Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,501
- 51,093
Katika mkutano wa Chadema leo Kawe, Askofu Mwamakula na Sheikh Katimba leo wametoa dua nzito sana dhidi ya mtu yeyote atakayetenda dhulma kudhulumu haki za watanzania kwenye kupata viongozi wao halali wa nchi hii.
Askofu Mwamakula amesoma dua nzito ya kuomba Mungu ashushe Malaika wawashughulikie wote watakaojaribu kupora haki za watanzania kuchagua wawatakao. Ametoa mfano wa namna Malaika walipopambana na majeshi ya Ibilisi na kumnyang'anya funguo za kuzimu.
Sheikh Katimba akaomba Mungu amdhalilishe mtu yoyote atakayekula njama za za dhulma ya haki za wananchi, ameomba Mungu amdhalilishe hapahapa duniani na huko Mbinguni
Mimi nasema hawa viongozi wa kitaifa, viongozi wa CCM, VIongozi wa NEC na wote wanaokula njama za kuvuruga uchaguzi MWENYEZI MUNGU ANAONA, LAANA HAZITAWAACHA SALAMA IWAPO MTATEKELEZA UDHALIMU HUU!
Mwaka 2015 Mkuu wa nchi wakati anaapishwa pale uwanja wa Taifa kuwa rais, alisomewa dua na Askofu na Sheikh dua nzito huku akiapa kuwa mtenda haki na kutoonea wala kubagua. Sasa Dua za Mungu huwa haziendi bure, namshauri ajipime aone kama amekiishi hiki kiapo. Viapo mbele ya Mungu ni vizito!
Nimkumbushe tu Rais Magufuli kuwa siku anaapishwa pale Uwanja wa Taifa, Sheikh Mkuu alimsomea dua nzito sana akiambatanisha dua hiyo na aya Nzito kuliko zote kwenye Qu'ran aya ya Mamlaka ya Mungu (Ayatul' Kursiyyu). Hii ni Aya yenye Ulinzi mzito!, Waislamu huitumia aya hii kwenye kujilinda dhidi ya mamlaka za Ibilisi, uchawi, wenye nia mbaya n.k. Na kweli Mungu kamlinda Rais katika Mengi mpaka sasa. Lakini nimkumbushe tu mheshimiwa rais kuwa Qur'an huwa haichezewi chezewi, Mwisho wake siyo Mzuri. Ni bora atende haki la sivyo Mungu hadhihakiwi!, Adhabu yake ni kali!
Maamuzi ni yake atekeleze kiapo chake au akivunje!. Mungu anamuona!
Askofu Mwamakula amesoma dua nzito ya kuomba Mungu ashushe Malaika wawashughulikie wote watakaojaribu kupora haki za watanzania kuchagua wawatakao. Ametoa mfano wa namna Malaika walipopambana na majeshi ya Ibilisi na kumnyang'anya funguo za kuzimu.
Sheikh Katimba akaomba Mungu amdhalilishe mtu yoyote atakayekula njama za za dhulma ya haki za wananchi, ameomba Mungu amdhalilishe hapahapa duniani na huko Mbinguni
Mimi nasema hawa viongozi wa kitaifa, viongozi wa CCM, VIongozi wa NEC na wote wanaokula njama za kuvuruga uchaguzi MWENYEZI MUNGU ANAONA, LAANA HAZITAWAACHA SALAMA IWAPO MTATEKELEZA UDHALIMU HUU!
Mwaka 2015 Mkuu wa nchi wakati anaapishwa pale uwanja wa Taifa kuwa rais, alisomewa dua na Askofu na Sheikh dua nzito huku akiapa kuwa mtenda haki na kutoonea wala kubagua. Sasa Dua za Mungu huwa haziendi bure, namshauri ajipime aone kama amekiishi hiki kiapo. Viapo mbele ya Mungu ni vizito!
Nimkumbushe tu Rais Magufuli kuwa siku anaapishwa pale Uwanja wa Taifa, Sheikh Mkuu alimsomea dua nzito sana akiambatanisha dua hiyo na aya Nzito kuliko zote kwenye Qu'ran aya ya Mamlaka ya Mungu (Ayatul' Kursiyyu). Hii ni Aya yenye Ulinzi mzito!, Waislamu huitumia aya hii kwenye kujilinda dhidi ya mamlaka za Ibilisi, uchawi, wenye nia mbaya n.k. Na kweli Mungu kamlinda Rais katika Mengi mpaka sasa. Lakini nimkumbushe tu mheshimiwa rais kuwa Qur'an huwa haichezewi chezewi, Mwisho wake siyo Mzuri. Ni bora atende haki la sivyo Mungu hadhihakiwi!, Adhabu yake ni kali!
Maamuzi ni yake atekeleze kiapo chake au akivunje!. Mungu anamuona!