TANZIA Askofu Mkuu Novatus Rugambwa amefariki dunia

TANZIA Askofu Mkuu Novatus Rugambwa amefariki dunia

Heparin

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2021
Posts
442
Reaction score
3,219
1758101237498.png

1000446047.jpg
Aliyekuwa Balozi wa Baba Mtakatifu nchi mbalimbali duniani Mtanzania Askofu Mkuu Novatus Rugambwa amefariki dunia usiku wa Septemba 16, 2025 huko Roma nchini Italia.

Hayati Askofu Mkuu Novatus Rugambwa alizaliwa Oktoba 08, 1957 Mkoani Kagera nchini Tanzania, aliwekwa wakfu katika Daraja Takatifu ya Upadre Julai 06, 1986 na Mhashamu Nestorius Timanywa, aliyekuwa Askofu wa Jimbo Katoliki Bukoba, March 18, 2010 aliwekwa wakfu katika Daraja Takatifu ya Uaskofu na Askofu Mkuu Tarcisio Pietro Evasio Kardinal Bertone, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Vatican.

Amehudumu katika nchi mbalimbali kwa nafasi ya Balozi wa Baba Mtakatifu nchi hizo ni kama vile Angola, Honduras, Visiwa vya Fiji.

Chanzo: Radio Maria
 
Dah! Rest in peace Balozi wa Papa na pia Mtanzania Mwenzetu Askofu Mkuu Novatus Rugambwa. Hakika familia yenu ni ya kipekee kwenye Kanisa Takatifu Katoliki la Mitume.

Kuanzia Kardinali wa kwanza Afrika na Tanzania marehemu Laurent Rugambwa; Askofu Mkuu na Balozi wa Papa marehemu Mhashamu Novatus Rugambwa; na Kardinali Protas Rugambwa, ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Jimbo kuu la Tabora! Ni baraka ya aina gani hii!
Mazee yule Cardinal Rugambwa wa Tabora akiiona hii komenti yako atashangaa sana🤣🤣.
 
Dah! Rest in peace Balozi wa Papa na pia Mtanzania Mwenzetu Askofu Mkuu Novatus Rugambwa. Hakika familia yenu ni ya kipekee kwenye Kanisa Takatifu Katoliki la Mitume.

Kuanzia Kardinali wa kwanza Afrika na Tanzania marehemu Laurent Rugambwa; Askofu Mkuu na Balozi wa Papa marehemu Mhashamu Novatus Rugambwa; na Kardinali Protas Rugambwa, ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Jimbo kuu la Tabora! Ni baraka ya aina gani hii!
Mkuu, hakuna jina la ukoo kwenye hili kabila. Mtu anaweza kuwa ukoo wa Abasaizi, akaitwa Rugambwa na mwingine akawa ukoo wa Abashamura akaitwa Rugambwa na mwingine akawa ukoo wa Abalwani akaitwa jina hilohilo.

Ni coincidence tu imetokea jina la Rugambwa limetoa maaskofu watatu kwenye generations tatu tofauti. Naona mseminari umekumbuka asili yako.
 
Dah! Rest in peace Balozi wa Papa na pia Mtanzania Mwenzetu Askofu Mkuu Novatus Rugambwa. Hakika familia yenu ni ya kipekee kwenye Kanisa Takatifu Katoliki la Mitume.

Kuanzia Kardinali wa kwanza Afrika na Tanzania marehemu Laurent Rugambwa; Askofu Mkuu na Balozi wa Papa marehemu Mhashamu Novatus Rugambwa; na Kardinali Protas Rugambwa, ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Jimbo kuu la Tabora! Ni baraka ya aina gani hii!
Hawa ni familia moja?
 
Dah! Rest in peace Balozi wa Papa na pia Mtanzania Mwenzetu Askofu Mkuu Novatus Rugambwa. Hakika familia yenu ni ya kipekee kwenye Kanisa Takatifu Katoliki la Mitume.

Kuanzia Kardinali wa kwanza Afrika na Tanzania marehemu Laurent Rugambwa; Askofu Mkuu na Balozi wa Papa marehemu Mhashamu Novatus Rugambwa; na Kardinali Protas Rugambwa, ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Jimbo kuu la Tabora! Ni baraka ya aina gani hii!
Ni familia ya kipekee sanaa..mtu asiye kua na nidhamu huwezi kuruka viunzi na kuweza kupata daraja la upadrii..

Binafsi Mimi sina nidhamu ya kutoboa kusoma seminary ambapo rafiki yangu alifukuzwa pale MULUTUNGURU SEMINARY kisa alikutwa ziwani akipunga upepo muda ambao alitakiwa awepo darasani..

Ila familia ikiwa na wito wa ki padre mwisho wake inaweza ku extinct
 
Back
Top Bottom