingi la uendeshaji biashara zilizo chini ya serikali halijatatuliwa, haitakuwa jambo la ajabu ATCL kufuata projectile ya mashirika/makampuni ya umma.
Jawabu ni kutumia ICT katika kufanya booking, kulipa na boarding pass.
 
Wewe lijamaa ni liongo na linafiki. Hujui biashara ya ndege na hujawahi kutumia usafiri wa ndege kama unavyosafiri na basi tofauti na sisi wengine tulioishi nje na kuishi maisha ya kupanda ndege kama wewe unavyopanda basi kwenda kijijini kwako. Alichokisema rais ni sahihi, siku hizi kuna ma mpesa, tigopesa, etc etc, je kuna haja ya kuwa na ofisi nyingi? Huo ni mfano mmoja, ipo mingi wengine wameonesha. Juu ya PhD na ufanyaji biashara, wewe ni mbumbu na umerukwa na akili. Rais anatumia PhD holders ili waweze kufanya maamuzi yenye ushahidi wa kitafiti au hata kama ni ngumu basi wafanye tafiti kabla ya maamuzi, tofauti na wenye MBA au bachelor, wengi tafiti na umuhimu wa tafiti hawajui, na kama wanajua ni kwa mbaali sana. Ndiyo maana USA na obama imepiga hatua kwa sababu ya PhD holders na obama ni PhD holder.
Ajifunze kwa mashirika kama ryana air wanavyotengeneza faida kwa kutumia ICT Ryanair Flights Search - Search for prices & book Ryanair flights online
 
Ili uweze kukata ticket mahali popote ulipo ni lazima utumie mawakala. Haijalishi unakata ticket kwenye ofisi, simu au kwenye laptop yako, utatumia wakala. Kutaka kila kitu ufanye wewe mwenyewe ndiyo mbinu ya kizamani ya kuendesha biashara.

Hivi unajua hata unapokata ticket yako na kulipia kupitia mitandao kama Airtel, Vodacom na wengineo unatumia wakala? Hii niliyoitoa hapa ni sehemu ya elimu maana usiamini kuwa wanaohitaji elimu ni wale watu wa chini kabisa, kila mtu anahitaji elimu kwenye jambo fulani. Watawala na viongozi wa serikali wanahitaji elimu pia kwenye masuala ya biashara kama ilivyo kwa mfanyabiashara akiingizwa serikalini atahitaji elimu juu ya jinsi serikali inavyofanya kazi. Hakuna anayejua kila kitu, ndiyo maana ukifanya biashara kwa kutaka ufanye kila kitu wewe mwenyewe lazima uangukie pua.

Anayekuonesha mahali penye hitilifu ndiye anayekujenga kuliko anayekushangilia kila mahali. Ndiyo maana hata kwenye management performance assessment wewe uliye boss unatakiwa uwaombe direct reports wako wakueleze your weaknesses na siyo your strengths. Hayo ya Deo RIP ni out of context.
Duh pamoja na busara nyingi ulizozitoa hapo juu katika mchanganuo wako, lakini naona umesifiwa na umeamua kulitia maji, ningekuuliza swali dogo sana hivi ukitaka kununua chakula kutoka Tesco online utatumia mawakala?????
 
Ajifunze kwa mashirika kama ryana air wanavyotengeneza faida kwa kutumia ICT Ryanair Flights Search - Search for prices & book Ryanair flights online
Hiyo search inachakifanya ni kukupeleka katika website ya mashirika na mawakala mbali mbali hivyo sijui mantiki ya comment yako.
Mkuu Msambichaka, kwenye digital world, inawezekana kabisa kuuza tiketi online bila kuwatumia mawakala. Mawakala wanaozungumzwa hapa sio mawakala traveling agents, bali mawakala commissioned agents wana operate kama ofisi za
ATCL, badala ya kutumia mawakala, wanauza tickets on line. Fast Jet wana ofisi zao kule tuu mdege yao inakotua, na hawana wakala popote na mauzo yote ni online!, ila kwa mujibu wa sheria ya kimataifa ya shirika la kimataifa la wakala wa usafiri wa Anga, IATA, wakala yoyote aliyesajiliwa IATA kupitia mtandao wa Galileo, anaweza jyfanya booking yoyote ya ndege yoyote, hivyo abiria wa Tanzania yote watapata tiketi za ATCL popote kupitia traveling agents wengine, ila kule ATCL inatua, lazima wawe na agents for clearing.

