On His Day...Partey ni Mnyama tena Mnyama Mkali Haswaaaa....
Tangu Msimu Uanze Hii ndo Big Game Tumeingia Tumeshiba Kila kitu Mbinu,Juhudi,Maarifa,na Kila Kitu kizuri ...Tulichokosa ni Ukatili Mbele ya Lango Lao...
How I Wish Hii Game Ingeisha Kipindi Cha Kwanza Tungetoka na Goli 2-0 ingekuwa Rahisi Kumeza Pressure na Kutulia na Kumiliki Mpira Zaidi..
Ahsante sana Referee na Team Nzima ya VAR ..mmejua Kutudhulumu Leo Kwa kiasi Chenu... Ile ya Gabriel Wangeweza Kuzima tuu kama foul ya kawaida game ingeendelea na ile penalty ya Odergaard wangeenda Kwenye VAR kuangalia pia...
Hii Game imethibitisha kuwa mfululizo wa matokeo tulivyokuwa tunapata haikuwa bahati Mbaya wala Game Rahisi ni Mabadiliko makubwa mno yamefanyika kwenye uwanja vya mazoezi..
Leo nimeishuhudia Arsenal Niliyokuwa Naitaman sana Tangu Arteta Amekuja..Yes hatuna Quality ya City wala Liverpool ila tunaweza kuingia na Game plan yetu nzuri na tukapambana na kuwapa Game ngumu team Yeyote..Sio Kinyonge kama Tulivyokuwa Mwanzo ...
Team Yetu Saivi Ukiiangalia kila idara imeunganishwa vyema imebaki kuongea Quality kwenye kila idara team itakuwa tam Hii kama Chupa ya Mirinda kwa Yule Dada..
Tumepoteza Game ila Tunajivunia Mengi katika game ya Leo na uzuri sio kila game tutacheza na City kwaio wale wa Size yetu tuhakikishe tunapata pointi za kutuweka pazuri