GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 63,006
- 126,388
Kwa kifupi tu ni kwamba ulichokifanya Jana ni Akili ya Kitoto na Kipuuzi ya kutaka sasa Kuliingiza Kanisa Katoliki katika Sakata lako na Utawala wa sasa nchini.
Baada ya kuona huungwi mkono na Makanisa kwa kujifanya una Akili (wakati huna) ukatafuta Kanisa lililo na Ushawishi na Kubwa la Katoliki ambalo unahisi nalo lina Mgogoro na Utawala wa sasa ili ujibanie / ujifichie humo kusudi Wakatoliki wakuunge mkono katika Malalamiko yako.
Askofu Gwajima hivi unadhani Sisi Wakatoliki wenye Akili kubwa kukuzidi akina GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE hatujui au hatukumbuki Mahubiri yako katika Kanisa lako la Ufufuo na Uzima tokea ukiwa pale Kawe na kuhamia pale Ubungo yalikuwa ni ya Kutusema vibaya?
Askofu Gwajima hivi siyo Wewe uliyekuwa Ukitunanga Wakatoliki na Injili yetu? Siyo Wewe pamoja na Waumini wako Kutwa mnatusema vibaya Wakatoliki? Leo hii kwakuwa unatafuta Kuungwa mkono baada ya kuona hakuna Mtanzania mwenye Akili Timamu anakuelewa kutokana na Unafiki wako ndiyo unajifanya Kutuzungumzia Sisi Wakatoliki?
Na kama kweli ulikuwa na Hoja ya maana kwanini 90% ya Mazungumzo yako ya Jana ulikuwa unalijumuisha tu Kanisa moja la Katoliki huku ukiyaacha Madhehebu mengine na hata Ndugu zetu Waislamu?
Hayo Madhehebu mengine yalikuambia kuwa Wao hawana matatizo na Utawala wa sasa? Shida mbalimbali zilizopo sasa Tanzania zinawahusu na kuwaumiza tu Wakatoliki ila Walokole, Walutheri, Waanglikana, Madhehebu yenu ya Kiroho na Waislamu wao Kwao mambo ni poa na hakuna shida?
Askofu Gwajima unataka kusema kuwa TEC (Wakatoliki) ninaowajua Mimi (tena baadhi yao walikuwa ni Wahadhiri wangu SAUT Mwanza 2006-2009) ndiyo wamekutuma Jana uwe Msemaji wao kwa mtazamo wao juu ya Utawala wa sasa na Serikali ya CCM?
Labda nikuambie tu Askofu Gwajima kuwa Sisi Wakatoliki tunatambua kuwa kuna Changamoto fulani fulani katika Utawala wa sasa (ambazo hata katika Tawala zilizopita za nchi yetu ya Tanzania) zilikuwepo ila hatuzikabili kwa Chuki kama zako na Unafiki kama wako bali Wakatoliki hulka yetu ya Kitunu ni Kufanya majadiliano ya Kiutu, Uvumilivu na Hekima kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Askofu Gwajima ni nani labda alikudanganya kuwa ndani ya CCM na Serikali hakuna Waumini wa Kikatoliki? Tena labda nikusaidie tu kukutaarifu kuwa Wakatoliki ndiyo wengi Serikalini na hata katika CCM kuliko unavyodhania.
Kutujumuisha Wakatoliki katika Matatizo yako ya Kisiasa na hadi ya Kiimani ndani ya CCM na Serikali yake ni kutukosea sana Heshima na sijui ni Mpumbavu gani alikushauri uitumie Strategy hiyo ya kututumia Wakatoliki kama Daraja lako la kuwasilisha Hoja zako zilizojaa Chuki, Kisasi na Unafiki mwingi kwa wale unaowaona ni Maadui zako CCM na Serikali yake chini ya Rais Samia.
Askofu Gwajima unataka kusema kuwa katika Utawala wa Hayati Magufuli ambao Ulifaidika nao pakubwa Kisiasa na Kimaisha haya matatizo uliyoyaainisha kuwepo katika Awamu ya sasa (Utawala huu wa sasa wa Rais Samia) hayakuwepo tena kwa Ukubwa kabisa? Mbona wenye Akili kubwa hatukuwahi Kukuona ukiyashupalia na Kuyaongelea kama kweli Wewe ni Msemaji Kivuli wa Waumini wa Dini zote Tanzania?
Askofu Gwajima nakuomba iwe mwanzo na mwisho Kutuhusisha Wakatoliki na Bifu lako la Kiimani na Maslahi ya Kisiasa na CCM na Serikali yake. Wakatoliki hatuna Chuki hizo na ama Rais Samia au Serikali yake au Chama Cha Mapinduzi (CCM) na hata Vyama vingine vyote vya Kisiasa Tanzania bali tunapambana tu na Changamoto kadhaa zilizopo ambazo tunaamini kuwa Msaada wa Mwenyezi Mungu, Busara zetu na Hekima zetu tutazitatua kwa njia ya Amani kwa Kuwahusisha Watanzania wote bila kujali Imani zao au Dini zao au Vyama vyao vya Kisiasa na tunaamini kuwa kwa Mazungumzo na Masikilizano basi ipo Siku tu mambo yote yatakaa sawa kwa Maslahi ya Mama Tanzania.
