Askofu Bagonza: Anayetugawa hawezi kutuunganisha

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,015
Tofauti za dini zilishindwa kutugawa. Serikali haina dini na hakuna anayelazimishwa kuwa na dini. Tofauti za makabila zilishindwa kuligawa Taifa. Makabila madogo yana fursa sawa kama makabila makubwa. Faida ya makabila ni kutambika na kufanya fujo katika misiba ya watani.

Tofauti ya rangi ya ngozi ya mwili haikuligawa Taifa. Baada wa kupata uhuru, baadhi ya waliokuwa wanaitwa wakoloni waliteuliwa kuwa mawaziri. Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja. Tofauti za vipato hazikuligawa Taifa. Tajiri na maskini wanaweza kunyea ndoo moja huko mahabusu. Utajiri ni wa mtu lakini umaskini ni wa Taifa. Aliyewapa hawa ndiye kawanyima wale.

Tofauti za kiitikadi zinaligawa na kulisambaratisha Taifa letu. Kwanini?

1. Tofauti za kiitikadi zaweza kukutia hatiani au kukuweka huru.

2. Tofauti za kiitikadi zaweza kukupa au kukunyima maji ya bomba, barabara, HOSPITALI na
Shule.

3. Tofauti za kiitikadi zaweza kumpa uongozi kichaa na kumnyima Profesa kazi hiyo. Chama kinakuwa bora kuliko mtu. Hatuko salama.

4. Chama kinakuwa na nguvu kuliko Muumba. Mmoja amependekeza akishinda atabadili jina la nchi liwe la chama chake! Mitume hawasikilizwi lakini makada wanashangiliwa. Ukame ukija tusitafutane.

Viongozi wa dini ombeeni na kugawa baraka kwa rangi zote. Wanyambo walisema "Lisha mbwa wote washibe kwa usawa na bila upendeleo maana hujui ni yupi atakayewinda vizuri na kupata mawindo". Na watani wangu wa Tarime husema, "Asiyetembelea kwa mtemi huwa ananungunika eti mtemi ni bahili".

Baba Askofu Bagonza.
 
Lissu hatajenga barabara, shule wala zahanati maana hayo ni maendeleo ya vitu.

Atakachokifanya ni kuwafukuza wamachinga barabarani maana hayo ndiyo maendeleo ya watu.
 
Huko Visiwani CCM inajitahidi kuwagawa Wananchi na kuwaita 'Machotara' ni aibu tupu.
ushahidi huu hapa
DSC_2469.jpg
 
Wewe hata kujitambua hujitambui. Njaa mbaya sana! Angalia ulivyopoteza utu wako na kudharaulika kila kona Nchini.

Uchumi wa Magufuli: Sekta Binafsi ina-Suffer. Yalianza Maduka, Yakafuata Mashirika, Sasa ni Zamu ya Media Ina-suffer!

Mimi mwenyewe na kale kajikampuni kangu ka PPR, ambapo tulibamba sana tenda za serikali, mwanzo tulikuwa na wafanyakazi 20, tukipangisha jengo la NHC pale Mtaa wa Mkwepu kwa kodi ya pango kwa mwezi, ya zaidi ya mshahara wa DC, sasa hakuna tena tenders za serikali, serikali inatangaza moja kwa moja na TBC, mwaka huu pia tenda zangu za kutangaza Maonyesho ya Saba Saba na Nane Nane zimefutwa, hivyo tumepunguza wafanyakazi 15!, tumebaki 5!. Na Mtaa wa Mkwepu hapakaliki hivyo tumehama, tumehamia jengo la Posta House kwenye kajichumba.

Mkuu AGITATOR , usiwajali vibaraka hawa, mwisho wao ni October 28, watalia sana!.

P
 
Mkuu AGITATOR , usiwajali vibaraka hawa, mwisho wao ni October 28, watalia sana!.
P
Africa is fighting independence for the second time everywhere. This indigenous colonialists like maccm /paskali mayala represent the worst form of colonialism, because they can camouflage as if they have the best interest of people.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tofauti za dini zilishindwa kutugawa. Serikali haina dini na hakuna anayelazimishwa kuwa na dini. Tofauti za makabila zilishindwa kuligawa Taifa. Makabila madogo yana fursa sawa kama makabila makubwa. Faida ya makabila ni kutambika na kufanya fujo katika misiba ya watani.

Tofauti ya rangi ya ngozi ya mwili haikuligawa Taifa. Baada wa kupata uhuru, baadhi ya waliokuwa wanaitwa wakoloni waliteuliwa kuwa mawaziri. Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja. Tofauti za vipato hazikuligawa Taifa. Tajiri na maskini wanaweza kunyea ndoo moja huko mahabusu. Utajiri ni wa mtu lakini umaskini ni wa Taifa. Aliyewapa hawa ndiye kawanyima wale.

Tofauti za kiitikadi zinaligawa na kulisambaratisha Taifa letu. Kwanini?

1. Tofauti za kiitikadi zaweza kukutia hatiani au kukuweka huru.

2. Tofauti za kiitikadi zaweza kukupa au kukunyima maji ya bomba, barabara, HOSPITALI na
Shule.

3. Tofauti za kiitikadi zaweza kumpa uongozi kichaa na kumnyima Profesa kazi hiyo. Chama kinakuwa bora kuliko mtu. Hatuko salama.

4. Chama kinakuwa na nguvu kuliko Muumba. Mmoja amependekeza akishinda atabadili jina la nchi liwe la chama chake! Mitume hawasikilizwi lakini makada wanashangiliwa. Ukame ukija tusitafutane.

Viongozi wa dini ombeeni na kugawa baraka kwa rangi zote. Wanyambo walisema "Lisha mbwa wote washibe kwa usawa na bila upendeleo maana hujui ni yupi atakayewinda vizuri na kupata mawindo". Na watani wangu wa Tarime husema, "Asiyetembelea kwa mtemi huwa ananungunika eti mtemi ni bahili".

Baba Askofu Bagonza.
Ni ajabu na kweli mtu anatafuta kura kwa kuwatishia wapigakura kura. Eti huwezi kuwapelekea maendeleo kwa sababu za utofauti wa kiitikadi. Hapo ndipo utakapo tambua kosa lililopo la kikatiba kutoa madaraka makubwa mno kwa mtu mmoja aliyekosa hekima na busara.

Hoja za askofu Bagonza zina mantiki kubwa sana. Ukiona mtu anazipinga ujue tu ni kwa sababu zitokanazo na unafiki tu na wala si vinginevyo. Watawala wa sasa wamejisahau kabisa, hawakumbuki tena ya kwamba madaraka ni dhamana waliyokabidhiwa kupitia matakwa ya kikatiba.

Wameamua kwa makusudi kushupaza shingo zao, hii hutokana na wao kujawa na kiburi cha uzima. Muumba wao hawakubali hata Ibilisi naye amekaa mbali nao. Ni heri kama wangalikuwa ni moto ama baridi ingalieleweka, lkn kwa kuwa wao ni vuguvugu basi watatapikwa na kukosa radhi itokayo mbinguni (rejea Ufunuo 13:14-16)
 
Back
Top Bottom