Rais Samia ameua ndoto ya Urais kwa wanawake wengine nchini!

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,976
Katika dunia hii kila kitu kina mwanzo na mwisho.

Mwanzo wa suala lolote hujenga msingi ambao unakuwa ni rejeo kwa kizazi na kizazi bila kujali kama ni mzuri au mbaya.

Historia yetu inabainisha wakoloni walikuwa na dhana ya kuwa Watanzania hatuna uwezo wa kujiongoza/kujitawala. Hii dhana ilitumika vizuri kwa muda mrefu ili kuhakikisha hatupati uhuru wetu na kujitawala.

Kwa nchini mwetu, uongozi wa Rais Nyerere ulifuta dhana hiyo na kuweka msingi na rejeo ambalo mpaka sasa linatumika katika kupima uongozi na uzalendo wa Rais nchini.

Kutokana na mfumo dume kutamalaki nchini, dhana ya wanawake kushika uongozi wa juu imekuwa ikipingwa sana na waumini wa mfumo dume nchini lakini dhana hii ilipata mtihani baada ya Rais Samia kushika nafasi ya juu ya uongozi wa kurithi nchini.

Urais wa Rais Samia ulikuwa na fursa ya kuifuta hii dhana ya mfumo dume lakini kutokana na hulka za uongozi za Rais Samia ambazo zimeonyesha wazi kuwa hana karama, kipaji na ujuzi wa uongozi unafanya wanaopigia chapuo dhana ya mfumo dume nchini wanaonekana wako sahihi na kwa msingi huo ameua ndoto za wasichana na wanawake wengine nchini wanaofikiria kushika uongozi wa juu kabisa serikalini kwa sababu hawataaminiwa tena nchini.

Kwa sasa itachukua miongo mingi kwa wanawake nchini kuja kuaminiwa na umma kushika tena nafasi ya Urais nchini kwa sababu ya rejea ya uongozi mbovu wa Rais Samia.

Nimesikia baadhi ya wanawake wameanza kuwalaumu wanaume kuwa ndio chanzo cha kushindwa kwa uongozi wa Rais Samia. Mmojawapo aliyetia lawama hizo kwa wanaume ni Mama Gertrude Mongella.
Angalia video;



Kuna baadhi pia wanasema eti anashauliwa vibaya au eti kuna “genge” la washauri linataka asifanikiwe. Ukijiuliza, kwani hilo “genge” au kundi aliyeliweka katika nafasi za kumshauri ni nani? Kwa mantiki hii tukubali kuwa Rais Samia hajui anachokifanya au ni kama “remote control” na kuna mtu/watu wengine wanaitumia!

Yaani Rais Samia anavurunda halafu lawama wanabebeshwa wanaume.

Kuendelea kuwabebesha lawama wanaume au viongozi wengine haimsafishi Rais Samia bali inazidi kuonyesha kuwa hana karama, kipaji na ujuzi wa uongozi. Hii pia inaonyesha ni Rais kivuli!

Katiba yetu katika Ibara ya 33 na Ibara ya 36 imempa Rais madaraka makubwa na uwezo wa kuajiri na kufukuza mtumishi yeyote wa serikali bila kuhojiwa au kuwajibika kwa mtu/taasisi yoyote nchini. Hii ina maana kuwa lolote linalofanyika serikalini linakuwa na baraka/limekubaliwa na Rais kama hajakanusha.

Kwa miongo mingi ijayo wanawake nchini watakuwa wanapimwa kwa kutumia kigezo cha uongozi mbovu wa Rais Samia.

Wanawake ni vema kwa sasa watambue “mchawi” wao katika kuaminiwa na jamii kubwa kuanzia sasa ni Rais Samia na sio wapenda mfumo dume kwa sababu toka Rais Samia apate Urais amejitahidi kuufungamanisha Urais wake na jinsia ya kike huku akijiita Mama na kutaka watanzania wamuone kama Mama.
 
Ni kweli dhana ya mwanamke haifai kuwa kiongozi au mtu wa mwisho katika maamuzi bali kuwa msaidizi inashika nafasi yake kwa usahihi wakati huu wa uongozi wa huyu rais wetu .
Kwa sisi ambao tunakutana wa wengi hasa wakina mama wengi kama sio wote wamekubali pasina shaka kwamba wao kwa hakika hapaswi kua kiongozi wa juu kabisa .

Sote tumeona tumeshuhudia na tumeamini mwanamke hatoshi kushika madaraka makubwa labda msaidizi .

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
 
Kwa hivyo naye ndio analididimiza zaidi kisa wanaume walifanya vibaya. Mimi kukaa bila umeme kumenifanya nione Sina Rais
Sasa kama wanaume nao hawakuweza kuiletea maendeleo nchi ,hiyo hoja ya kijinsia iliyo tolewa na mleta mada ina toka wapi?
Hapa Tz tatizo sio jinsia au wana siasa tatizo ni jamii nzima ya Kitanzania ni jamii iliyo jaa wapumbavu.
 
Katika dunia hii kila kitu kina mwanzo na mwisho.

Mwanzo wa suala lolote hujenga msingi ambao unakuwa ni rejeo kwa kizazi na kizazi bila kujali kama ni mzuri au mbaya.

Historia yetu inabainisha wakoloni walikuwa na dhana ya kuwa Watanzania hatuna uwezo wa kujiongoza/kujitawala. Hii dhana ilitumika vizuri kwa muda mrefu ili kuhakikisha hatupati uhuru wetu na kujitawala.

Kwa nchini mwetu, uongozi wa Rais Nyerere ulifuta dhana hiyo na kuweka msingi na rejeo ambalo mpaka sasa linatumika katika kupima uongozi na uzalendo wa Rais nchini.

