Traxtion
JF-Expert Member
- Dec 10, 2021
- 6,897
- 14,221
Kufuatia tukio la mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari Murieti Jijini Arusha, aitwae Daniel Jeremia (15), kutoweka nyumbani kwao January 26, 2026, nakuacha ujumbe unaosema kuwa anamuonea mama yake huruma kwa namna anavyomuhangaikia maishani, hatimaye leo January 31, amepatikana na kusema alikuwa anafanya kazi za kubeba mizigo maeneo ya stendi na sokoni ili siku moja arejee kumsaidia mama yake aliyemuacha akiwa anaumwa.
"Niliondoka mama alikuwa anaumwa, tulikuwa hatuna hela ndani ikabidi aende tu hivyo hivyo kazini tu, hicho kitendo kikaniuma, anateseka kisa mimi, nilikuwa nimeenda tu pale stendi nilikuwa nabeba tu mizigo, nalala hapo hapoo, ningerudi tu nikishapata ela yakumsaidia mamaa" Mtoto Daniel akizungumza na mwandishi wa GADI TV kupitia simu ya mama yake huku akiwa analia.
Mama mzazi wa mtoto huyo amekiambia chombo cha habari "GADI TV" mwanae amepatikana baada mtu mmoja kumuona maeneo karibu na Kituo Kikuu cha Polisi Jijini humo na kisha kufananisha picha zilizokuwa mtandaoni, na alipohojiwa alikiri kuwa ni yeye.
Source: GADI TV
"Niliondoka mama alikuwa anaumwa, tulikuwa hatuna hela ndani ikabidi aende tu hivyo hivyo kazini tu, hicho kitendo kikaniuma, anateseka kisa mimi, nilikuwa nimeenda tu pale stendi nilikuwa nabeba tu mizigo, nalala hapo hapoo, ningerudi tu nikishapata ela yakumsaidia mamaa" Mtoto Daniel akizungumza na mwandishi wa GADI TV kupitia simu ya mama yake huku akiwa analia.
Mama mzazi wa mtoto huyo amekiambia chombo cha habari "GADI TV" mwanae amepatikana baada mtu mmoja kumuona maeneo karibu na Kituo Kikuu cha Polisi Jijini humo na kisha kufananisha picha zilizokuwa mtandaoni, na alipohojiwa alikiri kuwa ni yeye.
Source: GADI TV