Pasco
Pasco umesaidia hapo kaka salute
 
Haaaaa haaa raisi wetu anaamini sana katika phd atembee akawaone akina bilgate kama wanazo ama yule dingi wa virgin.Biashara inahitaji madirector talented na motivated dirctor mmoja ana impact kubwa sana katika ufanisi wa serikali. Ni lazima hata kama ATCL italuwa na mkono wa serilali basi ijiandae kuwa flexible na kumake changes kutokana na issue.ndogondogo ila sifa moja ya serikali yoyote duniani ni ukiritimba kwani baadhi ya taratibu ni lazima zifuate channel ama mpaka bunge liamue huku mambo yameshaharibika na ndo maana haziwezi fanya biashara na biashara zinahitaji ultimate.responce
 
Hoja nzuri sana ndugu yangu. Kwa hili ATCL inaanza vibaya.
 
Pasco nakubaliana nawe kuwa siku hizi mashirika ya ndege karibia yote Duniani yanatumia online services. Lakini hata huko kuna agents. Unaposema ATCL wasitumie mawakala, ina maanisha itakuwa na miundombinu yao? Lakini pia tusiukatae ukweli kuwa bado watanzania wengi hawatumii online services. Ndiyo maana ukienda ofisi za fastjet, pamoja na kuwepo online service bado unawakuta wateja wamejazana. Sina uhakika kati ya wateja wanaotumia online service na wale wanaokata ticket zao kwenye ofisi, ni ipi idadi ambayo ni kubwa.

Unayefanya biashara, unatafuta faida na wateja wengi, hata kama una online service bado utalzimika uwatafute kwa njia nyingine yoyote ambayo itakupa wateja wengi zaidi.
Mkuu Mkinga naunga mkono hoja.
Ila pia kwa vile ni national flag carrier, it's high time Watanzania tuonyeshe uzalendo kwa shirika letu, tupande ndege zetu kwa faida ya kujenga nchi yetu tuache kuwafaidisha wageni.
Pasco
 
Mkuu Msambichaka, kwenye digital world, inawezekana kabisa kuuza tiketi online bila kuwatumia mawakala. Mawakala wanaozungumzwa hapa sio mawakala traveling agents, bali mawakala commissioned agents wana operate kama ofisi za
ATCL, badala ya kutumia mawakala, wanauza tickets on line. Fast Jet wana ofisi zao kule tuu mdege yao inakotua, na hawana wakala popote na mauzo yote ni online!, ila kwa mujibu wa sheria ya kimataifa ya shirika la kimataifa la wakala wa usafiri wa Anga, IATA, wakala yoyote aliyesajiliwa IATA kupitia mtandao wa Galileo, anaweza jyfanya booking yoyote ya ndege yoyote, hivyo abiria wa Tanzania yote watapata tiketi za ATCL popote kupitia traveling agents wengine, ila kule ATCL inatua, lazima wawe na agents for clearing.

Pasco
Nashukuru kwa kunielewesha. spot on.
 
Kaka mambo yamebadilika sana wewe fanya uchunguzi na uchunguzi huo ukusaidie kutambua nafasi yako katika kutatua changamoto ya uelewa na weledi wa mambo yaendavyo katika karne hii. Unaweza kata ticket ya ndege hata basi bila wakala kokote duniani. Chamsingi sisi tunaoweza una kwa jicho la tatu tuwasaidie ndugu zetu kujitambue tumuunge mkono Rais Magufuli ili twende mbele kwa speed na fahamu kuwa binafsi sipingani na wewe katika suala la kukosoa lakini unapokosoa njoo na altenative solution ya tatizo lililopo. Ahsante
Nilitegemea na wewe utakuja na njia mbadala lakini umekuja na maneno matupu yasemayo tusimkosoe Rais lakini hoja za mleta mada hujajibu
 
Mkuu Mkinga naunga mkono hoja.
Ila pia kwa vile ni national flag carrier, it's high time Watanzania tuonyeshe uzalendo kwa shirika letu, tupande ndege zetu kwa faida ya kujenga nchi yetu tuache kuwafaidisha wageni.
Pasco
Kweli kabisa. Tusaidie kulinyanyua shirika letu.
 
Noted!

Kikubwa hapa ATCL wahakikishe wanatumia mifumo ambayo inaruhusu na kuendana na mazingira tuliyonayo na henye tija kwa shirika ili kuongeza ufanisi. Online service yeyote inayotoa huduma inatumia mawakala hvyo hili bado haliepukiki au mh. Rais amemaanisha kama wale wanapatikana pale ferry wakikatisha tiketi za boti.
 
Pasco,
Usidanganye watu, hata ukiuza online bado unatumia agents. Hata mpesa au Tigo pesa au credit cards ni agents.

