Arusha city Geneva ya Afrika imegeuka Mogadishu ya Tanzania

Barbarosa

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
22,584
27,786
Serikali yetu imechangia kuuwa mji wa Arusha, kwa nini walijenga ukumbi wa Nyerere Dar wakati tayari AICC ipo ? AICC ilikuwa ni chanzo kikubwa sana cha Uchumi wa Arusha City baada ya UN, sasa UN wameondoka, AICC Mikutano hakuna kwa maana yote inafanyikia Dar unajiuliza kwanini waliamua kujenga huu ukumbi wa Mikutano Dar kwangu mimi ni fumbo, unawezaje kujenga uchumi wa Tanzania wakati unabomoa uliopo?

Sasa hivi Arusha Hoteli zinafungwa hakuna kitu, fikiria tu kwa mfano kwa kawaida Mkutano mkubwa kama wa SADC ungefanyikia Arusha City lkn ulifanyikia Dar sababu ya ukumbi wa Nyerere.

Dar tayari ni mji tajiri Tanzania hivyo hakuna haja tena ya kuipora Miji mingine chanzo cha mapato au mnataka Tanzania nzima wahamie Dar au vipi? Nilisafiri ktk Dar -Arusha inasikitsha sana, baada ya kukata kona ya Segera -Moshi-Arusha tu ni kama unaenda kijijini hakuna magari kabisa na ni mpaka Arusha, zamani hii barabara ilikuwa imejaa magari.

Bill Clinton aliita Geneva ya Afrika alipofika Arusha City leo hii hakuna kitu

AICC enzi za uhai wake, RIP ukumbi wetu.

1607712529290.png


1607712340200.png
 
Ndiyo ubaya wa nchi kuwa centralized. Ili uendelee lazima makao makuu wakurehemu.

Sidhani kama hilo ni tatizo mbona miaka yote tulikuwa ni centralized lkn bado AICC ndiyo uliokuwa ukumbi pekee wa Mikutano ya Kimataifa Tanzania hivyo kama Mkutano mkubwa wa Kimataifa ulifanyika Tanzania ndege zote zilielekea Arusha City, hata kama ni Raisi wa USA alitua KIA, leo hii wameleta Dar, tena cha ajabu ukumbi wa Mwalimu Nyerere wamejenga sehemu ambayo ni ya eneo la wazi, wamemega Gymkhana tena kama Sheraton walivyofanya .
 
Sidhani kama hilo ni tatizo mbona miaka yote tulikuwa ni centralized lkn bado AICC ndiyo uliokuwa ukumbi pekee wa Mikutano ya Kimataifa Tanzania hivyo kama Mkutano mkubwa wa Kimataifa ulifanyika Tanzania ndege zote zilielekea Arusha City, hata kama ni Raisi wa USA alitua KIA, leo hii wameleta Dar, tena cha ajabu ukumbi wa Mwalimu Nyerere wamejenga sehemu ambayo ni ya eneo la wazi, wamemega Gymkhana tena kama Sheraton walivyofanya .
Si ndiyo serikali ya muda huo ilikuwa inawarehemu. Sasa imeacha kuwarehemu. Tungekuwa hatuko centralized hivyo ungeshangaa mameya wanapeleka bids za kuandaa mkutano. Anayeshinda anachukua hata kama ni Sumbawanga au Tunduru.
 
Hatujui kujenga uchumi, huo ndiyo ukweli ni lazima tujifunze, AICC ilikuwa inasaidia sana uchumi wa huo Mji hata kuufanya tu ujulikane nje ya Tanzania kama Mikutano mikubwa ingefaynikia huko, fikiria enzi za Mandela kama msuluhishi wa Rwanda/Burundi Mzee Mkapa (RIP) alikuwa anafanyia Mikutano AICC Arusha City, Mikutano mikubwa ikienda Arusha Uwanja wa ndege wa KIA unatumika unajaa ndege na wageni hii ingesaidia sana uchumi wa huko, sasa kila kitu wamehamishia Dar, Dar ambayo tayari ina vyanzo vya kutosha vya mapato, ...
vipaumbele😂
 
Back
Top Bottom