Wakulu,
Mambo hayakwenda kama ilivyopangwa.
Inajulikana Walcott na Alex Song hawakuweza kucheza mechi ile pale Nou Camp na Cesc Fabregas alicheza baada ya msuli kutuna tena na ndio maana hakuweza kucheza katika hali yake ile tumwonayo akichezea Arsenal.
Cesc Fabregas -the engine room was cold at Nou Camp
Walcott aliwachosha sana Barca pale Emirates na hata tukaweza kufunga magoli yale mawili. Hata hivyo Barcelona kama wangetumia nafasi walizopoteza pengine wangefunga magoli mengi. Kwahio ile kasi ya mchezo ambayo Arsenal ilitumia pale Emirates haikuwepo kule Nou Camp isipokuwa Jack Wilshere tu ndio alikuwa akijaribu na alifanikiwa kumpa mpira Nichlas Bendtner kwenye dakika ya 89 na kama kawaida yake badala la kuunganisha kupeleka wavuni akataka "second touch" na akazuiwa na beki.
Alex Song pale Emirates alisaidia kulinda back four na alifanya kazi hio kwa ufanisi mkubwa. Abou Diaby alishindwa kazi hio pale Nou Camp na alikuwa alipoteza mipira mingi sana kwa Xavi na pia alisababisha msongamano pale kwenye "midfield" na hatimae Barca wakafunga goli la tatu ambalo ndio liliwakatisha tamaa Arsenal.
Wakulu msiwe na wasiwasi kwenye ligi kuu Arsenal ina "game in hand" na tupo nyuma kwa 3 points tu na nina imani tutawafunga West Brom na Blackburn kupata 6 points.
Jumamosi tunawatoa Man Utd hata kwa goli 2 tu zitatosha.