Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 4,783
- 14,975
Arusha: Rais Samia akishiriki Mkutano wa 25 wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Machi 7, 2026
Rais wa Uganda, Yoweri Kaguta Museveni, amechaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), akichukua nafasi ya Rais wa Kenya, William Ruto, ambaye amemaliza muda wake wa uongozi wa mwaka mmoja.
Tukio hilo la makabidhiano ya vitendea kazi limefanyika leo, Machi 7, 2026, wakati wa Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa EAC unaofanyika jijini Arusha.
Hii ni mara ya nne kwa Rais Museveni kushika wadhifa huo wa juu tangu kuanzishwa kwa jumuiya hiyo, jambo linalomfanya kuwa mmoja wa viongozi wenye uzoefu mkubwa zaidi katika masuala ya mtangamano wa Afrika Mashariki.
Mara tu baada ya kupokea kijiti, Rais Museveni ameanza rasmi majukumu yake kwa kuongoza vikao vya Mkutano huo wa 25 wa Wakuu wa Nchi, ambapo ajenda kuu ni pamoja na usalama wa kikanda, biashara, na uzinduzi wa mifumo mipya ya forodha
Balozi Stephen Patrick Mbundi Ateuliwa kuwa Katibu Mkuu Mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)
Balozi Stephen Patrick Mbundi, ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kabla ya uteuzi wake, alikuwa Katibu Mkuu katika Wizara ya Mambo ya Nje akisimamia masuala ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Kuanzia Bunge lijalo, Wabunge wa EAC kulipwa mishahafa na nchi zao
Katika hatua kubwa ya kupunguza matumizi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Wakuu wa Nchi wamepitisha uamuzi kuwa kuanzia Bunge lijalo la jumuiya hiyo (EALA), mishahara ya wabunge wa bunge hilo itagharamiwa na mataifa wanayotoka badala ya jumuiya.
Mwenyekiti aliyemaliza muda wake wa EAC, William Ruto amebainisha hayo leo, Machi 7, 2026, jijini Arusha, wakati wa Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), akieleza kuwa mishahara hiyo kwa sasa inachukua takriban 30% ya bajeti yote ya jumuiya.
Chini ya utaratibu huu mpya, EAC itabakiwa na jukumu la kulipa posho pekee pale wabunge hao wanapokuwa katika shughuli za kikazi za jumuiya, hali itakayookoa rasilimali nyingi kuelekezwa kwenye miradi ya kimaendeleo.
“Hatua hiyo itapunguza kwa kiasi kikubwa mzigo kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki ili tuweze kutumia rasilimali nyingi zaidi katika kuhakikisha tuna Jumuiya yenye ufanisi. Ni posho za wabunge pekee ndizo zitalipwa na EAC wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao, lakini mishahara italipwa na nchi zao binafsi”, ameeleza Ruto.
Kutokana na jumuiya kukua hadi kufikia nchi nane, mfumo wa awali wa kuhitaji makubaliano ya wote ulikuwa unachelewesha ufanisi. Sasa, maamuzi yatatolewa kwa makubaliano au kwa kura za 65% ya wanachama.
Ruto amesema kuwa mabadiliko haya ni muhimu kwa sababu sheria zilizoanzisha jumuiya hiyo ziliandikwa wakati kukiwa na nchi tatu pekee, hivyo hazikukidhi mahitaji ya sasa ambapo jumuiya inaendelea kutanuka.
Rais wa Uganda, Yoweri Kaguta Museveni, amechaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), akichukua nafasi ya Rais wa Kenya, William Ruto, ambaye amemaliza muda wake wa uongozi wa mwaka mmoja.
Tukio hilo la makabidhiano ya vitendea kazi limefanyika leo, Machi 7, 2026, wakati wa Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa EAC unaofanyika jijini Arusha.
Hii ni mara ya nne kwa Rais Museveni kushika wadhifa huo wa juu tangu kuanzishwa kwa jumuiya hiyo, jambo linalomfanya kuwa mmoja wa viongozi wenye uzoefu mkubwa zaidi katika masuala ya mtangamano wa Afrika Mashariki.
Mara tu baada ya kupokea kijiti, Rais Museveni ameanza rasmi majukumu yake kwa kuongoza vikao vya Mkutano huo wa 25 wa Wakuu wa Nchi, ambapo ajenda kuu ni pamoja na usalama wa kikanda, biashara, na uzinduzi wa mifumo mipya ya forodha
Balozi Stephen Patrick Mbundi Ateuliwa kuwa Katibu Mkuu Mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)
Balozi Stephen Patrick Mbundi, ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kabla ya uteuzi wake, alikuwa Katibu Mkuu katika Wizara ya Mambo ya Nje akisimamia masuala ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Kuanzia Bunge lijalo, Wabunge wa EAC kulipwa mishahafa na nchi zao
Katika hatua kubwa ya kupunguza matumizi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Wakuu wa Nchi wamepitisha uamuzi kuwa kuanzia Bunge lijalo la jumuiya hiyo (EALA), mishahara ya wabunge wa bunge hilo itagharamiwa na mataifa wanayotoka badala ya jumuiya.
Mwenyekiti aliyemaliza muda wake wa EAC, William Ruto amebainisha hayo leo, Machi 7, 2026, jijini Arusha, wakati wa Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), akieleza kuwa mishahara hiyo kwa sasa inachukua takriban 30% ya bajeti yote ya jumuiya.
Chini ya utaratibu huu mpya, EAC itabakiwa na jukumu la kulipa posho pekee pale wabunge hao wanapokuwa katika shughuli za kikazi za jumuiya, hali itakayookoa rasilimali nyingi kuelekezwa kwenye miradi ya kimaendeleo.
“Hatua hiyo itapunguza kwa kiasi kikubwa mzigo kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki ili tuweze kutumia rasilimali nyingi zaidi katika kuhakikisha tuna Jumuiya yenye ufanisi. Ni posho za wabunge pekee ndizo zitalipwa na EAC wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao, lakini mishahara italipwa na nchi zao binafsi”, ameeleza Ruto.
Kutokana na jumuiya kukua hadi kufikia nchi nane, mfumo wa awali wa kuhitaji makubaliano ya wote ulikuwa unachelewesha ufanisi. Sasa, maamuzi yatatolewa kwa makubaliano au kwa kura za 65% ya wanachama.
Ruto amesema kuwa mabadiliko haya ni muhimu kwa sababu sheria zilizoanzisha jumuiya hiyo ziliandikwa wakati kukiwa na nchi tatu pekee, hivyo hazikukidhi mahitaji ya sasa ambapo jumuiya inaendelea kutanuka.