



Masingeli banaaa, wewe kila siku unashinda kwenye jukwaa la Man Utd kule unaona kabisa jinsi demokrasia ilivyotamalaki yaani ni ruhusa kumpiga spana 7+3 Hag, tunapiga spana wachezaji, tunawapiga spana wamiliki na hakuna fans yoyote wa Utd ataethubutu kukutukana, kukukejeli wala kukubeza.
Kwa nini Masingeli hamtaki kuwapa watu uhuru wa kutoa maoni yao kwa upeo wa fikra zao?
Yaani humu mnataka Arsenyau wote mue na mtazamo mmoja unaofanana juu ya timu, mwingine akiwa na mtazamo tofauti kidogo tu mnamshambulia na kumuona ni mamluki?
Hebu jifunzeni basi hata kwenye majukwaa ya Chelsea, Liverpool au Man Utd namna watu wanavyo jadiliana kwa mitazamo tofauti.
Yaani humu mnataka watu wote wawe kama mang'ombe Masingeli akisema hivi basi watu wote wanafata, hebu badilikeni jamani zile zama za "Zidumu fikra za mwenyekiti" zishapitwa na wakati.




kuna watu wamepigwa marufuku humu hadi kumquote mtu.
#Poor Arsenyo