Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Siku ya pili yamechukua ubingwa hakuna lolote lililotoke....hayajui hata kushangilia dadekiii.....timu ndogo ni timu ndogo tu
Angalia image hizi 3, kisha sema ipi timu na ipi ndogo popoma wee.

1- viva arsenal 🔥
FB_IMG_17793535405832557.jpg



2 - city uchwara
FB_IMG_17793535287006101.jpg

3- liver kuku
FB_IMG_17793535326269676.jpg
 
Wadau wa Gunners hongereni sana hasa wale die hard fans kama Castr , arsenal2004 mkorea Will Jr na mwanangu HENRY14 pamoja na wengine wote ambao hamkuionea aibu timu yenu hata ilipokuwa inapitia nyakati ngumu zaidi.

Kama mnavyojua furaha ya mpira inakuja unapokuwa na mnyonge zaidi yako, hivyo kwa fans wa timu pinzani. arsenal ilikuwa timu inayofurahisha kutaniwa kutokana na rekodi zake kwenye mbio za mataji makubwa.


Kusema kweli tumehuzunika sana kwa jana kuchukua moja ya mataji makubwa ila hatuna namna tarehe 30 tutakuwa dhidi yenu ili tuendeleze utani wetu wa jadi maana tofauti na hapo pataboa sana humu na mtarudi kuwa mateka wa hamis77 kabla Flano hajaja kuwaokoa na mbwembwe zake za inverted pressing ambazo hazikuzaa matunda hadi mlivyorudi kwenye LOW BLOCK ila mkaibatiza jina la kiutaalam kuwa ni HARAM FOOTBALL
Shukran mkuu.
Sasa tufurahi kwa muda mpaka tarehe 30 na tukiweza kubeba UCL tutambe mpaka ma aliens kule Mars na Jupiter watutambue kuwa sisi ndiyo mabingwa.
 
CONGRATULATIONS KIBAO SANA KWETU ZE GANAAAAAAZ.

KUMBE JF IPO,

Nilikuwa nashindwa kuingia mpaka nikakata tamaa. Ila sasa naona tupo hewani. Akina Flano na Labyrinth 84 lazima watutambue sisi ni nani.

Flano najua amekuwa anatamani kuhamia chama hili kubwa muda mrefu sema tu kikombe kilikuwa kinamzuia ila sasa tumekipata jamaa atazamia kwetu mazima.

Labyrinth 84 najua alijidanganya kuhamia kwa wale wahuni wa Newcastle ila najua tayari amesharudi huku kwetu. Hongera sana kaka. Sasa na wewe ni bingwa wa Ligi Kuu Uingereza, siyo tu kile ki Carabao. Kile kikombe hata sisi tulifika fainali msimu huu ila tu tukazingua tukaanguka kwa yule ambaye tumempiga bao na kuchukua ubingwa mbele yake. Kwa kifupi tumebeba kombe kubwa zaidi na huenda tarehe 30 May tutachukua lingine mbele ya akina Dembele na Hakimi.

Yaani kwa sasa duniani hakuna chama kubwa kama ARSENAL!!!
 
Hongereni sana wanangu wa Arsenyau kwa msaada wa VAR kufanikiwa kubeba English Corner Trophy msimu huu.
Hii ni fedheha kubwa mno kwa ulimwengu wa Soccer. View attachment 3591885
Kama rahisi na ww beba mkuu....nyny ni makubwa jinga ya hivi sasa...mara ya mwisho kubeba ligi mabomu ya gongo la mboto ndo yalikuwa yanalipuka...kazeni miguu msimu ujao....ila UEFA itakuwa na majina ya ajabu msimu ujao....Mbeumo sijui Dialo mara Kunya huku Kobe Mauno....yaani vurugu tafrani
 
CONGRATULATIONS KIBAO SANA KWETU ZE GANAAAAAAZ.

KUMBE JF IPO,

Nilikuwa nashindwa kuingia mpaka nikakata tamaa. Ila sasa naona tupo hewani. Akina Flano na Labyrinth 84 lazima watutambue sisi ni nani.

Flano najua amekuwa anatamani kuhamia chama hili kubwa muda mrefu sema tu kikombe kilikuwa kinamzuia ila sasa tumekipata jamaa atazamia kwetu mazima.

Labyrinth 84 najua alijidanganya kuhamia kwa wale wahuni wa Newcastle ila najua tayari amesharudi huku kwetu. Hongera sana kaka. Sasa na wewe ni bingwa wa Ligi Kuu Uingereza, siyo tu kile ki Carabao. Kile kikombe hata sisi tulifika fainali msimu huu ila tu tukazingua tukaanguka kwa yule ambaye tumempiga bao na kuchukua ubingwa mbele yake. Kwa kifupi tumebeba kombe kubwa zaidi na huenda tarehe 30 May tutachukua lingine mbele ya akina Dembele na Hakimi.

Yaani kwa sasa duniani hakuna chama kubwa kama ARSENAL!!!
Roho inauma kinoma huku mtaani tunaishi kwa shida sana, ila sio mbaya furaha yetu tumemuachia PSG tunajua hawezi kutuangusha.
1779371733294.jpg
 
Mkuu fuentte Nashangaa mpaka saivi, sijamwona Aaron Arsenal. Au tuseme ana multiple ID, jamaa ni moja ya die hard fans wa arsenal. Kwa kupitia michango yake mingi, kwenye hili jukwaa. Alikua sio tu mchambuzi wa mpira, Yani alikua na zile pigo za kiutafsiri, kama marehemu mkandala lufufu. Aliyekuwa mtafsiri wa action movie hasa kipindi cha mikanda ya (VHS). Aliponikosha sasa hadi kwenye masuala ya dini jamaa yumo.

Sijui ndio huyu huyu, hamis77 masingeli. A.K.A kiraka kinachofiti kila sehemu, kuanzia kwenye mpira,dini na jukwaa la kimataifa. Sio kwa ubaya, niseme tu baadhi ya mashabiki wa arsenal, huwa mnaishi kwenye dunia yenu ya kipekee. Hawa watu inatakiwa warudi, na waendelee na michango yao kwenye ili jukwaa.

Mkuu tarehe 30, nikiwa kama mshabiki mwenzako wa man Utd, nitakua upande wa arsenal.
Walikuwa wengi sana ila shid ilikuja kwamba ukienda tofauti na mtizamo wa masingeli, anakuundia zengwe kiasi kwamba jukwaa zima wanakuona mamluki wa timu. Wengine wengi waliamua kujitoa jukwaani sababu ya masingeli, jamaa alikuwa mtemi sana kwenye huu uzi
 
Walikuwa wengi sana ila shid ilikuja kwamba ukienda tofauti na mtizamo wa masingeli, anakuundia zengwe kiasi kwamba jukwaa zima wanakuona mamluki wa timu. Wengine wengi waliamua kujitoa jukwaani sababu ya masingeli, jamaa alikuwa mtemi sana kwenye huu uzi
Hata Aaron arsenal nae alikua mtemi sijui ndio huyu huyu masingeli.
 
Back
Top Bottom