Arusha: Mtoto ajinyonga na kuacha barua yenye ujumbe huu, 'Mungu mpe bibi hela ya marejesho'

Arusha: Mtoto ajinyonga na kuacha barua yenye ujumbe huu, 'Mungu mpe bibi hela ya marejesho'

TheCrocodile

JF-Expert Member
Joined
May 31, 2021
Posts
1,343
Reaction score
3,704
Mtoto mmoja wa kike mwenye umri wa miaka 11, darasa la sita anayefahamika kwa jina la Lightness Mkiindi, mkazi wa Mtaa wa Namayana, Kata ya Ilboru, wilayani Arumeru mkoani Arusha, amefariki dunia akidaiwa kujinyonga

Kwa mujibu wa maelezo ya mama mzazi na bibi wa marehemu, siku ya tukio Januari 29, mtoto huyo hakuenda shule kutokana na kuwepo kwa msiba wa jirani uliokuwa karibu na makazi yao, ambapo familia ilikuwa ikishiriki shughuli za maombolezo. Kabla ya tukio hilo, inaelezwa mtoto alikuwa nyumbani akicheza na wenzake.

Familia imesema walipokea taarifa ya dharura wakati wakiwa msibani, iliyomtaka mama wa mtoto kurejea nyumbani haraka. Alipofika, alikuta mtoto huyo tayari amefariki katika mazingira yanayoashiria alijinyonga kwa kutumia kanga ya kuogea.

"E baba Mungu ninaomba kwa niaba ya familia yangu na jamii nzima pamoja na majirani, Mungu naomba umpe bibi yangu hela pamoja na mama yangu pamoja na baba yangu, bibi yangu apate hela ya marejesho na baba na mama wapate hela ya ada ya shule. Mungu atusaidie, Milele Amina amefanya maajabu jina lake liimidiwe" ameandika mtoto ambaye anadaiwa kujinyonga bafuni.

Chanzo cha tukio hilo bado hakijabainika mara moja, huku tukio hilo likiacha majonzi makubwa kwa familia, ndugu na wakazi wa eneo hilo.

FB_IMG_1769873280256.jpg
 
Inasikitisha sana, Inawezekana mtoto alikuwa akisikia malalamiko ya Bibi yake kuhusu marejesho yakamletea stress na pengine yalikuwa yakihusishwa na ada zake akaona isiwe tabu.

NB:Nadhani matatizo yetu tusiruhusu watoto wayajue hasa wa umri mdogo
 
Duuh miaka 11 anapata vp mawazo ya kujinyonga?
Ni swali gumu pia lenye majibu tata.

Ninafikiri utandawazi unachangia.
Inawezekana dogo aliona tukio kama hilo kwenye mitandao ya kijamii la mtu kujinyonga na kuacha maandishi.
Kwa umri wake akaamua kuigiza bila kujua kwamba kwenye maigizo, kipengele cha "kujitundika" kuna utaalamu wake.

R.i.p toto..!
 
Ni swali gumu pia lenye majibu tata.

Ninafikiri utandawazi unachangia.
Dogo anawekana aliona tukio kama hilo kwenye mitandao ya kijamii la mtu kujinyonga na kuacha maandishi.
Kwa umri wake akaamua kuigiza bila kujua kwamba kwenye maigizo, kipengele cha "kujitundika" kuna utaalamu wake.

R.i.p toto..!
Kweli kabisa, inawezekana dogo alijua labda atarudi.... Hata hiyo barua yake anaomba pia mama yake apate hela ya ada (kwa ajili yake)
 
Mtoto mmoja wa kike mwenye umri wa miaka 11, darasa la sita anayefahamika kwa jina la Lightness Mkiindi, mkazi wa Mtaa wa Namayana, Kata ya Ilboru, wilayani Arumeru mkoani Arusha, amefariki dunia akidaiwa kujinyonga

Kwa mujibu wa maelezo ya mama mzazi na bibi wa marehemu, siku ya tukio Januari 29, mtoto huyo hakuenda shule kutokana na kuwepo kwa msiba wa jirani uliokuwa karibu na makazi yao, ambapo familia ilikuwa ikishiriki shughuli za maombolezo. Kabla ya tukio hilo, inaelezwa mtoto alikuwa nyumbani akicheza na wenzake.

Familia imesema walipokea taarifa ya dharura wakati wakiwa msibani, iliyomtaka mama wa mtoto kurejea nyumbani haraka. Alipofika, alikuta mtoto huyo tayari amefariki katika mazingira yanayoashiria alijinyonga kwa kutumia kanga ya kuogea.

"E baba Mungu ninaomba kwa niaba ya familia yangu na jamii nzima pamoja na majirani, Mungu naomba umpe bibi yangu hela pamoja na mama yangu pamoja na baba yangu, bibi yangu apate hela ya marejesho na baba na mama wapate hela ya ada ya shule. Mungu atusaidie, Milele Amina amefanya maajabu jina lake liimidiwe" ameandika mtoto ambaye anadaiwa kujinyonga bafuni.

Chanzo cha tukio hilo bado hakijabainika mara moja, huku tukio hilo likiacha majonzi makubwa kwa familia, ndugu na wakazi wa eneo hilo.

View attachment 3537053
RIP Lightness.

Imani ya Mungu inechangia kifo hiki.
 
Back
Top Bottom