Beleave you me Basilio Matei was a real professional. This guy calling himself Tobias Andengenye sijua hata kama anajua kazi zake vizuri au ni maelekezo ya aliyemteu kuwa anaweza ku-behave anyhow. Mimi namfahamu toka akiwa Morogoro kuwa ni mtu wa kupigana na wake zake kila kukicha, nahofia hiyo altitude yake ya ugomvi (confrontation) will never work for him in Arusha.
Nasema Basilio was professional kwa sababu alikuwa anatumia resources alizopewa vizuri kwa maana ya kulinda usalama/utulivu na sio kuvuruga usalama/utulivu. Imagine RPC Tobias kama ndio angekuwa anasimamia mkoa wa Arusha wakati wa uchanguzi mkuu. Sidhani kama uchaguzi ungefanyika kwa utulivu/amani. Mtu anashindwa kusimamia uchaguzi wa umeya tu!!.
Leo kulikuwa kufanyike mkutano wa CDM maeneo ya uwanja wa NMC, badala ya RPC kutimia resources alizonazo kulinda mkutano ufanyike kwa amani yeye anaupiga marufuku nakutoka sababu kibao ambao actually zinamfanya yeye kuoneka si professional au hata kuwa hajua kazi yake vizuri, unless ametumwa na viongozi wake.
Katika kauli ya RPC (Triple A radio) ya kufuta mkutano huo pamoja na aliyosema ni kuwa maombi ya Kibali yalikuwa yametolewa siku 29 kabla ya mkutano badala ya siku 48, pili sababu za mkutano huo hazikutolewa!! sababu nyingine ni taarifa za ki-intelligence kuna vijana watafanya fujo kwa kubomoa maduka na kuwa wenye maduka hawatakubali nao itabidi wajitetee na hivo kuvuruga amani. Kutokana na sababu hizo anafuta mkutano.
Great thinkers hivi huyu Tobia Andengenye anataka kutuambia kuwa aliyapokea maombi ya CDM au aliyakataa in the first place? Je wakati CDM wanafanya matangazo ya huo mkutano walikuwa na kibali cha polisi au la. Je hayo mapungufu aliyosema alishauriana na CDM? au aliona kuwa ni sababu nzuri kwake za kusitisha mkutano siku ya mkutano? Najiuliza maswali mengi lakini nachoona ni unafiki mkubwa tu ambao RPC anajaribu kuuonyesha kwa kudhania kuwa huenda anawaimpress wakuu wake. Kwa maelezo yake mwenyewe kwa vyombo vya habari ni wazi kuwa hakuwashauri CDM kuwa maombi yao yana mapungufu bali alitoa kibali na baadae kukipinga!!
Nionavyo mimi kwanza behavior ya RPC Tobias inaharibu utulivu wa mji wa Arusha pia sina hakika sana kama RPC Tobias anaelewa implications ya shughuli zake. Pili Arusha si kama Morogoro au Pwani hulka na tabia za watu wa mkoa huu ni tofauti sana na mikoa mingine. Kwa tabia ya RPC huyu ni wazi kuwa kikazi hatadumu mkoa wa Arusha na ambao anadhani kuwa anawafurahisha watakuwa wa kwanza kumtimua mkoani Arusha. Kwa ushauri ni kwamba Arusha haitawaliwi kwa nguvu bali ni kwa hekima zaidi kama anataka kujifunza awaulize ma-RPC waliomtangulia!