ATCL: Another Richmond!

ATCL: Another Richmond!

Huko tuendako...haya!

Mimi kama wewe Kitila .Nimepatwa na kichaa baada ya kuona wananchi wanakimbilia JF kusema yanayo wakuta.Naamini kwamba wanao husika wamesha pata ujumbe .

Naomba waleta habari wapunguze jazba na wanaweza kuleta ujumbe wao kwa utulivu ukawa na uzito mkubwa sana badala ya kutumia maneno mazito ya kushusha uzito wa ujumbe wao.
 
Kwani William Hajji vipi maana sisi wengine tunaona majina tu.. !

Huyu bado ni kijana mdogo. Nadhani hata miaka 40 hajafikisha huyu kijana. Na nilitegemea awe mstari wa mbele kukemea ufisadi, kumbe yeye ndio wa kwanza kuufakamia.
 
Jamani ee si ndio tunatengenezewa mabilionea 100 au hamtaki?


miye sitaki bwana; ukiwa na mabilionea 100 halafu ukawachukua tena na kuwagawia mabilioni mengine katika jitihada za kutengeneza mabilionea 100, ukishamaliza utakuwa na mabilionea wangapi wapya?
 
miye sitaki bwana; ukiwa na mabilionea 100 halafu ukawachukua tena na kuwagawia mabilioni mengine katika jitihada za kutengeneza mabilionea 100, ukishamaliza utakuwa na mabilionea wangapi wapya?

Hii hesabu ngumu sana itabidi wataalamu wa hesabu kina Mtanzania watusaidie kidogo hapa. Inavyoonekana Kikwete ameamua kubaki na mabilionea mia moja wale wale aliokuwa nao Mkapa!
 
Cha msingi ni kuhakikisha kuwa wale mabilionea tulionao tunawaimarisha zaidi katika ubilionea halafu hao sasa ndio watasaidia kuongeza idadi ya mabilionea, first things first, mpo hapo?!
 
Cha msingi ni kuhakikisha kuwa wale mabilionea tulionao tunawaimarisha zaidi katika ubilionea halafu hao sasa ndio watasaidia kuongeza idadi ya mabilionea, first things first, mpo hapo?!


Sasa hawa mabilionea ambao watakuwa wanaongezwa na hawa mabilionea wa awali watakuwa ni ndugu zao (wake, watoto, shangazi, wajomba, binamu, vitukuu na vilembwe, na vining'ina) au watakuwa ni watu baki tu?
 
Jamani ee si ndio tunatengenezewa mabilionea 100 au hamtaki?

..hao mia moja watakapochomewa nyumba na magari yao,na wakanusurika kukatwa mapanga,tutaomba mungu tungejua tungeongeza masikini elfu moja badala.
 
Hii hesabu ngumu sana itabidi wataalamu wa hesabu kina Mtanzania watusaidie kidogo hapa. Inavyoonekana Kikwete ameamua kubaki na mabilionea mia moja wale wale aliokuwa nao Mkapa!

Mwafrika wa Kike,

Tuache utani, mimi nimejaribu wee ili angalau niwe katika hao mabilionea
wa kutengenezwa kihalali na JK lakini sijaambulia kitu.

Hao mabilionea ni geresha tu. Sisi ambao tumejaribu na tumebaki pale pale tulipokuwa wakati mheshimiwa anaingia madarakani. Labda kilichoongezeka ni uchovu tu baada ya kupita pale ikulu zaidi ya mara 100 bila kuambiwa japo jambo linalotia matumaini.

Suala la mabilionea sahau, labda kama ni mafisadi. Lakini wale vijana wanaotaka kutumia elimu zao kutengeneza pesa kihalali, hilo la JK sahau.

Hata yule mheshimiwa wa Kasungura naye hivyo hivyo. Siku naamua kuandika kitabu, kuna mengi kweli kweli kuhusu hawa waheshimiwa.

Bila kumwaga sana mtama hapa, kuna siku nitakuandikia (PM) zaidi. Tuna wasanii hasa, ila tatizo la TZ ni kwamba hata ukiangalia walio nje ya system na wenyewe ndio wababaishaji ile mbaya tukiwemo sisi hapa JF. Wengine tunabaki kuomba tu labda watawala wetu wafike mahali na kusema sasa basi, tumewanyanyasa mno hawa watu na wacha tufanye kweli.
 
Cha msingi ni kuhakikisha kuwa wale mabilionea tulionao tunawaimarisha zaidi katika ubilionea halafu hao sasa ndio watasaidia kuongeza idadi ya mabilionea, first things first, mpo hapo?!

Wengi wa mabilionea tulio nao, hawazalishi kitu. Sasa hiyo kuwakomboa wengine itatoka wapi? Wao ni mission town.

Wewe angalia kama Manji, hivi anazalisha nini?

Afadhali mno akina Mengi au hata Barehsa.

Hivi hapa JF kuna wafanyakazi wa TIB? Hiyo bank ndio ilitakiwa isaidie kutengeneza mabilionea lakini si ajabu hata wenyewe hawajui mabilionea wanatengenezwaje.
 
Mnahangaika kutengeneza mabillionea hamuoni Jongwe (Mugabe) alivyotengeneza wa kwake Zimbabwe?

1.jpg
 
Mnahangaika kutengeneza mabillionea hamuoni Jongwe (Mugabe) alivyotengeneza wa kwake Zimbabwe?

1.jpg



duh.. nusura nimuonee wivu huyo mtoto kumbe ningemkwapulia ningekuwa bilionea na mimi.. duh..
 
Ole... si mpaka nikubali? lakini nadhani tukikubali watafurahi sana. Unaweza kuiweka hii kwenye "Sticky" hapo juu.. iunngane na ndugu zake..
 
Hiyo bank ndio ilitakiwa isaidie kutengeneza mabilionea lakini si ajabu hata wenyewe hawajui mabilionea wanatengenezwaje.

..ilitakiwa isaidie kuwapa mitaja wachapakazi wa tanzania. badala yake mitaji wanapata wachapiakazi kupitia bot. unategemea nini?

..hii nchi hamna anayetaka kulima,kila mmoja anataka ugali tu. unafikiri ingekuwa otherwise watu wangeenda chota pesa za wenzao pale mirambo? wangetafuta zao!
 
Jibu swali wacha uppuzi wako. Kilichokukera nini hapo? huna adabu nini wewe.

Jibu la swali liko ndani ya CD.Kilichonikera ni hiyo useless criticism yako.Siwezi kuwa na adabu kwa mtu anayeonyesha dalili ya kuwa kibaraka wa mafisadi.Satisfied?
 
Ahsante wandugu Idimi, Mtanzania, na wengine wote na hasa ndugu Enigma, finally muziki Kamanyola na Mbuya Makonga Adios, muda tu kidogo ili tulichambue hili Chekeencha! Duh!

I love JF!
 
Back
Top Bottom