Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Furaha ya jana ilinizidi kiasi cha kwamba siku mtendea haki Fabianski kwa kusahau kumshukuru kutokana na perfomance yake nzuri sana.


Big up Fabianski na nategemea utapata confidence ya kufanya zaidi ya jana huko mbeleni.
 
...............Wenger was asked about Rooney.......................
Would you have liked to sign him for Arsenal?


.....................He answered........................
We never thought about it because we have enough people able to play up front. Moreover, if Manchester United are not able to pay his contract, Arsenal cannot even think about it.
 
...Rooney wamemkosa na kufungwa wamefungwa. Shukran mkuu Eqlypz...wiki ijayo muwaendelezee machungu hawa...
Tunacheza na City tarehe 10, ila weekend hii tuko na Spurs.
Fabianski akiendeleza hii form basi Almunia ana hali ngumu.
 
Tunacheza na City tarehe 10, ila weekend hii tuko na Spurs.
Fabianski akiendeleza hii form basi Almunia ana hali ngumu.

....REALLY? Basi hiyo game yenu na Citeh inavyonadiwa nilidhani mnacheza nao wikiendi hii,
Almunia kamroga WENGER, soon utamuona tena uwanjani.
Gaffer wetu ana maudhi kidogo?
 
Tuko pamoja wakuu kwenye kombe la mbuzi .


kikosi chetu:szcesny,eboue,djouro,koscienly,gibbs,denilson,eastmond,rosicky,walcott,bendtner na vela.
 
goooal tumpepata goli hapa baada kazi nzito sana. kasi ya mpira ni nzuri sana kwa pande zote ,wao wanajaribu kutukamata kwenye counter attack na sisi tunapiga mpira wetu.
 
Hey folks! I do not want upset anyone, but this is the fact. Arsenal won vs Man Citeh and Paul the Octopus dies of a heart attack. So sad in deed.
 
Walcot kapiga la pili hapa.goli lina utata kidogo linaonekana bendtner kamchezea rafu beki wa newcastle.
 
Naona Wenger ameamua kuditch policy ya kupanga watoto....!! Hii mechi yenu nimekosa dakika 60 za mwanzo.
 
Wenger vipi huyu? fabregas wanini sasa? mambo ya kwenda kuumia bila sababu na game ilivyokuwa physical noma sana.
 
watoto wote ambao wako katika next step ya first team wako onloan.
Babu ili kombe aliharibu Mourinho maana yeye alikuwa anafield wachezaji kibao kutoka kwenye first IX yake. Anyway hongereni kwa ushindi naona Aston Villa na West Ham nao wamepita.
 
Babu ili kombe aliharibu Mourinho maana yeye alikuwa anafield wachezaji kibao kutoka kwenye first IX yake. Anyway hongereni kwa ushindi naona Aston Villa na West Ham nao wamepita.

tusbiri draw tuone itakuwaje hawachelewi kutupanga na nyinyi lol.
 
Wakuu nini utabiri wa leo kwenye mechi yetu ya nyumbani Emirates?
Kwa kufananisha ki-uwezo (on paper) kila mtu anategemea tutashinda kwa idadi nyingi ya magoli, lakini mimi ninatia wasiwasi kidogo, kwa vile hii ni derby game na W/ham watakuja na staili ya "route 1 football" (4-5-1) formation.
Watapaki basi kule nyuma (defending deep) kuweka msongamano pale kati (5 midfield) na kutegemea mashambulizi ya (counter-attack) kwenye kila nafasi ni long ball kwa (lone striker) Carlton Cole
Hizi timu ndogondogo zinajua kwamba ukicheza staili hii inakuwa vigumu na ni njia pekee ya kuwa-frustrate Arsenal, kwani sistimu yetu ni pasi-pasi hadi goli.(Nobody try long range SHOT!!!:A S angry🙂

Lakini pia inatia moyo kwamba Cesc atacheza, ni yeye peke yake mwenye uwezo wa kuifungua difensi kwa kuweka pasi za usahihi behind the defenders. Utabiri wangu ni tutashinda (3-1) half-time (1-1) magoli 2 tutapata kwenye dakika 20 za mwisho baada ya kuchoka kwa W/ham defenders.
Ningependa timu ya leo iwe:

Fabianski –
Sagna, Squillaci, Koscielny, Clichy –
Song, Cesc, Denilson –
Walcott, Chamakh, Nasri.
 
Back
Top Bottom