Asante kwa Rais Samia kwa kuruhusu binti huyu aote tena

Anna Nkya

Member
Oct 21, 2021
69
341
Kabla nawe hujageuka mchawi, tazama video niliyokuwekea halafu usiwe mgumu wa kuelewa.

Aliyeruhusiwa kuota tena ni binti wa Kitanzania, popote pale alipo. Nazungumzia binti yeyote ambaye sasa ameruhusiwa kurudi shule (Kuota tena) kupambania ndoto yake baada ya kukukosea na kupata ujauzito. MFANO MZURI NI HUYO ANAYEONGEA HAPO KWENYE VIDEO.

Wachawi ni wale watu wote ambao wanajipa kazi ya Mungu kuhukumu, na kusema kwamba hawa mabinti hawana haki ya kurudi shuleni kupambania ndoto zao.

Rais Samia anawaruhusu hawa mabinti kuota tena kwani hizo mimba walizopata halijawahi kuwa tamanio lao, wengine wamezipata kwa kubwaka au kurubuniwa, ama ufinyu tu wa kuwaza mbali jambo ambalo sidhani kama linawafanya wakose haki ya kujiuliza tena na kupambania ndoto zao.

Ni uchawi wa hali ya juu kutaka binti kama huyo wa kwenye video hapo chini aendelee kujiona maisha yake yamefika mwisho, anyimwe kabisa nafasi ya kupambani tena ndoto zake. Ni uchawi kwa sababu hao wanaofanya hivyo pia wana madhaifu yao, wamewahi kukosea lakini wanapata nafasi ya kurekebisha.

ARUDI SHULE, Asante kwa Rais Samia kwa kuruhusu binti huyu aote tena.

KWAKO BINTI UTAYERUDI SHULE : Waoneshe uwezo wako, usikubali kurubuniwa tena, usikubali kukata tamaa.
 

Attachments

  • UJAUZITO WANAFUNZI.mp4
    42.8 MB
Hapa kuna siasa fulani fulani, hakuna binti mwenye ujasiri wa kurudi shule ileile aliyoondolewa kwa sababu ya ujauziyo,stajinyanyapaa na kunyanyapaliwa hapo shuleni. Kama serikali inamaanisha kweli basi haina budi kuwatafutia shule nyingine tofauti na ile ya awali.

Vv
 
Watoto watazaaa kama njugu. Mimi niliona hili swala lingekua kwa wale tuu waliobakwa maybe na its has been proven beyond doubt kwamba amebakwa..sio kila mtoto na tamaa zake amebeba huko halafu warudi shule
 
Kabla nawe hujageuka mchawi, tazama video niliyokuwekea halafu usiwe mgumu wa kuelewa.

Aliyeruhusiwa kuota tena ni binti wa Kitanzania, popote pale alipo. Nazungumzia binti yeyote ambaye sasa ameruhusiwa kurudi shule (Kuota tena) kupambania ndoto yake baada ya kukukosea na kupata ujauzito. MFANO MZURI NI HUYO ANAYEONGEA HAPO KWENYE VIDEO.

Wachawi ni wale watu wote ambao wanajipa kazi ya Mungu kuhukumu, na kusema kwamba hawa mabinti hawana haki ya kurudi shuleni kupambania ndoto zao.

Rais Samia anawaruhusu hawa mabinti kuota tena kwani hizo mimba walizopata halijawahi kuwa tamanio lao, wengine wamezipata kwa kubwaka au kurubuniwa, ama ufinyu tu wa kuwaza mbali jambo ambalo sidhani kama linawafanya wakose haki ya kujiuliza tena na kupambania ndoto zao.

Ni uchawi wa hali ya juu kutaka binti kama huyo wa kwenye video hapo chini aendelee kujiona maisha yake yamefika mwisho, anyimwe kabisa nafasi ya kupambani tena ndoto zake. Ni uchawi kwa sababu hao wanaofanya hivyo pia wana madhaifu yao, wamewahi kukosea lakini wanapata nafasi ya kurekebisha.

ARUDI SHULE, Asante kwa Rais Samia kwa kuruhusu binti huyu aote tena.

KWAKO BINTI UTAYERUDI SHULE : Waoneshe uwezo wako, usikubali kurubuniwa tena, usikubali kukata tamaa.
Lakini si amefafanua kuwa msamaha huo hauwahusu mabinti wa shule za msingi? Au sikumuelewa? Kama ni kweli basi pongezi umezitoa mapema mno.

Amandla...
 
Samia a real money faita...skatai kabsa kwa mabnt hawa kurud school shda family ming hawatawasapot plus school zile wanakwenda naunga mkono hoja but wapelekwe another school
 
Watoto watazaaa kama njugu. Mimi niliona hili swala lingekua kwa wale tuu waliobakwa maybe na its has been proven beyond doubt kwamba amebakwa..sio kila mtoto na tamaa zake amebeba huko halafu warudi shule
Kwa sababu wanaitwa watoto, hivyo kila aliyepata mimba kwenye umri huo anahesabika amebakwa ndiyo maana wanaume, kama ni watu wazima wanashitakiwa kwa kosa la kubaka.
 
Back
Top Bottom