Wanajamvi, ndiyo Uniform zenyewe hizi, ndiyo hapo utakaposhindwa kushangaa na kuanza kujiuliza hivi ni lini tutaamua kuacha kujiaibisha wenyewe kwa mambo yaliyo wazi kama hili.
wamependeza lakini
ila hivi jamani jezi kama hizi mafundi wetu hawawezi kutengeneza? jamani mbona aibu hii,pale VETA wanatengeneza hizi jezi tena kwa bei rahisi zaidi,jamani watendaji tumsaidie raisi,hivi hata hili tunataka raisi aje asimamie utengenezaji wa jezi,mnapeleka china kwa bei kubwa tena kwa pesa ya walipa kodi
nilitaka kushangaa maana hizi nguo za batiki kuna mafundi wazuri tu hata hapa kwetu wanashona tena zaidi ya hizi.
Wanajamvi, ndiyo Uniform zenyewe hizi, ndiyo hapo utakaposhindwa kushangaa na kuanza kujiuliza hivi ni lini tutaamua kuacha kujiaibisha wenyewe kwa mambo yaliyo wazi kama hili.
Wangetafuta basi angalau wadada wazuri wazuri zikawapendeza...
mwakyembe anapayuka ili kujustify usanii wa kumuweka binamu yake. Mpaka cag atakapokagua hapo na kuthibitisha hayo matumizi ndo nitaamini. Amejumlisha gharama za safari na malazi ya hao maafisa kwenye uniform bila ya kueleza cost per unit uniform ni shs ngapi. Sasa mitanzania mijinga ikishaona tu inakurupuka na kusema huu ni ufisadi. Haiingii akilini maafisa wa shirika waende kushona nguo uchina halafu wakae huko huko kuzisubiria. Tupate taarifa kutoka upande wa pili ndio tufanye judgement. We hujiulizi kwa nini mwakyembe alikuwa anaongea kwa jazba na kutokwa na mapovu?? Anataka kuficha kukurupuka kwake.
Nimeamini Dr Mwakyembe ni member humu jamvini, tena atakuwa ...expert! Mi namuomba radhiii kubwa!! Anisamehe!!Mliomtukana Mwakyembe jana muombe radhi sasa