Mpita Njia
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 6,997
- 1,163
sasa kama hali ndio hii, Mataka na Nyang'anyi wanangoja nini hapo?
Wana ndugu mkuu ashany.mi nipo huku ulipo wewe nje ya dar natumaini napata data muhimu kuliko unazokuja kuwambia watu uongo....habari zenye uhakika ile kampuni ya madalali ijulikanayo kama YONO AUCT.MART kwaniaba ya STANBICBANK wameanza kukamata magari (VX)LANDCRUISER SABA walizotoa kama dhamana na kuchukua kiasi fulani cha pesa kwa ajili ya kutolea magari mengine na nyingine kutumika kwenye mafuta ili hali hakuna gari zilizotuolewa baada ya hapo.....chanzo chetu cha habari kimesema baada ya kufika pale walitafuta mwenyeji ambapo wengi ama wahusika walijitahidi kujificha kukimbia maswali na majibu.....na ndipo kazi ilipoanza.....
wenye habari zaidi msisite kutuleteta ...jf aifungamani na upande wowote wala kula rushwa
maloovee!!!
Huu ni ujinga wa serikali ya Tanzania, Boeng wanauza ndege kwa mkopo, kwa nini serikali haikopi ndege mpya za kisasa. All airlines in the world wananunua ndege kwa kulipa kidogo kidogo nyie mmeamua kukodi MITUMBA ili Richmonduli and Family wapate kitu kidogo. mikataba feki kama hii itaendelea hadi pale bunge la Tanzania litakapopitisha sheria ya kuweka limit za mikataba bila kupitiwa na kamati za Bunge. Richmonduli ataendelea kutesa tu, inabidi baba wa taifa afufuke kwani aliwaonya.
Asiyesikia la mkuu huvunjika guu.
Mkandara,
Mahesabu nliyoweka ni as far as leasing is concerned, hawa jamaa wamelease hizi ndege kwa miaka miwili. Na nnavyofahamu ni some sort of quick measure baada ndege yao ya mwisho kuwa grounded for technical reasons, ilhali kuna watu wameshalipia tiketi zao hawajaweza kuzitumia.
At $50K per month, a 2 years lease fee comes to $1.2M
Buying a new Boeing B737 will cost you over $40M (Ref: http://www.boeing.com/commercial/prices/). But of course, ikiwa ni ndege yako utaitumia kwa miaka mingi, sio miwili tu.
Point ya hivyo vimahesabu ni kuonyesha kuwa: IF... a big IF, hizo ndege ziko katika hali nzuri na hatukupewa kwa ajili tu ya kuclear junk yard ya hao jamaa, na hakuna some wierd clauses katika leasing agreement .... basi hili ni dili zuri mno!
Normal leasing fees ni far more expensive than the $50K/month.
By the way, Mfano wako kukodisha gari kwa dola 75 kwa siku na kuconclude kuwa eti ni rahisi mno kiasi tusingenunua magari, nauona sio sahihi. $75 per day comes to more than $80K for 3 years alone, whereas you can get a nice new car for that amount, lasting you 5 to 10 years in very good condition. Au hata kama huna lumpsum, ukilipia monthly installments, utalipa less that 25% per month compared to bei hiyo ya $75 per day.
Duuuuhhhhhhhalafu angalia hapa
if the hiring is as above then another richmond saga on the making a cool 40,000 usd a month on some peoples pockets.
Ndivyo nchi inavyoliwa na wenye meno makali
Usishangae habari ya mwaka 2007 hiiDuuuuhhhhhh
Kuweka kumbukumbu sahihiIle ndege "mpya" iliyokodiwa na ATC kutoka kampuni ya Wallis Trading ya Liberia aina ya Airbus 320 bado haijaanza safari zake, na kwa karibu miezi saba sasa imeishaligharibu shirika hilo zaidi ya shilingi Bilioni 2 za malipo ya kukodi na matengenezo mbalimbali ya kuifanya ndege hiyo ipendeze.
Habari za kuaminika toka ndani ya shirika hilo kongwe la ndege nchini zinasema kuwa hadi hivi sasa ndege hiyo ambayo ilipokewa kwa mbwembwe wiki chache zilizopita bado haijaanza safari zake na hata itakapoanza itaanza kwa deni kubwa ambalo itachukua muda mrefu sana kuweza kuona faida. Kwa mwezi huu tu unaoisha shirika hilo litalipa karibu shilingi milioni 700 kama malipo mbalimbali yanayohusiana na ndege hiyo.
Baadhi ya wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya ATCL wameanza kuonesha wasiwasi endapo habari za jinsi ndege hii inavyoshughulikiwa zitajulikana na vyombo vya habari. Hata hivyo hofu hizo zimechelewa kwani hadi hivi sasa inajulikana wazi kuwa mkataba mzima na jinsi ndege hii ilivyopatikana, kuingizwa na kusimamiwa na uongozi wa juu wa ATCL ni aibu kubwa kwa taifa.
Licha ya mkataba huo wa Wallis ambao unakodisha ndege hiyo kwa karibu dola milioni 30, shirika la ATCL liliingia mikataba mingine na kampuni ya Aeroman ya El Salvador ambayo ilipewa jukumu la kuitengeneza ndege hiyo ambayo ilikuwa na mapungufu mengi ambayo unaweza kuyaona kwenye eneo la "Pics and Documents" hapo juu. Mkataba huo ambao na wenyewe si chini ya shilingi milioni 400 nao unaliongezea deni shirika hilo.
Pamoja na kampuni ya Aeroman, ATCL imeingia mkataba mwingine na shirika la ndege la Mauritius ili kuwapatia mafunzo na mafundi wa kuisimamia ndege hiyo. Kinachoshangaza watu wengi ambao wamekuwa wakifuatilia suala hili ni jinsi gani shirika ambalo halina wataalamu na marubani wenye uzoefu wa kurusha ndege aina ya Airbus ambayo ni mojawapo ya ndege za kisasa na zinazotumika zaidi duniani hasa kutokana na kutumia kiasi kidogo cha mafuta kulinganisha na Boeing iliweza kuingia mkataba wa kuipata ndege hiyo bila kuandaa raslimali watu.
Habari mpya zinasema kuwa baada ya taarifa za ndege hii kucheleweshwa kuruka kutoka mapema leo kuna dalili kuwa safari za ndege hiyo zinaweza kuanza saa yoyote kuanzia sasa na si mwezi mmoja baadaye kama ilivyokuwa inatarajiwa.
KLH News inatoa wito wa serikali kufuatia ukodishaji wa ndege hiyo na kuangalia mapungufu yote yaliyotokea kabla (Mungu aepushie mbali) jambo baya halijatokea na ndipo watu wajifanye wanajali na wanataka kufuatilia.
Kabla ya kukodishwa na ATCL ndege hiyo ilikuwa inamilikiwa na shirika la ndege la Jamaica ambao walipoiachia ilikuwa na kila aina ya ubovu wa ndani ambao haulingani na umri wake. Hata hivyo haijulikani ni kwanini ilipoingia nchini ndege hiyo ilisemwa kuwa imekodishwa toka kampuni ya Wallis Trading ya Ufaransa wakati mkataba uliosainiwa ambao KLH imeuona unaonesha wazi kuwa kampuni hiyo ni ya Liberia (hata kama kampuni yake mama ni ya Ufaransa).