ATCL Cabin ... Uniforms Cost USD49,000 ( PHOTO)

ATCL Cabin ... Uniforms Cost USD49,000 ( PHOTO)

Kimbunga huyu jamaa kafanya sana ufisadi ATCL halafu dada zetu wafanyakazi wa kwenye ndege wanamjua vizuri sana.

Mkuu ritz kumbe na huko kwa mair hostess pia huyo mkuu yupo? Nadhani amekaa pale chini ya mwaka lakini ufisadi wa miaka kumi! Angekaa miaka 2 ingekuwaje? Yaani pamoja na aliowarithi kuburuzwa mahakamani yeye hakuogopa hata kidogo!
 
Last edited by a moderator:
Huyo bwana anaetetea doller 50,000. Embu tumsaidie kwanza kimahesabu
50,000 *1600 =80,000,000 (Wasiojua ni Million themanini)
Waliokaa huko siku 45 wawili @250 USD
250USD*45*2=USD22,500. USD hizi ni sawa na 22,500*1600=36,000,00o yaani Million thelathini na sita. Divide by 2 unapata kila mmoja aliondoka na million 18,000. OK

Million 80,000-36,000=44,000,000.
Katika watu wawili walipata discount ya USD478 kila mmoja.
So USD478 *2=USD956. Approximately USD1000 sawa na Tsh1,600,000.

Milioni 44- Milliono1.6 = Millioni42.4. Tufanye Million 42.

Sasa basi na akili yako wewe unaetetea hili!
Chukua Tsh42,000,000/17=Tsh2,470,588 each uniform.

Ok toa Tsh470,000 kwa kila mtu peleka kwa dalali alietoa hilo dili usiulize wapi.

So, Tsh470,000*17=Tsh7,990,000. Hizi za udalali.

Sasa nchi gani inatengeneza nguo kwa million Tsh2? Ukiacha kwenu sumbawanga?

Ahasante kwa kukokotoa hayo mahesabu, maana watu wengine mpaka uwawekee kinywani. Hata common sense ina-dictate extravagant use of public funds
Pdidy na CHUAKACHARA


Kwenye fani ya Uhasibu kuna kitu kinaitwa 'Historical Cost Concept' ambayo ina state kwamba 'Thet cost of an Asset should be reported at its cost (Cost or cash equivalent amount) at the time of exchange transaction and should include all cost necessary to get the asset in place and ready for use'. Kwa kiswahili rahisi Maana yake nini? Maana yake ni kwamba jumla ya gharama ya kitu chochote ni pesa uliyotumia kununulia hicho kitu jumlisha gharama zote muhimu ambazo utazitumia kwa ajili ya kukipata hicho kitu ili kiwe tayari kwa matumizi.

Kwa hiyo katika kesi hii, gharama zote za Per-Diem, Air ticket, Commission ya dalali nk zinaform part ya gharama ya Uniform. Mfano rahisi ni wewe unapoagiza gari kutoka nje ya nchi. Hadi gari linakufikia wewe mtumiaji Jumla ya gharama ya gari ni pamoja na Gharama ya kununulia kutoka kwa manufacturer + Gharama za Kusafirisha + Ushuru + Commission ya Clearing Company + Gharama ya kulibeba na Folk lift hadi nyumbani (Au gharama ya mafuta utakapolijaza kwa mara ya kwanza kwa ajili ya kulitoa bandarini hadi nyumbani).

Huo ndio ukweli kama uamini muulize Muhasibu yoyote atakwambia hivyo.

TUMBIRI (PhD, Hull University - UK),
tumbiri@jamiiforums.com
 
Hiyo haitoshi, walipelekwa maofisa wawili eti kuzisimamia zishonwe. wacha Chisi afukuzwe, jizi kubwa

yaani sawa kabisa kwanza bei hiyo mbona nafuu...yaani ilibidi iwe mara mbili zaidi
 
attachment.php

Wanajamvi, ndiyo Uniform zenyewe hizi, ndiyo hapo utakaposhindwa kushangaa na kuanza kujiuliza hivi ni lini tutaamua kuacha kujiaibisha wenyewe kwa mambo yaliyo wazi kama hili.


huyu wa sita toka kushoto mbona mbibi...hayafika kweli muda wa kustaafu huyo?khaaa
 
Bw Chizi alikodisha ndege ya bilioni 80 kwa zaidi ya bilioni 270, ameshonesha unifom kwa bilioni zaidi ya 78. Halafu kuna watu wanamtetea aendelee kuwepo ATCL

ninamchukia mtu anayeiba mali ya umma, ninamchukia zaidi mtu anayekurupuka na kupost bila taarifa sahihi, bilioni 78 ni sawa na milioni elfu sabini na nane (78,000,000,000) just in case unahitaji kusaidiwa
 
Bw Chizi alikodisha ndege ya bilioni 80 kwa zaidi ya bilioni 270, ameshonesha unifom kwa bilioni zaidi ya 78. Halafu kuna watu wanamtetea aendelee kuwepo ATCL

Mkuu rudia tena yaani uniform zaidi ya billion 78 au millioni 78! Hata kama ni millioni 78 si haki hata kidogo. Anatakiwa apate haki yake tena achapwe viboko 12 wakati anaitwa kuhojiwa na 12 wakati anatoka kwenda kwake akamuonyeshe mkewe. Mali zake zitafutwe zikamatwe ziwe za ATCL.
 
Acheni porojo huna ushahidi huna haki ya kuongea. Waziri amesema kuwa uteuzi wake haukuzingatia kanuni za utumishi na si ufisadi wala wizi. Halafu kama ulikuwa na taarifa hizo mbona hukuziandika tangu awali.
 
hata ukimuita mwanao shida ,masumbuko ,tabu , kifo lazima tabia na maisha yaendane naye
 
Mie nadhani hizi ni uniform za precision walivyokuwa wanaanza, kwa hakika sio za air tanzania.
 
huyu wa sita toka kushoto mbona mbibi...hayafika kweli muda wa kustaafu huyo?khaaa
Wote hao wanatakiwa wawe kwenye admnistrative post, kazi ambazo si za kukutana na wateja kila wakati! Wawaachie vijana zaidi lakini kwa vile mambo kujuana, basi shida tupu!!
 
Tatizo lipo kwa alomteua. Kwani Chizi alijipeleka mwenyewe pale ATCL?
Huu ni mradi wa watu kufisadi kupitia migongo ya watu. Aibu kubwa hii, wakurugenzi kukaa china siku 45 wakisubiri nguo zishonwe! Only in Tanzania.
 
Back
Top Bottom