Naam kuanzia sasa hamtaitwa false hopers tena Bali champions.
Nadhani nyinyi ndo mashabiki bora zaidi kuliko mashabiki wa team yoyote Ile , nyinyi ni real true fans wa arsenal.
Miaka 22 mmekuwa loyal fans wa arsenal pasipo uwepo wa kombe lolote kubwa (EPL & UEFA) na mkaendelea kuamini na kuisapoti Arsenal.
YOU DESERVE THIS WAZEEE NYINYI NI CHAMPIONS!
Mkuu, umeongea jambo la maana sana yaani ukiwa shabiki wa timu kama Arsenal yakupasa kutokata tamaa.
Nilipokua pale London mwaka 2004 niliona jinsi Invicibles walivyonyakua kombe lile pale Highbury Islington nahodha akiwa Patrick Vieira.
Lakini kuna kitu Arsene Wenger alifanya nacho ni kuishawishi bodi kuingia benki na kuchukua mkopo wa milioni 300 kujenga uwanja mpya wa Emirates.
Lakini Arsenal ikayumba uwanjani huku Wenger akishindwa kusajili wachezaji wa maana akawa akisajili wachezaji kwa mkopo. Wachezaji wengine walikuwa na kiwango cha chini sana akina Yaya Sanogo, yule beki wa hovyo alieitwa Schuilachi na wengine.
Angalieni yanowapata Tottenham Hotspurs wameiga kuchukua mkopo na sasa watishiwa kushuka daraja.
Hivyo Arsenal kumaliza deni la benki kwa muda ulopangwa na pesa kuanza kuingia zikiwemo kuuzwa kwa yale majengo pale penye uwanja wa zamani Highbury, Arsenal sasa wana pesa na waweza kusajili mchezaji yoyote wakitaka.
Tiyari mipango ipo mbioni bwana Andrea Beta yupo sokoni na kuna wachezaji wa kufuatilia kama Tijjani Reijnders wa Manchester City ambae atagharimu kama pauni milioni 45 hivi na Bdadley Barcola wa PSG ambae nae Arsenal wamemweka kwenye "Radar".
Na wapo wachezaji kama Gabriel Jesus ambae huenda akarudi Brazil kwenye timu ya Palmeiras na Jose Mourinho ataka kumsajili Gabriel Martinelli.
Beki Piero Hincapie atasajiliwa rasmi baada ya kuchezea Arsenal kwa mkopo kutoka Bayern Leverkusen. Declan Rice nae ambae apata mshahara wa pauni 240,000 kwa wiki na Julian Timber ambae mshahara wake ni 90,000 kwa wiki mikataba yao itaboreshwa (fresh Terms) ili kuendana na hadi ya kubwa bingwa wa ligi kuu ya UK.
Hivyo wana Gunners, mie Richard ambae nilkuwepo mwaka 2004 leo nipo na ntakuwepo.
Balantanda, BAK, Steve D na wengine karibuni hapa jukwaani tushereheke ubingwa wa baada ya miaka mingi ya maumivu.
COYGs