Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Nacheka sana nyumbu wanavyogombana kisa kutosajili
Ni mwanzo wa July. Siyo muda wa kujistress sana japo timu zinaweza kuonekana kama hazifanyi kitu. Huku kwetu sisi wenyewe tulikuwa tunastress na bado tunastress kuhusu sajili. Hata pale tulipojua tumeshamchukua Zubimendi, watu walipata wasiwasi kuwa Madrid wanaweza kumchukua. Watu walibidi wahakikishiwe kuwa jamaa tumempata May ila hatutamtangaza mpaka July kwa sababu za kifedha ila haikusaidia sana kuwapa amani. Na mpaka sasa bado tunastress maana kama mashabiki tunataka tuwe tumeshamaliza kusajili na kuuza wachezaji ili tuwe tuanawatambia na kuwapiga biti akina Nyumbuz na Chelkenge na kuwaonya wasiingize timu uwanjani ila hatuoni hizo sajili mapema...

Manyumbu watulie tu. Sajili zitakuja tu.

Cha muhimu ni waelewe kuwa sajili zao hazitawasaidia chochote. Bado sisi na timu zingine tutaendelea kujipigia na kuchota points 6 au zaidi kwao kama kawa.
 
Kuna hiki kitoto kipo Spain namba 10, kinachezea Barcelona, Vicky Lopez. Tukikipata Arsenal, tutachukua makombe yote. Kinajua football
 
na wale wanaosema kwamba mwaka huu arsenal mwaka huu asipotwaa kombe kibarua cha arteta kitakuwa mashakani sio kweli,kwanza wamiliki wa arsenal wanajua arteta msimu uliioisha ndio kaingiza pesa nyingi kuliko timu yoyote ya EPL kwahyo kazi yake ipo secured
 
Kwangu ntaona usjali bora zaidi kama kweli tukimchukua rodry au EZE sisi timu yetu kimuundo haina tofauti na city au PSG,number tisa sio mchezaji muhimu,mfano mechi yetu na PSG martnel angekuwa mzuri kwa umaliziaji tusingetolewa nao,hatuaji tu magoli tunahitaji mfumo uliokamilika mbape kaongoza kwa magoli hispania lakin madrid hawakuwa na kombe
 
Ana magoal 7 kazidiwa na Kai magoal 3
Bakini naye

Screenshot_2025-07-07-21-21-03-294_com.twitter.android-edit.jpg
 
Fungu la kukosa nyie,,,, ! Arteta ana kimavi tangu akiwa mchezaji, hawezi kushinda kombe la maana
 
Sio kufeli kwani kipindi fabregas yupo Barca akawa hapati namba ya mara kwa mara kwani alikuwa mmbaya au ni kwasababu nafasi alikuwa anacheza ilikuwa ni ngumu kupata namba baada ya kuamia Chelsea akawa top assist. Kukosa namba sehemu Kuna sababu kuu mbili moja ni kusidiwa uwezo, mbili preference ya kocha kulingana na mfumo wake
Salah, chelsea alifeli,
Swali dogo tu angekuwa na moto ule wa Roma tu ama huu wa liverpool, nani angemuweka benchi!?
Hakuwa na kiwango bora hichi ..
 
Back
Top Bottom