Siku hizi sio Mimi mchangiaji kwenye hili jukwaa lakini nitatoa maoni yangu kwa hii timu
Kosa la Arsenal ni kumuacha Partey aondoke, hili linaweza kuwakosesha makombe
Pili, huwezi kupata rhythm ya mchezo kwa kubadilisha midfielder kwa midfielder
Kukosa uoni wa kutafuta striker
Umakini wa goalkeeper
Ujuaji wa coach
Kosa la Partey ni kubwa kuliko linavyotizamwa, huwezi kusubiri mpaka mwaka wa mwisho ndio ujadili mkataba wa mchezaji muhimu, case ya kubaka ya Partey kwa uoni wangu ni kumkomoa Partey kwa kutokubaliana na mkataba
Partey akicheza kati ilikuwa rahisi kwa Rice kufanya majukumu mengine lakini Zubimendi itamchukua muda mrefu na mazoezi magumu ya kuhimili ligi ngumu ya premium
Kubadilisha midfielder inahitaji maarifa kabla ya kubadilisha, ili kuweza kupata rhythm ya mchezo kulikuwa na ulazima kumtoa Martineli na kumuingiza midfielder aweze kucheza na Merino mpaka apate speedy ndio onamtoa Merino
Striker bado ni tatizo kwa Arsenal, Gyokeres sio ufumbuzi na ikiwa Arteta anafikiri amepata suluhisho tutakuja kuona mwisho wa msimu Gyokeres amefunga magoli mangapi
Goalkeeper ni nafasi ina lawama nyingi unapokosa umakini kwa sekunde tu, tayari utoe mpira wavuni, Raya anarejea makosa
Ujuaji wa coach ni mkubwa, binafsi ninampenda Maurinho kwa falsafa zake za ushindi
Hii team akipewa yeye haitochukuwa muda kupata makombe lakini Arteta itategemea bahati, inawezekana falsafa ya uongozi wa team sio kipaumbele chao
Ahsante