mkomatembo
JF-Expert Member
- Dec 17, 2011
- 1,477
- 816
Jamani hii nchi imeoza, inahitaji ukombozi wa nguvu - inahitaji serikali ambayo itakuwa ikisikia Challenger amefisaji haraka sana wanakuja nyumbani kwangu na kuchukua kile kinachowezekana ambacho kitaringana na dhamani ya ufisaji halafu kwenda gerezaji ili kwenda kujifunza uzalendo na uzawa.
Huu mtiririko wa wizi ukianzia juu ni vigumu sana kuu-control kuliko ukianzia chini. Mfano iwapo mtoto akichemka ni rahisi sana kumuonya na kumhadabisha iwapo wewe baba ni muadilifu - ndipo nina maana wizi ukianzia chini ni rahisi kuu-control. Aidha ikiwa baba nimekubuhu kufanya madudu mtoto akifanya yale yale sitapata nguvu ya kumuonya na kumuadabisha.
Hii ndiyo hali halisi madudu, wizi, ufisadi umeanzia toka pale Magogoni - "White House", je unategemea rais atamwambia nini waziri, waziri atamwambia nini Katibu, makatibu na mwaziri watawaambia nini wakurugenzi, hivyo hivyo hadi chini iwapo wooote hawa ni wezi.
Nchi hii ina kundi kubwa la viongozi ambao hawana uchungu na nchi hii!!
Ingekuwa ni kweli maneno yako, leo tusingeshuhudia hayo tunayoyajadili, mpeni sifa zake Rais jamani kama anafanya kazi nzuri, kutwa kumkandia tu hata anapojaribu kujitutumua kuonesha ukali? hebu kueni waungwana kwanza !