GE2025 Atawatawala kwa Risasi na Mamluki?

GE2025 Atawatawala kwa Risasi na Mamluki?

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
Wamemtangaza..watamuapisha
Watawalazimisha Watanzania kumpenda na kumuimbia tena...picha zake zitajazwa kila kona
Atakapoapishwa atapangua jeshi la polisi na kuwalaumu wao...

Lakini hadi hivi sasa hawajaonesha hata kidogo kuelewa kilichotokea...kusikitika lakini kitendo cha kuleta mamluki kwenye nchi yetu ni dhambi kubwa sana...

Wao wamemtangaza kwa risasi
Mioyo imemkataa na kuasi.
Nchi itaendeshwa kwa mtutu wa bunduki,ila Samia hana akili sijui alifika kwenye hiyo ngazi ya umakamu wa raisi kwa njia zipi
 
..uwezo wa kushinda bila kumwaga damu alikuwa anao.

..lakini kwa ujinga wake akaamua kutafuta ushindi kwa njia zisizofaa.
JokaKuu.

Nakubaliana nawe Mkuu, CCM inaweza kabisa kushinda bila kutumia njia wanazotumia, wana kila kitu mikononi mwao, lakini njia wanazotumia ni kama wamepumbazwa katika uwezo wa kufikiri. Kwangu mimi hili ndilo linalonitisha mno!

CCM imegota kimawazo kabisa, na uchaguzi huu unaonyesha ili wazidi kubaki madarakani walichonacho ni nguvu ya dola tu, hivyo wanazidi kutengeneza tatizo juu ya tatizo, na huhitaji kuwa nabii, mbele ya Tanzania kuna kumwagika damu nyingi katika taifa letu! CCM wanaweza kuliepusha taifa hili katika hilo janga wakitulia na kutafakari kwa maslahi ya taifa, wala sio ya Chama chao!
 
Kwa vile ni YEYE huziweka tawala za mataifa, then ni YEYE ameruhusu huu ushetani utokee kwenye ardhi yetu na kumruhusu shetani atamalaki na ushetani kutamalaki, tumwachie YEYE MWENYEWE, Atatenda!.
P
Huu ujinga wa kuamini Mungu wengine tulishaukataa kitambo.

Nikikwambia uthibitishe Mungu yupo huwezi.

Huwezi.

Usitulishe huu ujinga in secular spaces nenda kahubiri kanisani huko.
 
Watch and see brother, wanaweza kutushinda wananchi sababu hatuna silaha..lakini amini nachokuambia , JWTZ kwa asilimia kubwa vikosi vingi vimekwisha muasi , ni suala la muda ,inaweza kua hata mwaka ,au zaidi ila atakutana na shughuli ambayo itamfanya ajutie Siku Mungu aliyomuumba!!..kama ameshindwa kuilinda major city dar es salaam, Hana ubavu wa kupambana na Tanganyika..hata Uganda nzima imsaidie!!
Futa kabisa akilini mwako kuhusu Jwtz hawa hawana msaada wowote.
Kama mamluki wameingia na wanatuua bado unatumaini na jeshi la namna hii?

Yaani adui anaingia kwenye mipaka ya nchi hadi ndani na kuanza kuua raia huku jwtz wana silaha kilakitu ajabu wanakodoa tu pale mwanza wameingiza hadi vifaru barabarani utadhani wapo serious kweli.

Hakuna la maana tena. Tegemea mama kupewa umalikia kabisa yaani atawale milele na badae Abdul awe mfalme wetu

Kuhusu jeshi futa hilo wazo. Wanachi walikuwa wanawaambia hapohapo site wanajsshi chukueni nchi chukueni nchi lakni wapo tu wanakodoa macho

Je kilichowafanya washindwe kuchukua nchi kipindi hiki ni kipi kitawafanya wachukue nchi hapo badae?
Useless jwtz
 
CCM iko ukingoni kuanguka walichokipanda watavuna hakika, chama kinategemea nguvu za dola ili kishinde,

Chama kinamwaga damu za watanzania bila huruma ,

Mbaya zaidi ni kutumia hawa mamluki hii ni kashfa kubwa sana kwa vyombo vya usalama.
 
..wote waliopotezwa familia zao zifutwe machozi.

..waliohusika na utekaji, na mauaji, wachukuliwe hatua za kisheria.

..hili jambo la utekaji na mauaji ya kisiasa halipaswi kufumbiwa macho, au kusukumwa chini ya zulia.
Sahihi, utekaji hauna afya kwa taifa, ufike mwisho. Ila sioni kama utakoma bila suluhisho la namna ya kuendesha siasa za nchi.
 
JokaKuu.

Nakubaliana nawe Mkuu, CCM inaweza kabisa kushinda bila kutumia njia wanazotumia, wana kila kitu mikononi mwao, lakini njia wanazotumia ni kama wamepumbazwa katika uwezo wa kufikiri. Kwangu mimi hili ndilo linalonitisha mno!