Kutokana na mfumo dume kutamalaki nchini, dhana ya wanawake kushika uongozi wa juu imekuwa ikipingwa sana na waumini wa mfumo dume nchini lakini dhana hii ilipata mtihani baada ya Rais Samia kushika nafasi ya juu ya uongozi wa kurithi nchini.

Urais wa Rais Samia ulikuwa na fursa ya kuifuta hii dhana ya mfumo dume lakini kutokana na hulka za uongozi za Rais Samia ambazo zimeonyesha wazi kuwa hana karama, kipaji na ujuzi wa uongozi unafanya wanaopigia chapuo dhana ya mfumo dume nchini wanaonekana wako sahihi na kwa msingi huo ameua ndoto za wasichana na wanawake wengine nchini wanaofikiria kushika uongozi wa juu kabisa serikalini kwa sababu hawataaminiwa tena nchini.

Kwa sasa itachukua miongo mingi kwa wanawake nchini kuja kuaminiwa na umma kushika tena nafasi ya Urais nchini kwa sababu ya rejea ya uongozi mbovu wa Rais Samia.

Nimesikia baadhi ya wanawake wameanza kuwalaumu wanaume kuwa ndio chanzo cha kushindwa kwa uongozi wa Rais Samia. Mmojawapo aliyetia lawama hizo kwa wanaume ni Mama Gertrude Mongella.
Angalia video;

View attachment 2765193

Kuna baadhi pia wanasema eti anashauliwa vibaya au eti kuna “genge” la washauri linataka asifanikiwe. Ukijiuliza, kwani hilo “genge” au kundi aliyeliweka katika nafasi za kumshauri ni nani? Kwa mantiki hii tukubali kuwa Rais Samia hajui anachokifanya au ni kama “remote control” na kuna mtu/watu wengine wanaitumia!

Yaani Rais Samia anavurunda halafu lawama wanabebeshwa wanaume.

Kuendelea kuwabebesha lawama wanaume au viongozi wengine haimsafishi Rais Samia bali inazidi kuonyesha kuwa hana karama, kipaji na ujuzi wa uongozi. Hii pia inaonyesha ni Rais kivuli!

Katiba yetu katika Ibara ya 33 na Ibara ya 36 imempa Rais madaraka makubwa na uwezo wa kuajiri na kufukuza mtumishi yeyote wa serikali bila kuhojiwa au kuwajibika kwa mtu/taasisi yoyote nchini. Hii ina maana kuwa lolote linalofanyika serikalini linakuwa na baraka/limekubaliwa na Rais kama hajakanusha.

Kwa miongo mingi ijayo wanawake nchini watakuwa wanapimwa kwa kutumia kigezo cha uongozi mbovu wa Rais Samia.

Wanawake ni vema kwa sasa watambue “mchawi” wao katika kuaminiwa na jamii kubwa kuanzia sasa ni Rais Samia na sio wapenda mfumo dume!
Alianza urais wake kwa kujitetea kupitia jinsia

Kiufupi mama ametuangusha vibaya mno. Wanaomuaminisha kuwa haya tunayoyasema ni kelele za mitandaoni lakini hawamwambii ukweli kwamba sisi wa mitandaoni hatutoki kata moja
 
Ni kweli dhana ya mwanamke haifai kuwa kiongozi au mtu wa mwisho katika maamuzi bali kuwa msaidizi inashika nafasi yake kwa usahihi wakati huu wa uongozi wa huyu rais wetu .
Kwa sisi ambao tunakutana wa wengi hasa wakina mama wengi kama sio wote wamekubali pasina shaka kwamba wao kwa hakika hapaswi kua kiongozi wa juu kabisa .

Sote tumeona tumeshuhudia na tumeamini mwanamke hatoshi kushika madaraka makubwa labda msaidizi .

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
Wenye mtazamo wa namna hiyo ni wapumbavu, hata na ww kama mtazamo wako ndo huo na ww ni mpumbavu.

Kwa mtazamo wenu huo mnamaanisha kuwa mwaume ni bora kuliko mwanamke kwenye uongozi, lakini mna sahau kuwa tangu nchi hii ipate uhuru imeongozwa na wanaume watano (5) kwa zaidi ya miaka 60 lakini wameshindwa kumaliza hata tatizo la vyoo mashuleni ,
Sasa huyu mama mnataka afanye maajabu gani ndani ya Tz hii ambayo hao wanaume watano walishindwa kufanya kwa zaidi ya miaka 60?

Tatizo la nchi hii halipo kwa wanasiasa wa nchi hii tatizo liko kwa jamii nzima ya watz.
 
Ni kweli dhana ya mwanamke haifai kuwa kiongozi au mtu wa mwisho katika maamuzi bali kuwa msaidizi inashika nafasi yake kwa usahihi wakati huu wa uongozi wa huyu rais wetu .
Kwa sisi ambao tunakutana wa wengi hasa wakina mama wengi kama sio wote wamekubali pasina shaka kwamba wao kwa hakika hapaswi kua kiongozi wa juu kabisa .

Sote tumeona tumeshuhudia na tumeamini mwanamke hatoshi kushika madaraka makubwa labda msaidizi .

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
Yani hao wanawake wachache unaokutana nao ndio wakufanye ufikie hitimisho kwamba tumekubali hatupaswi kupewa nafasi za juu?

Angela Merkel ni mwanaume? Tena nafasi ya juu kwa nchi kubwa kama Germany na aliongoza kwa ufanisi mkubwa. Vipi Rais wa Croatia?
Watu mnakutana na wanamama vilabu vya mataputapu huko mnasikiliza mawazo yao ndio mnayatumia kama reference, sio sawa.
 
Back
Top Bottom