Crashwise
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 22,227
- 8,735
Ilikuonyesha kumuunga mkono kamanda Godbless Lema, madereva wa daladala na Toyo kesho wataanza mgomo hapa Arusha....
=======
=======
Wito wa mgomo na maandamano ya kupinga Ukiukwaji wa Katiba, haki za Binadamu, ukatili wa police na udhalilishaji wa serikali kwa raia hapa nchini na hasa hapa Arusha. Damu ya mashujaa iliyomwagika kudai Uhuru, haki Uzalendo wa taifa iwe WINO wa kuasisi Taifa jipya.
Jasho la mateso na unyanyasaji liwe ISHARA ya utumwa wa mzawa ktk taifa lake na CHOZI la uchungu wa Umaskini, maradhi, ujinga na ufisadi liwe NISHATI ktk kuwasha taa ya HEKIMA, UJASIRI na NGUVU ya UMMA kuleta mapinduzi ya Kiraia.
KULAANI NA KUPINGA OCD-ARUSHA KUWAITA WANANCHI "PANYA".
Nawasilisha!
Last edited by a moderator: