Swali lako ni la msingi sana, sana na jibu lake siyo rahisi kama unavyotaka tutaje majina. Kwa sababu tatizo lililopo siyo watu ila ni mfumo wa uendeshaji wa mambo yetu. Tujadili mfumo wa uendeshaji mambo yetu kwanza tukishakubaliana tuwaweke watu wa kutuendeshea mambo yetu. Binaadamu wote ni dhifu kama watoto wadogo wanavozaliwa ni lazima tuweke chech and balances za kweli!!!!
Nakubaliana na wewe, tatizo ni mfumo. Kwa mfano, bodi ya ATCL ingekuwa na watu makini, wasikubali kuyumbishwa, kurubuniwa, kudanganywa wangeweza kutambua udhaifu wa menejimenti ya ya ATCL na kutumia uwezo wao wa kisheria kuzui, kufichua na kuadhibu mafisadi.
Ninavyodhani, wajumbe wa bodi siyo waajiriwa. Kama bodi inafanya kazi nchini ya kiwango iondolewe. tatizo ni nani wa kuwaondoa? Rais hafanyi maamuzi bila tume, nani wa kushinikiza ili iundwe tume? .... unakuta ktk mlolongo wa matukio ili kumwajibisha FISADI ni mrefu mno.
Uwajibikaji mzuri wa bodi, utamfanya Mtendaji mkuu kutimiza majukumu yake vizuri kwa kujiongezea sifa nzuri ya utendaji mzuri, pia kuogopa kuwajibishwa. Mtendaji mkuu anapokuwa smart lazima watendaji wa chini watakuwa wawajibikaji kwani wanajua boss hana mchezo.
Mfumo huu, unapokuwa umelega, lazima mabo yaharibike kwani MAFISADI wanakuwa na uwezo wa kupenyeza hoja/mipango/mikakati/mapendekezo nk vyenye mlengo wa kujinufaisha.
Kwa haya yanayotokea sasa ATCL, RICHMOND, KIWIRA, IPTL, BOT nk yanatuonyesha kwamba mfumo wa uwajibikaji ulisha vurungwa sana na hakukuwa na mtu/watu wenye kupaza sauti ya kilio kwamba hapo kuna FISADI.
Washauri wa Rais wanaosoma maongezi ya wanaJF wamshauri Rais afanye mapinduzi ya kweli, vinginevyo ataonekana hafai, kwa kukosa kufanya jambo linalotakiwa ktk kipindi muafaka.