Baada ya kuona huungwi mkono na Makanisa kwa kujifanya una Akili (wakati huna) ukatafuta Kanisa lililo na Ushawishi na Kubwa la Katoliki ambalo unahisi nalo lina Mgogoro na Utawala wa sasa ili ujibanie / ujifichie humo kusudi Wakatoliki wakuunge mkono katika Malalamiko yako.
Askofu Gwajima hivi unadhani Sisi Wakatoliki wenye Akili kubwa kukuzidi akina GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE hatujui au hatukumbuki Mahubiri yako katika Kanisa lako la Ufufuo na Uzima tokea ukiwa pale Kawe na kuhamia pale Ubungo yalikuwa ni ya Kutusema vibaya?
Askofu Gwajima hivi siyo Wewe uliyekuwa Ukitunanga Wakatoliki na Injili yetu? Siyo Wewe pamoja na Waumini wako Kutwa mnatusema vibaya Wakatoliki? Leo hii kwakuwa unatafuta Kuungwa mkono baada ya kuona hakuna Mtanzania mwenye Akili Timamu anakuelewa kutokana na Unafiki wako ndiyo unajifanya Kutuzungumzia Sisi Wakatoliki?
Na kama kweli ulikuwa na Hoja ya maana kwanini 90% ya Mazungumzo yako ya Jana ulikuwa unalijumuisha tu Kanisa moja la Katoliki huku ukiyaacha Madhehebu mengine na hata Ndugu zetu Waislamu?
Hayo Madhehebu mengine yalikuambia kuwa Wao hawana matatizo na Utawala wa sasa? Shida mbalimbali zilizopo sasa Tanzania zinawahusu na kuwaumiza tu Wakatoliki ila Walokole, Walutheri, Waanglikana, Madhehebu yenu ya Kiroho na Waislamu wao Kwao mambo ni poa na hakuna shida?
Askofu Gwajima unataka kusema kuwa TEC (Wakatoliki) ninaowajua Mimi (tena baadhi yao walikuwa ni Wahadhiri wangu SAUT Mwanza 2006-2009) ndiyo wamekutuma Jana uwe Msemaji wao kwa mtazamo wao juu ya Utawala wa sasa na Serikali ya CCM?
Labda nikuambie tu Askofu Gwajima kuwa Sisi Wakatoliki tunatambua kuwa kuna Changamoto fulani fulani katika Utawala wa sasa (ambazo hata katika Tawala zilizopita za nchi yetu ya Tanzania) zilikuwepo ila hatuzikabili kwa Chuki kama zako na Unafiki kama wako bali Wakatoliki hulka yetu ya Kitunu ni Kufanya majadiliano ya Kiutu, Uvumilivu na Hekima kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Askofu Gwajima ni nani labda alikudanganya kuwa ndani ya CCM na Serikali hakuna Waumini wa Kikatoliki? Tena labda nikusaidie tu kukutaarifu kuwa Wakatoliki ndiyo wengi Serikalini na hata katika CCM kuliko unavyodhania.
Kutujumuisha Wakatoliki katika Matatizo yako ya Kisiasa na hadi ya Kiimani ndani ya CCM na Serikali yake ni kutukosea sana Heshima na sijui ni Mpumbavu gani alikushauri uitumie Strategy hiyo ya kututumia Wakatoliki kama Daraja lako la kuwasilisha Hoja zako zilizojaa Chuki, Kisasi na Unafiki mwingi kwa wale unaowaona ni Maadui zako CCM na Serikali yake chini ya Rais Samia.
Askofu Gwajima unataka kusema kuwa katika Utawala wa Hayati Magufuli ambao Ulifaidika nao pakubwa Kisiasa na Kimaisha haya matatizo uliyoyaainisha kuwepo katika Awamu ya sasa (Utawala huu wa sasa wa Rais Samia) hayakuwepo tena kwa Ukubwa kabisa? Mbona wenye Akili kubwa hatukuwahi Kukuona ukiyashupalia na Kuyaongelea kama kweli Wewe ni Msemaji Kivuli wa Waumini wa Dini zote Tanzania?
Askofu Gwajima nakuomba iwe mwanzo na mwisho Kutuhusisha Wakatoliki na Bifu lako la Kiimani na Maslahi ya Kisiasa na CCM na Serikali yake. Wakatoliki hatuna Chuki hizo na ama Rais Samia au Serikali yake au Chama Cha Mapinduzi (CCM) na hata Vyama vingine vyote vya Kisiasa Tanzania bali tunapambana tu na Changamoto kadhaa zilizopo ambazo tunaamini kuwa Msaada wa Mwenyezi Mungu, Busara zetu na Hekima zetu tutazitatua kwa njia ya Amani kwa Kuwahusisha Watanzania wote bila kujali Imani zao au Dini zao au Vyama vyao vya Kisiasa na tunaamini kuwa kwa Mazungumzo na Masikilizano basi ipo Siku tu mambo yote yatakaa sawa kwa Maslahi ya Mama Tanzania.