JWTZ kama baadhi yenu mpo humu jukwaani, basi mnatakiwa mjitafakari. Mimi sitawatukana. Isipokuwa nitawapa tu ushauri wa bure.
Wakati mwingine wekezeni nguvu kubwa kwenye ulinzi wa raslimali za Taifa mfano madini, wanyama, pembe za ndovu, fedha za walipa kodi, bahari, nk. Badala ya kuhangaika kuwalinda watawala walioingia madarakani kwa njia za hila, ikiwemo wizi wa kura!
Pia mnatakiwa kufahamu hiyo mishahara na posho mnazolipwa zinatokana na kodi za wananchi hao hao mnaowazuia kuandamana ili tu kudai haki zao za msingi kutoka kwa watawala viziwi na wenye dharau.