Sukununu
Member
- Feb 23, 2008
- 23
- 5
Ujumbe kwa waliotuma hii CD
"Tumefikia kutoa CD hii ili kuchangia katika utawala wa uwazi na ukweli. ATC inapojaribu kujirejesha kwenye mafanikio haina budi kufanya hivyo kwa uwazi na ikiweka maslahi ya Taifa mbele. Ndege yetu mpya tuliyokodi toka kampuni ya Wallis Trading ya Liberia inatarajiwa kuwasili nchini siku yeyote ndani ya wiki hii au siku chache zijazo endapo mambo ya logistics na permissions za kutua sehemu mbalimbali zitakamilika katika hiyo Ferry Flight.
Kwa hakika ni ndege ambayo inapendeza na itageuza shingo za watu pindi itakapopaa kwenye anga letu. Na kwa vile tayari tumepokea ndege mbili za Dash 8 siku chache zilizopita basi ni wakati muafaka kwa Watanzania kuiona mikataba inayohusiana na ndege hizo zote.
Tafadhali fungua kwanza File le PDF la "Introduction" ambalo litakupa utangulizi wa nyaraka nyingine. Baadhi ya Nyaraka zimefanyiwa marekebisho ya mwisho ambayo hayajaweza kupatikana na hivyo kuwapa wasomaji idea tu; pale ambapo marekebisho yamejulikana basi tumeyaambatanisha.
La msingi ni kutambua kuwa hadi hivi sasa tumeshaanza kuilipia ndege hiyo zaidi ya dola 400,000 kwa mwezi pamoja na faini ya kuchelewa kupata udhamini ya dola elfu sitini kwa kila mwezi ambapo udhamini huo haujapatikana. Tunatumaini Watanzania wataelewa zaidi kuhusu shirika lao hilo jipya.
Na mwisho tumeweka habari hii hadharani kama ishara ya kupinga ufukuzwaji kazi wa watumishi wenzetu watano siku chache zilizopita hasa baada ya wao kuonekana wanahoji hoji sana utendaji kazi wa baadhi ya viongozi wakuu wa shirika hili."
Enigma
Mshikaji, CD ina mikwaruzo