Ina maana atcl itengeneze utaratibu wake yenyewe wa kupokea malipo kitu ambacho haina uwezo.
Nyie watu mnaishi dunia gani na huyo rais wenu?
Food for thought.
 
mkuu sikuhizi systems zimebadirika! ulisafiri lini mala ya mwisho? I mean international freight? huwakilakitu kiko online na mawakala huwa makampuni mengi wanadiscourage! Ila ni hoja ukizingatia systems ya zamani hapo agents role yao ilikua kubwa

Kwa heshima zote kaka ungerudi shule kwanza ukajifunze hata spellings kabla hujaanza kubishana na watu waliokuzidi uwezo wa kufikiri kama sio elimu. ("International freight", "mala ya mwisho", "system zimebadirika"!)
 
ATCL kama yalivyo mashirika mengine ya umma, kila mara imekuwa ikizaliwa na kufa kutokana na muundo wake usiokuwa wa kibiashara. TANESCO isiyo na mshindani yeyote, TTCL ambayo awali haikuwa na mshindani, na mengine mengi yaliyokwishakufa na yaliyouzwa, mashirika yote hayo yalikufa kwa sababu yalianzishwa, kuendeshwa na kusimamiwa kiserikali/kisiasa.

Serikali haijawahi kuendesha biashara ikafanikiwa. Tatizo linaanzia kwenye muundo wa haya mashirika/makampuni. Wanasiasa/viongozi wa serikali ambao kimsingi si wafanyabiashara ndiyo waliotengeneza muundo wa uendeshaji na ndiyo wenye kauli ya mwisho. Vigezo vya wajumbe wa bodi na watendaji wakuu wanavyo wao. Na siku hizi PhD imekuwa ni kigezo kikubwa sana ingawa kiuhalisia, kwa Dunia nzima, ni nadra sana kuwaona wenye PhD wakiwa wafanyabiashara wazuri na waliofanikiwa.

Juzi wakati Mh. Rais akizindua ujio wa ndege mpya alisema ATCL imezaliwa upya, ina ndege mpya, bodi mpya na uongozi mpya, sikusikia kama ina muundo mpya wa uendeshaji na usimamizi. Bado inaonekana ATCL itandeshwa kwa mkono wa serikali.

RAIS - 'ATCL ISITUMIE MAWAKALA WA KUKATISHA TIKETI'

Hili tayari ni agizo ambalo naamini ni agizo lisilo sahihi. Tayari serikali imeanza toka hatua za mwanzo kuingilia uendeshaji wa ATCL. Rais anapoagiza ATCL isitumie mawakala wa kukatisha tiketi inamaanisha ATCL iwe na wafanyakazi waajiriwa kila mahali nchini. Gharama za maelekezo hayo itakuwa kama ifuatavyo:
  • ATCL italazimika kuwalipa wakatisha tiketi mishahara, matibabu, posho, michango kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii, usafiri, n.k. ATCL italazimika kulipia gharama hizo zote bila ya kujali mkatisha tiketi anakatisha tiketi ngapi au kama amepata wateja au hakupata kabisa
  • ATCL italazimika kulipia ofisi na kuweka miundombinu ya ukatishaji ticket nchi nzima. Ifahamike kuwa ukitaka kuwa na ufanisi unalazimika kuwa na ofisi za ukatishaji tiketi hata mahali ambapo ndege haitui, kwaajili ya kuhudumia abiria wanaotoka maeneo hayo wanaotarajia kutumia usafiri wa ATCL kutokea uwanja ulio karibu
  • ATCL italazimika kuwapa mafunzo wakatisha ticket watakaotapakaa nchi nzima
Wakati ATCL watakapokuwa wanahangaika na kuwa na wakatisha ticket wao na ofisi zao, washindani wao wataendelea kuwa na wafanyakazi wachache, wakiwa na mawakala wengi wanaolipwa kutokana na idadi ya ticket na thamani ya ticket walizokatisha. Hawalipii ofisi, hawalipii matibabu, hawalipii michango ya hifadhi ya jamii, hawalipii likizo ya mfanyakazi. Mawakala wao wanalipwa kutokana na wanachozalisha, wasipozalisha hawalipwi chochote.