CCM imegota kimawazo kabisa, na uchaguzi huu unaonyesha ili wazidi kubaki madarakani walichonacho ni nguvu ya dola tu, hivyo wanazidi kutengeneza tatizo juu ya tatizo, na huhitaji kuwa nabii, mbele ya Tanzania kuna kumwagika damu nyingi katika taifa letu! CCM wanaweza kuliepusha taifa hili katika hilo janga wakitulia na kutafakari kwa maslahi ya taifa, wala sio ya Chama chao!
Kwa post hii na ile na comment inayo fanana na yako iliyotangulia
Si hawana uwezo kufikiri, maoni yangu hali hio unayo eleza ndani ya CCM imechangiwa na kutopatikana muafaka ndani yao wenyewe nani awe mgombea wa urais. Hivyo wameingia ktk uchaguzi si tu hawana umoja, bali wanasalatiana na kukwamishana. Mwisho wa siku yule mwenye nguvu/madaraka anajikuta anatumia vyombo kudhibiti damage inayo fanywa na wenzake au kuzuia wasifikie malengo yao.

Mpasuko ukiwa mkubwa zaidi, wananchi ndio watashinda kwasababu mabadiliko yatapatikana (japo kitanzi ni kuwa tume ikishatangaza ndio basi). Hofu yangu tu, wale walio saliti kwakuwa wameshindwa tayari kwa maana rais amepatikana huenda wakarudi tena na kutulia ndani ya CCM, hivyo hata haya tunayo ona kama mafanikio ya resistance kwasasa yanaweza fifia kwa haraka sana baada ya muda, hasa pale CCM watakapo weza kupata muafaka kati yao.
 
Yes the biggest change ni YEYE atafanya kitu!, kuna jambo litatokea kuwafuta machozi Watanzania.

Pili kukataliwa ni kubaya, hivyo Bi Dada will be just a figure head, ana move back na kumuacha VP, ndie will be running the show, and he is dam good, tatizo la VP ni moja tuu, ni mtu wa ule mtandao wa wale wahuni wa Polepole!.
P
Umeshajidhihirisha upo wapi. Na post zako za kinafiki.. Raisi Samia is here to stay for five years.. na ata run the show. Anza kupambana na halinp yako Bto
Wamemtangaza..watamuapisha
Watawalazimisha Watanzania kumpenda na kumuimbia tena...picha zake zitajazwa kila kona
Atakapoapishwa atapangua jeshi la polisi na kuwalaumu wao...

Lakini hadi hivi sasa hawajaonesha hata kidogo kuelewa kilichotokea...kusikitika lakini kitendo cha kuleta mamluki kwenye nchi yetu ni dhambi kubwa sana...

Wao wamemtangaza kwa risasi
Mioyo imemkataa na kuasi.
Unaumia kutoka wapi? Maumivunyakizi muone Daktari ..
 
Raisi Samia is here to stay for five years.. na ata run the show. Anza kupambana na halinp yako Bto
Kwani wewe ni Mungu?, kuna mtu alikuwa mbabe kama JPM?, yuko wapi?, kama tulipambana na hali zetu wakati wa Chuma, Magufuli na bado tupo, itakuwa huyu Dada yangu Samia?. Nipo napambana na nipo sana tuu!.
P
 
Kwa post hii na ile na comment inayo fanana na yako iliyotangulia
Si hawana uwezo kufikiri, maoni yangu hali hio unayo eleza ndani ya CCM imechangiwa na kutopatikana muafaka ndani yao wenyewe nani awe mgombea wa urais. Hivyo wameingia ktk uchaguzi si tu hawana umoja, bali wanasalatiana na kukwamishana. Mwisho wa siku yule mwenye nguvu/madaraka anajikuta anatumia vyombo kudhibiti damage inayo fanywa na wenzake au kuzuia wasifikie malengo yao.

Mpasuko ukiwa mkubwa zaidi, wananchi ndio watashinda kwasababu mabadiliko yatapatikana (japo kitanzi ni kuwa tume ikishatangaza ndio basi). Hofu yangu tu, wale walio saliti kwakuwa wameshindwa tayari kwa maana rais amepatikana huenda wakarudi tena na kutulia ndani ya CCM, hivyo hata haya tunayo ona kama mafanikio ya resistance kwasasa yanaweza fifia kwa haraka sana baada ya muda, hasa pale CCM watakapo weza kupata muafaka kati yao.

Kwa mtazamo wangu mpasuko ndani ya CCM naona ni mgumu sana ( sisemi hauwezi kutokea) Tatizo kubwa la nchi yetu, CCM inashikilia livelihood ya maisha ya Watanzania wengi katika nafasi za juu, serikalini na hata katika biashara, Kujitenga na CCM ni kujifungia kitanzi chako mwenyewe! au kuwa kinyume nayo tu, ndio unayamaliza maisha yako hata bila kukutoa roho! Katiba ya Tanzania ilitengenezwa hivyo kwa makusudi kabisa!

