Ngongo
Platinum Member
- Sep 20, 2008
- 21,204
- 37,555
Mkuu jmushi1.
Mkuu ninaweza jadiliana na wewe kwakuwa najua uwezo wako ni wajuu sana.
[1] Mkuu jmushi,Lema kashtakiwa Mahakamani kwa makosa ya kufanya maandamano na mkutano bila kibali.
[2] Mkuu jmushi,Lema kapewa haki ya dhamana kosa lake lina haki ya dhamana kagoma kutumia haki ya dhamana.
Nianze na hili la kwanza nina amini mashtaka dhidi ya Lema na wapenzi wake yangepanguliwa mahakamani bila shida yoyote kwasababu mazingira kwamba alifanya maandamano bila kibali ni rahisi sana kujitetea ila hili la kufanya mkutano bila kibali sijui mazingira yakoje ingawa pia kwa nafasi yake ya ubunge siamini kama atakosa utetezi.Kwa ujumla suala lote lingemalizwa kimahakama zaidi kuliko kisiasa.
Nije kwenye suala la pili mheshimiwa mbunge kapewa dhamana kakataa kabisa,kaamua kwa hiyari yake kwenda magereza sijui anataka kufungua matawi huko gerezani au anatafuta wanachama wapya kwa kweli anajua mwenyewe na wapambe wake.Sina tatizo na uamuzi wa Lema kukataa dhamana hata kidogo anajua anachotaka yeye,chama chake na wafuasi wake.
Tatizo langu nikuhamishia hili tatizo kwa wananchi tena wananchi wa kipato cha chini.Mwananchi huyu tayari ana mzigo mkubwa vyakula vimepanda bei,vifaa vya ujenzi ndiyo usiseme,thamani ya shilingi yetu kila kukicha inazidi kushuka thamani dhidi ya dola bado wanasiasa wenye kufikiria maslahi yao tu wanaona ni vyema kabisa kushawishi,kushinikiza na kusimamia zoezi la mgomo wa daladala ?.Tukiendelea na mtindo huu iko siku akigombana na mke wake mtashinikiza maduka yote yafungwe.
Mkuu ninaweza jadiliana na wewe kwakuwa najua uwezo wako ni wajuu sana.
[1] Mkuu jmushi,Lema kashtakiwa Mahakamani kwa makosa ya kufanya maandamano na mkutano bila kibali.
[2] Mkuu jmushi,Lema kapewa haki ya dhamana kosa lake lina haki ya dhamana kagoma kutumia haki ya dhamana.
Nianze na hili la kwanza nina amini mashtaka dhidi ya Lema na wapenzi wake yangepanguliwa mahakamani bila shida yoyote kwasababu mazingira kwamba alifanya maandamano bila kibali ni rahisi sana kujitetea ila hili la kufanya mkutano bila kibali sijui mazingira yakoje ingawa pia kwa nafasi yake ya ubunge siamini kama atakosa utetezi.Kwa ujumla suala lote lingemalizwa kimahakama zaidi kuliko kisiasa.
Nije kwenye suala la pili mheshimiwa mbunge kapewa dhamana kakataa kabisa,kaamua kwa hiyari yake kwenda magereza sijui anataka kufungua matawi huko gerezani au anatafuta wanachama wapya kwa kweli anajua mwenyewe na wapambe wake.Sina tatizo na uamuzi wa Lema kukataa dhamana hata kidogo anajua anachotaka yeye,chama chake na wafuasi wake.
Tatizo langu nikuhamishia hili tatizo kwa wananchi tena wananchi wa kipato cha chini.Mwananchi huyu tayari ana mzigo mkubwa vyakula vimepanda bei,vifaa vya ujenzi ndiyo usiseme,thamani ya shilingi yetu kila kukicha inazidi kushuka thamani dhidi ya dola bado wanasiasa wenye kufikiria maslahi yao tu wanaona ni vyema kabisa kushawishi,kushinikiza na kusimamia zoezi la mgomo wa daladala ?.Tukiendelea na mtindo huu iko siku akigombana na mke wake mtashinikiza maduka yote yafungwe.
Ngongo,mimi nilidhani bifu lako ni kwa Lema tu,kumbe ni kwa harakati nzima za kutaka mabadiliko?
Yani ni sawa na kutaka kuwanyima watu wasile chakula kwasababu tu hukushiriki kukipika?Unataka wafe njaa?
Nadhani umenielewa....Kuwanyima watu mabadiliko kwasababu ya Lema?Kwa hapa JF ninakumbuka kuwa wewe ni NCCR,na ukweli bifu lako na Lema ni linanikumbushia bifu la Mrema na Ndesamburo.
Mkuu ukimpinga Lema,hilo hakuna atakayeingilia,lakini unapokuwa against mabadiliko na huku ukijiita mependa mabadiliko,then ni sawa na usaliti si tu kwa wenzako,bali hata kwa nafsi yako.
Nina uhakika kabisa kuwa kuna namna ungeweza kuplay your game smart,hata hivyo hakuna anayeweza kukupangia,only ushauri tu mkuu.
Style ya bora tukose wote siyo nzuri especially kama madhumuni ni kumwodoa mkoloni mweusi.
Ugombeaji wa fito kwenye ujenzi wa nyumba moja kunaweza kuleta madhara.