OG anaenda chelsea David luiz anaingia arsenal,Abu keshapima tayari,Mavnoplas anaingia naye kuimarisha ulinzi.
Yaani sasa ile arsenal iliyomaliza ligi bila kupoteza rekodi inayotamba duniani na haijavunjwa huenda ikatokea.
Bellerin beki ya kulia ,kushoto monreal,mustafa mvunja miguu anafuata,Luiz anatulia kati.Daaah yaani eti laurent sub,metesacker,holding .
Kati hapa anakaa granit xchaka zulu na wilshere hapo ramsey anasugua bench,mipira yote ya nyuma kulia mbele atapokea Ozil kwa bellerin au wilshere anamtengenezea assist Abu na lacazate sasa mhitaryan hatazeeka mapema maana mashetani yalitaka kumuua kwa kumkimbiza ovyo tulia hapa tunahesabu gonga tu hadi ndani ya sita zinapigwa gonga unashitukia gooooooooooooal beki zimegongana na kujifunga zenyewe.
Jamani tuombe uzima toten watakaa,mashetani nao watakaa tuu hakuna beki wa kumkaba Abu na laccazate pale.Man city yeye asubiri maumivu tuna hasira na ushenzi wa refa aliowabeba.
Vikosi viwili imara sasa vimepatikana.
Sanchez man itakuwa kama yanga na okwi walivyopeana talaka.
Karibuni arsenal kwa kandanda la adabu pasi za kasi na uhakika.
Mungu ibariki arsenal,tubariki na mashabiki wake popote tulipo.