Watanzania wengi wenye nafasi au uwezo wa kufikiri ambao labda wengeweza kuja na njia mbadala wa kuongoza nchi hii, hawana ujasiri wa kuchukua kujitenga na CCM, huu ni mfumo ambao ulitengenezwa kuanzia TANU mpaka CCM umewaweka watanzania wengi wenye mitazamo tofauti rehani! Na CCM inalijua hilo na inalitumia kikamilifu, rejea hotuba nyingi za Kikwete utaona statements kama hizi "nawajua sana watanzania". Na yoyote tu atakaye kuja na mawazo tofauti atabebeshwa majina mengi "anatumiwa na mabeberu" " analetea udini" " anavunja amani yetu" etc.

Kwangu naamini kabisa kuindoa CCM kwa njia ya kura kwa mfumo huu , ambayo umebebwa na kusimamiwa na watendaji wa serikali ambao uhai wao wa maisha kila siku unategemea CCM, ni kitu kisichowezekana kabisa, uchaguzi huu umeonyesha hivyo, lakini pia umetoa mwanga kuwa mwisho wa CCM utakuwa violent! Hii haikimbiliki kabisa! Naamini kabisa ni vigumu CCM kukaa na kujirekebisha! Na haina Uwezo huo! CCM wanajua wazi kuibadili Katiba kwa njia yoyote ni kujifungia kitanzi chao, na vilevile utafungulia mlango wa wazi wa kuuangalia Muungano upya, kwa CCM hiyo ni kama Imani ya dini! ambayo you cannot negotiate! Wanajua madhara yake!

Maandamano haya yameonyesha wazi ni njia ipi ya kuchukua kuibadili Nchi yetu! Ni njia mbayo CCM yenyewe wameilazamisha na ambayo kwa sehemu kubwa haina uwezo wa kui control!
 
Kwa mtazamo wangu mpasuko ndani ya CCM naona ni mgumu sana ( sisemi hauwezi kutokea) Tatizo kubwa la nchi yetu, CCM inashikilia livelihood ya maisha ya Watanzania wengi katika nafasi za juu, serikalini na hata katika biashara, Kujitenga na CCM ni kujifungia kitanzi chako mwenyewe! au kuwa kinyume nayo tu, ndio unayamaliza maisha yako hata bila kukutoa roho! Katiba ya Tanzania ilitengenezwa hivyo kwa makusudi kabisa!

Watanzania wengi wenye nafasi au uwezo wa kufikiri ambao labda wengeweza kuja na njia mbadala wa kuongoza nchi hii, hawana ujasiri wa kuchukua kujitenga na CCM, huu ni mfumo ambao ulitengenezwa kuanzia TANU mpaka CCM umewaweka watanzania wengi wenye mitazamo tofauti rehani! Na CCM inalijua hilo na inalitumia kikamilifu, rejea hotuba nyingi za Kikwete utaona statements kama hizi "nawajua sana watanzania". Na yoyote tu atakaye kuja na mawazo tofauti atabebeshwa majina mengi "anatumiwa na mabeberu" " analetea udini" " anavunja amani yetu" etc.

Kwangu naamini kabisa kuindoa CCM kwa njia ya kura kwa mfumo huu , ambayo umebebwa na kusimamiwa na watendaji wa serikali ambao uhai wao wa maisha kila siku unategemea CCM, ni kitu kisichowezekana kabisa, uchaguzi huu umeonyesha hivyo, lakini pia umetoa mwanga kuwa mwisho wa CCM utakuwa violent! Hii haikimbiliki kabisa! Naamini kabisa ni vigumu CCM kukaa na kujirekebisha! Na haina Uwezo huo! CCM wanajua wazi kuibadili Katiba kwa njia yoyote ni kujifungia kitanzi chao, na vilevile utafungulia mlango wa wazi wa kuuangalia Muungano upya, kwa CCM hiyo ni kama Imani ya dini! ambayo you cannot negotiate! Wanajua madhara yake!

Maandamano haya yameonyesha wazi ni njia ipi ya kuchukua kuibadili Nchi yetu! Ni njia mbayo CCM yenyewe wameilazamisha na ambayo kwa sehemu kubwa haina uwezo wa kui control!
Naunga mkono, isipokuwa paragraph ya mwisho niweke maneno kidogo.

Maandamano haya yana element nyingi sana ndani yake, naamini hata wao na vyombo vyao kuna kitu wamejifunza. Huko mbele hali itakuwaje, ni swali ambalo nadhani nitaweka akiba ya maneno kidogo kwasababu ni ukweli CCM wakipata tishio la msingi kabisa hufanya jitihada za kubadilika. Ngoja tuendelee tazama wanavyo changa karata zao upya.
 
Kwani wewe ni Mungu?, kuna mtu alikuwa mbabe kama JPM?, yuko wapi?, kama tulipambana na hali zetu wakati wa Chuma, Magufuli na bado tupo, itakuwa huyu Dada yangu Samia?. Nipo napambana na nipo sana tuu!.
P
Pasco umenikumbusha siku ulipo uliza lile swali pale ikulu lilo fanya tujue Mayalla maana yake ni njaa! Hivi siku ile uli lala katika hali gani?
 
Narudia tena kusema raia msumari viongozi nyundo
Nalog off Z
 
Back
Top Bottom