Kuhusu Man Utd kukosa uvumilivu na kubadili makocha kila wakati ndio sababu inayopelekea kukosa program endelevu hilo nakubaliana na wewe maana kila kocha anaekuja anakua na falsafa yake.
Ila kusema Arsenal ya sasa ni matokeo ya kuanza upya hilo nakupinga kwa nguvu zote,
Arsenal ya sasa ni Arsenal ileile ya miaka iliyopita ambayo tatizo lenu kubwa hua ni washambuliaji na walinzi makini, kikubwa ni sajili mbili hizi mlizozifanya za Zinny na Jesus zimesaidia kuziba madhaifu yenu ya muda mrefu.
Muhimu ni kuomba tu Jesus asije mapata majeruhi akakaa nje kwa muda mrefu, nina uhakika wa asilimia 90 Jesus akiumia kule mbele kutaendelea kua butu kama zamani kwa zile kosakosa za kina Nketiah.
Uwepo wa Jesus umeongeza ari kubwa sana kwenye safu ya ushambuliaji na timu kwa ujumla.
Flano , Arsenal sio ile Ile, tulimtimua auba ,na laca na timu ikaendelea kupata matokeo
Arsenal aliyoikuta Arteta ilikuwa hata pass 5 haiwez kupiga,Arsenal ya emery hiyo, ilikuwa kwa msimu mzima mech za away inashinda mechi 3-4 basi, mech za away inakaa nyuma .
Arteta akaanza kuisuka taratibu kwa kuondoa toxic players wote ,na wiki hii anamalizana na pepe ,
Kikosi alichokikuta wamebaki Saka aliyemkuta ni beki wa kushoto, XHAKA aliyekuwa anajiandaa kusepa, na Martinell ambaye Ni Usajiri was skauti ,
Kwahiyo ukisema Arsenal Ni ile Ile unakosea Sana, Arsenal tulifikia hatua mech za away hata na vibonde tunapelekewa Moto .
Kuhusu eneo la CF , Jesus kweli kaongeza kitu, lakin anachofanya Kocha anatawanya magori, magoli yanatokea pande zote ,kumbuka Arteta ni muumini wa pep ,
Jana Jesus hajafunga lakin chances zinatengenezwa nyingi ,anafunga kila mtu , pale CF Martinell ndio namba yake aliyekuwa anacheza Brazil na kufunga goli nyingi. Alipokuja Arsenal anatumika Kama winger , Na anachokitaka Kocha kwa CF kwanza u press , hiyo Kaz Nketiah anaiweza, japo hamfikii GJesus
Rebuilding ya Arsenal ilianza kwanza kwa kumpa Mamlaka yote Arteta ,Kisha wachezaji asiowataka awaondoe , now yupo mwishon kabisa ,
Kwahiyo hata hi sex football tunayocheza sio kwa bahati mbaya .