ATCL wanaanza na quandary ya kwanza, wafuate maagizo ya mwenye mali au kanuni za biashara? Je, hii ni ya mwanzo na ya mwisho au zitaendelea kuja na nyingine? Kwa kuwa tatizo la msingi la uendeshaji biashara zilizo chini ya serikali halijatatuliwa, haitakuwa jambo la ajabu ATCL kufuata projectile ya mashirika/makampuni ya umma.
Mnamjaribu eeeehhhhh
 
mkuu sikuhizi systems zimebadirika! ulisafiri lini mala ya mwisho? I mean international freight? huwakilakitu kiko online na mawakala huwa makampuni mengi wanadiscourage! Ila ni hoja ukizingatia systems ya zamani hapo agents role yao ilikua kubwa

Ndugu Kasimba kwa taarifa tu, Mleta hoja ni mdau wa biashara kubwa tu na kwenda nje kwake sio deal (nisimsemee sana)...Mie naunga mkono kuwa serikali isiingilie kabisa biashara kama maagizo ya kutotumia agent, wengine tupo porini miaka sasa lakini tunakata ticket za Fastjet kwa mtandao, tunapata ticket kwa mtandao na siku ya safari ni kuripoti tu pale Mwanza airport na safari inakuwepo bila utata
 
Umeeleza vyema.

Hata suala la lini na aina gani ya ndege zinunuliwe hapo baadae wangeachiwa ATCL wenyewe sababu ndiyo wako field.
wenyewe wenye nini? tuliwaachia ndege kibao tu zote wameua, nazo hizi unataka waziue?
 
Kaka dunia imebadilika unaweza kata ticket ya ndege popote ulipo bila msaada wa mtu yeyote kilichopo nikuchukua nafasi zetu katika jamii kutoa elimu au kuwasaidia kupata elimu waendane na dunia ya sasa kuleta ukinzani katika kila jambo linalokuwa initiated na serikali haliwezi kukufanya ukawa na busara za kuongoza bali kutatua changamoto zilizoko katika jamii yako ndio ngazi itakayokupandisha daraja na kuwa kiongozi. Je unamkumbuka Marehemu Deo Filikunjombe vaa viatu vyake vikikutosha basi hayo mambo mengine hayatakusumbua. Hongera Magufuli kwa kuonyesha tofauti hata sisi tusio wanachama wa ccm tunaona mwanga kupitia wewe.
..ATCL wame-advance kitekenolojia kuliko Emirates, BA, KQ, KLM, Ethiopian Airlines etc? Hawa wanatumia travel agents+ofisi zao pamoja na kuwa mara 1,000 ahead of us. Huyu katoa mchanganuo wake wa kiutendaji ni vipi si sahihi kuoiga marufuku travel agents wasiuze tiketi za ATCL na kama wewe una mchanganuo ulete hapa tuulinganishe.
 
Kaka dunia imebadilika unaweza kata ticket ya ndege popote ulipo bila msaada wa mtu yeyote kilichopo nikuchukua nafasi zetu katika jamii kutoa elimu au kuwasaidia kupata elimu waendane na dunia ya sasa kuleta ukinzani katika kila jambo linalokuwa initiated na serikali haliwezi kukufanya ukawa na busara za kuongoza bali kutatua changamoto zilizoko katika jamii yako ndio ngazi itakayokupandisha daraja na kuwa kiongozi. Je unamkumbuka Marehemu Deo Filikunjombe vaa viatu vyake vikikutosha basi hayo mambo mengine hayatakusumbua. Hongera Magufuli kwa kuonyesha tofauti hata sisi tusio wanachama wa ccm tunaona mwanga kupitia wewe.
Wewe ni ukoo ule wa kusifu na kuabudu, eti?

Mbona Msambichaka amepita humo humo unakozusha wewe? Kuna namna gani ya kukata tiketi popote ulipo bila wakala? Kama ulitaka kufikiri umezindua tiGO, Airtel na Western Union, basi hao ndio hasa MAWAKALA wanaofahamika.

Msambichaka haleti ukinzani, analeta smoothness kwa wazo mujarab. Shida ya ukoo wa kusifu na kuabudu ni kudhani kila kilichowazwa nje ya fikra za mwenyekiti wa chama ni dhambi na upinzani. Ukiwa na low mind, siku zote utaongozwa na woga dhidi ya mawazo mbadala. Mawazo haya ni resource sio rivalry. Ni wapi alisema anataka kupanda ngazi na kuwa kiongozi? Hii ndio mentality inayotukwamisha, kudhani kila anayesema kinyume chako, anataka kukalia kiti chako.

Nimalizie kwa kukukumbusha kuwa: ni kazi ngumu na nzito kuhamasisha soko la sanda kwa watu wasio na msiba. Huna haja ya kuikana CCM ikiwa una mawazo ya namna yako. Huo mwanga ulioupata kwa Magufuli kabla hujautumia, ulinganishe na wa Msambichaka. Usiyakimbie maoni, yatafakari ukiwa neutral ndio utapata jibu sahihi
 
Back
Top Bottom